Home Habari za michezo MANARA:- KWA YANGA HILI HALIJAWAHI KUTOKEA….KUNA WATU WAMEMDANGAJA MPAKA BALOZI..

MANARA:- KWA YANGA HILI HALIJAWAHI KUTOKEA….KUNA WATU WAMEMDANGAJA MPAKA BALOZI..

Habari za Yanga

Wengi mmeandika kuhusu Tuzo za CAF za mwaka huu, lakini kuna eneo mmeogopa kusema au mmesahau au pengine hamjui.

Toka tupate Uhuru Tanzania mwaka 1961,Hakuna Team yoyote ya mpira iliyowahi kuwania au kuingia katika kinyang’nyiro cha kuwania Tuzo ya team bora ya Afrika zaidi ya Yanga!!

Haijapata pia kutokea kwa Mchezaji aliyecheza team ya Tanzania kama @mayelefiston aliyekuwa @Yangasc , kuwa nominated kuwania Tuzo ya Best Player wa Afrika na pia mchezaji bora wa Afrika kwa Wachezaji wanaocheza ligi za ndani!!

Halikadhalika haijapata pia kutokea Kwa kipa anaecheza Ligi ya Tanzania kuwania Tuzo ya kipa Bora wa Continent zaidi ya @djiguidiarraofficial ambae anaenda kushinda hii Tuzo.

Kiufupi @yangasc imeihishimisha Nchi hasa, katika hili Makolo mtulie, Hammo katika ubora walionao Yanga hii , Yanga imefanya mambo makubwa ambayo hamjawahi hata kuyasogelea!!

Tulipokuwa tukiwaambia Robo Robo zenu hazilipi ndio hii sasa.mlikuwa mkijidai na Wachambuzi wenu wa Mpata Mpatae kuhusu Robo zenu, haya, kiko Wapi na zimewafikisha wapi?

Halaf linatokea jitu limeshiba Mafenesi na kande Mbichi eti linasema watani Zao ni Raja Casablanca na Ahly, sasa mmeona nani Level za Club ya Yanga!! Au kwa kushiriki lile Bonanza la naniliu? Mngekuwa moja ya Team bora Afrika mngekuwa Nominated katika hizi tuzo.

Nb:: Mkinuna natuma kombe lenu la Uongo mliomuonyesha Balozi wa Uingereza jana, SEMENI SU,,nimsanue Mh Balozi, mmemuonyesha kombe la ubingwa wakati nyi sio Mabingwa,,,hadi mzungu mnamuongopea Bata Wahed.

SOMA NA HII  KISA UDHAIFU WA REAL BAMAKO...MAYELE AIONA ROBO FAINAL CAF...