Home Habari za Yanga YANGA YAIPIGA KO SIMBA…WAMSAINISHA BEKI HUYU KISIKI…YANASUBIRIWA MAOKOTO TU

YANGA YAIPIGA KO SIMBA…WAMSAINISHA BEKI HUYU KISIKI…YANASUBIRIWA MAOKOTO TU

Habari za Yanga leo

Mlinzi wa pembeni wa Yanga ambae alikuwepo kwa mkopo kutoka Singida Fountain Gate Nickson Kibabage amesaini mkataba wa miaka mitatu Yanga, makubaliano ya mauzo kati ya Singida na Yanga yameshafanyika.

Awali Singida ilipokea ofa ya Simba ambao walikuwa wanamuhitaji Kibabage.

Aidha, Klabu ya Singida Fountain Gate imethibitisha kufanya mazungumzo na klabu ya Yanga kwa ajili ya kumuuza mchezaji wao Nickson Kibabage ambaye anatumika kwa mkopo klabuni hapo.

Singida imesema wamemaliza mazungumzo na Yanga na kinachosubiriwa sasa ni Wananchi kuingiza fedha katika account za walima alizeti.

Ikumbukwe Kibabage alijiunga na Yanga katika dirisha kubwa la usajili kwa mkopo wa mwaka mmoja huku Simba ilikuwa ikihusishwa kuitaka huduma ya mlinzi huyo wa pembeni raia wa Tanzania

SOMA NA HII  KUHUSU ISHU YA KOCHA MPYA TAIFA STARS...TFF WAJA NA JIPYA HILI...POULSEN ATAJWA TENA...