Kikosi cha Simba Msimu huu 23/24
Habari za michezo

KLABU YA SIMBA YAONDOLEWA KATIKA MASHINDANO YA LIGI KUU, ISHU IKO HIVI

Staff Desk August 8, 2023 12:11 pm

Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi (TPLB), Almasi Kasongo amesema waandaaji wa mashindano ya Super League wameomba klabu ya Simba itolewe kwenye ratiba ya Ligi Kuu Bara kuanzia Oktoba 20 hadi Novemba 21 kwa ajili mashindano ya kimataifa ya African Super League.

Almasi aliyasema hayo jana Agosti 7, 2023 alipokuwa akitangaza ratiba ya Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2023-24.

“Wameomba na ndio maana unaona michezo yao katika kipindi hicho tumeiwekea TBA, hivyo michezo yao watakuja kuicheza pale nafasi itakapopatikana,” alisema Kasongo.

Hivyo Simba, watasimama kwa takriban mwezi mzima kwenye Ligi Kuu isipokuwa mchezo mmoja wa dabi ya Kariakoo kati ya Simba na Yanga (Novemba 5) ambao kwa mujibu wa Kasongo, umeachwa tarehe hiyo mpaka pale Shirikisho la Mpira Afrika watakaposema vinginevyo.

KUHUSU ‘MWENYE UALBINO’ KUONEKANA SIMBA DAY…MAPYA YAIBUKA… YANGA WATAMBA KUNYAKUA UBINGWA WA AFRIKA ISHU IKO HIVI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply