Home Habari za michezo AFCON YAISOGEZA TAIFA STARS KWEYE VIWANGO VYA JUU VYA FIFA….

AFCON YAISOGEZA TAIFA STARS KWEYE VIWANGO VYA JUU VYA FIFA….

Taifa Stars leo

Tanzania imepanda nafasi mbili juu kwenye viwango vya shirikisho la soka Duniani FIFA kwa mwezi wa pili [February] zilizotolewa hii leo.

Tanzania kabla ya kupanda ilikuwa nafasi ya 121 ikiwa na alama 1155.19 na sasa imepanda hadi nafasi ya 119 ikifikisha alana 1160.98.

Tanzania imeongeza alama 5.79 kutokana na kiwango walichokionyesha kwenye michezo ya fainali za mataifa ya Afrika zilizomalizika hivi karibuni nchini Ivory Coast.

Tanzania inashika nafasi ya 30 Barani Afrika ikiwa imepanda kwa nafasi mbili juu kutoka nafasi ya 32.

Kinara Duniani.

Argentina
Ufaransa
England

Vinara Afrika

Morocco
Senegal
Nigeria

Ukanda wa Cecafa

Uganda
Kenya
Tanzania.

SOMA NA HII  BAADA YA KUBANJULIWA NA YANGA JUZI....MAKI APUKUTISHA MIKONO SIMBA...ATOA TAHADHARI KWA TIMU ZA LIGI KUU...