Shirika la Umeme (TANESCO) limesema baada ya Majenereta ya Uwanja wa Taifa kushindwa kufanya kazi katikati ya mechi ya Yanga vs Rivers United ya Nigeria na taa kuzimika, umeme wa TANESCO ndio ulianza kutumika na mchezo ukaendelea.
Umeme huo ulikatika kwa takribani dakika 20 wakati mchezo ukiwa dakika ya 24 na kufanya refa kusimamisha mchezo huku wachezaji wakilazimika kusubiri hali irejee kawaida ili mchezo uendelee.
“Tunasikitika kwa kadhia iliyojitokeza na tutashirikiana na wenzetu kwa siku za usoni jambo hili lisijirudie, Uwanja wa Taifa unahudumiwa na vyanzo viwili vya umeme ambavyo ni TANESCO na Majenereta ya uwanja, mechi ya leo uwanja ulikuwa unahudumiwa na majenereta ya uwanja” TANESCO.