Mwinyi Zahera Kocha wa Polisi Tanzania
Habari za michezo

MSHAMBULIAJI LIGI KUU AWEKA WAZI…WANASUBIRIA MIUJIZA ITENDEKE…AMEZUNGUMZA HAYA

Marce Ben Komba April 10, 2023 3:25 pm

MSHAMBULIAJI wa Polisi Tanzania, Ambrose Awio ameweka wazi kikosi hicho kinahitaji miujiza kubaki Ligi Kuu Bara kwa msimu ujao baada ya kupoteza kwa mabao 3-0 juzi dhidi ya Singida Big Stars kwenye Uwanja wa Liti.

Akizungumza na SOKA LA BONGO, Awio alisema kwa hali ilivyo ni ngumu kwao kutokana na wengi wao kukata tamaa ila wataendelea kupambana katika michezo yao minne iliyosalia ili angalau waangukie kwenye mechi za Play-Off’.

“Kitendo cha kupoteza kinashusha sana morali ya timu na ndicho kitu ambacho kinatukumba kwa sasa, ni wazi tuna kazi kubwa ya kufanya kupata hata hiyo nafasi ya kucheza michezo ya mchujo kama hatutaongeza bidii.”

Kwa upande wa kocha msaidizi wa timu hiyo, John Tamba alisema michezo minne iliyobaki itatoa taswira yao kwa msimu huu hivyo wanahitaji kupambania pointi 12 ambazo anaamini wakizipata zitawaweka kwenye sehemu salama.

Tangu kikosi hicho ateuliwe, Mwinyi Zahera kukifundisha Desemba 2, mwaka jana kimeshinda michezo miwili tu kati ya 12 ya Ligi Kuu Bara aliyokiongoza huku minne akitoa sare na sita yote iliyosalia akichezea kichapo.

Zahera alichukua nafasi ya Mrundi, Joslin Bipfubusa aliyetimuliwa Oktoba 26, mwaka jana kutokana na matokeo mabovu na alikiongoza katika michezo saba ya Ligi Kuu akishinda pia miwili tu na kupoteza mitano.
Katika michezo 26 iliyocheza hadi sasa imeshinda minne tu, sare saba na kupoteza 15 ikiwa mkiani na pointi 19.

MFAHAMU SHABIKI HUYU KIPOFU WA SOKA…HAJAWAHI KUKOSA UWANJANI YANGA YAIPASUA KICHWA SIMBA…YAFANYIWA FIGISU KUBADILISHIWA UWANJA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply