Home Habari za michezo KAIZER CHIEF WAGOMEA MASHARTI YA NABI….KUMBE ALITAKA KUWACHUKUA MAKOCHA WOTE YANGA…

KAIZER CHIEF WAGOMEA MASHARTI YA NABI….KUMBE ALITAKA KUWACHUKUA MAKOCHA WOTE YANGA…

Habari za Yanga leo

Kocha Nasredine Nabi ameng’oa nanga Jangwani amegoma kuongezewa mkataba mpya na uongozi ukamtakia kila kheri tayari ameanza mazungumzo Kiaizer Chief ambayo alihisihwa nayo kablya kuaga Jangwani.

Hata hivyo, bado miamba hiyo ya Afrika Kusini wameendelea kunolewa na kocha wao Arthur Zwane, ingawa uongozi wa timu hiyo unataka kufanya mabadiliko ya haraka kabla ya msimu mpya kuanza.

Inafahamika kuwa kocha Nasreddine Nabi ameshapewa ofa na Kaizer Chiefs lakini bado hawajafikia muafaka kwenye suala la idadi ya wasaidizi wake ambao yeye amependekeza wote wapya.

Nabi amewaambia anataka kwenda na Kocha Msaidizi, Kocha wa Makipa pamoja na mtu wa video na inaripotiwa siku yoyote wiki hii atatua Sauzi kumaliza dili.

Habari zinasema kwamba Kaizer wanataka atumie baadhi ya waliopo lakini Kwa malengo waliyompa anasita kama ni watu sahihi wakupambania makombe.

SOMA NA HII  SIMBA NA TEMBO KUMALIZANA RASMI KESHO....NI 'SHOW YA MBUGANI' HII...