Habari za michezo
Zahera alichukua nafasi ya Mrundi, Joslin Bipfubusa aliyetimuliwa Oktoba 26, mwaka jana kutokana na matokeo mabovu na alikiongoza katika michezo saba ya Ligi Kuu akishinda pia miwili tu na kupoteza mitano.
MSHAMBULIAJI LIGI KUU AWEKA WAZI…WANASUBIRIA MIUJIZA ITENDEKE…AMEZUNGUMZA HAYA
MSHAMBULIAJI wa Polisi Tanzania, Ambrose Awio ameweka wazi kikosi hicho kinahitaji miujiza kubaki Ligi Kuu Bara kwa msimu ujao baada ya kupoteza kwa mabao 3-0 juzi dhidi ya Singida Big Stars kwenye Uwanja wa Liti.
Akizungumza na SOKA LA BONGO, Awio alisema kwa hali ilivyo ni ngumu kwao kutokana na wengi wao kukata tamaa ila wataendelea kupambana katika michezo yao minne iliyosalia ili angalau waangukie kwenye mechi za Play-Off’.
“Kitendo cha kupoteza kinashusha sana morali ya timu na ndicho kitu ambacho kinatukumba kwa sasa, ni wazi tuna kazi kubwa ya kufanya kupata hata hiyo nafasi ya kucheza michezo ya mchujo kama hatutaongeza bidii.”
Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.