Home Habari za michezo MZEE WA JAMBIA AIKATAA YANGA KIMATAIFA….”WAKIFUZU ROBO FAINAL ITAKUWA BAHATI KWAO”…

MZEE WA JAMBIA AIKATAA YANGA KIMATAIFA….”WAKIFUZU ROBO FAINAL ITAKUWA BAHATI KWAO”…

Habari za Yanga

Wakati wawakilishi wa Tanzania Katika Michuano ya Klabu Bingwa Afrika Timu za Simba na Yanga wakipiga mahesabu makali kuona ni kwa namna gani wanafuzu kwa hatua ya Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa baada ya kuanza vibaya kwa michezo yao ya hatua ya Makundi.

Mchambuzi wa Michezo kutoka Efm, Wilson Oruma amesema kuwa kwa upande wake haoni Yanga ikfuzu kwa hatua inayofuata.

Akizungumza Oruma anasema;

Swali; Yanga wana nafasi ya kwenda robo fainali ? Na vipi kuhusu Simba ?

“Kundi la Simba liko wazi japo ni ngumu kwa sababu Wydad wanazitaka points za nyumbani na ugenini, Simba anapaswa kushinda ugenini na nyumbani, Timu imecheza vizuri na Jwaneng, Kundi bado liko wazi”

“Yanga kufuzu ni ngumu, Kwangu Yanga kushinda mechi ni mafanikio kwao kwa sababu mara ya mwisho kucheza group stage champions league hawakushinda mechi yoyote na walimaliza wa mwisho kwenye kundi, Kwa sasa malengo ni kushinda mechi, ikitokea wameenda robo fainali ni bonus”

Je unakubaliana na mawazo ya Wilson Oruma?

SOMA NA HII  BAADA YA KUONA WALIVYOCHEZA ZNZ...NABI ASHINDWA KUJIZUA YANGA..ATOA SAA 48..LA SIVYO....