Habari za michezo
MWAMBA HUYU HAPA ALIYEBADILISHA MCHEZO SIMBA vs AL AHLY
Staff Desk
October 21, 2023
11:37 am
Sadio Kanoute Putin mimi napenda kumuita Midfielder Dynamo.
To be honest kipindi cha pili kijana kabadilisha mchezo mzima…..kwanza kaongeza kasi ya mchezo,fujo kwenye pressing na urefu wa feet 6’2 kwenye box la Al ahly.
Kipindi cha kwanza Simba hawakuwa vizuri kwenye kuzuia kwani muda mwingi walikaba nafasi (zonal Marking) kwenye 4-2-3-1 mid-block kuliko kutembea na mtu (man 2 man marking) hivyo Al ahly walipata mianya mingi ya kupenya kati kati ya uwanja na kumsumbua mnyama.
Lakini kipindi cha pili baada ya Kanoute kuingia Simba walitoka kwenye Mid-block na kuanza kufanya High pressing kwa fujo kitu kilichopelekea Al ahly kufanya makosa mengi na kuruhusu goli mbili.
Heshima kwa Sadio Kanoute
Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.