Home Uncategorized MANCHESTER CITY INAPIGA HESABU KUMREJESHA KOMPANY ETIHAD

MANCHESTER CITY INAPIGA HESABU KUMREJESHA KOMPANY ETIHAD


MANCHESTER City, inaelezwa kuwa ipo kwenye mpango wa kumrejesha nahodha wa zamani wa kikosi hicho Vincent Kompany.
Nyota huyo mwenye miaka 34 alisepa ndani ya City msimu uliopita baada ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu England na kuibukia ndani ya Klabu ya Anderlecht ambako huko ni kocha mchezaji.
Akiwa ndani ya City alikiongoza kikosi hicho kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu England mara nne jambo ambalo linakumbukwa ndani ya kikosi hicho kilicho chini ya Kocha Mkuu, Pep Guardiola.
Beki huyo bado anakumbukwa ndani ya City inayotumia uwanja wa Etihad kutokana na mchango wake mkubwa huenda akitua ndani ya kikosi hicho atapewa pia jukumu la kuwa msaidizi wa Guardiola ambaye msaidizi wake wa zamani Mikel Arteta kwa sasa ni kocha mkuu Arsenal.


SOMA NA HII  WAKATI FEI TOTO AKIZIDI KUDENGUA...MUDATHIRI AITEKA 'SHOW' YANGA...NABI KAPAGAWA MAZIMA...