Home Habari za Yanga Leo BALEKE ALIAMSHA YANGA…AONEKANA MAZOEZINI.

BALEKE ALIAMSHA YANGA…AONEKANA MAZOEZINI.

Baleke to Yanga

MSHAMBULIAJI wa zamani wa Simba, Jean Baleke Inaelezwa kuwa amesaini mkataba wa mwaka mmoja Yanga, baada ya kufuzu vipimo vya afya juzi na tayari ameanza mazoezi na wenzake kambini.

Ujio wa Baleke ni habari mbaya kwa Joseph Guede, ambaye rasmi amelazimika kuhamishiwa Singida Black Stars kumpisha Mkongomani huyo.

Guede alimaliza mkataba wa miezi sita ya awali na mabosi wa timu hiyo na kuamua kutokumuongezea mkataba mpya.

Jean Baleke, alianza mazoezi ya gym yaliyofanyika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es salaam, akiwa na wachezaji wenzake wa timu hiyo yake mpya.

Baleke anaifanya Yanga kuwa na mastaa wapya sita kambini kwao akitanguliwa na kipa Abubakar Khomeny, beki Chadrack Boka, viungo Clatous Chama aliyekuwa Simba, Aziz Andambwile na mshambuliaji Prince Dube kutoka Azam FC.

YANGA NA BALEKE WAHAMIA UFUKWENI

Kikosi cha Yanga, leo  jioni kinatarajiwa kuhama kutoka gym kwenda kujifua kwenye Fukwe za Coco (Coco Beach) kuendeleza hesabu zao za kujiweka sawa kabla ya kuanza msimu mpya wa mashindano.

Taarifa zinasema, mazoezi hayo ufukweni yataongozwa na kocha mkuu wa timu Miguel Gamondi, ambaye tayari ameshawasili nchini na kuungana na wachezaji wake pamoja na wasaidizi wake ambao walishatangulia kambini.

Na jana Jioni alikutana na wachezaji wote wa Yanga akiwemo Chama aliyewahi kupita katika klabu ya Simba kwa misimu 6 nyuma.

Akiwa Simba Chama aliifanyia makubwa timu hiyo, akiipa ubingwa wa Ligi mara 3 mfululizo,  ubingwa wa F mara 2 na kuifikisha hatua ya robo fainali ya Ligi ya MABINGWA mara 3,  na Kombe la Shirkisho mara moja.

Lakini pia Gamondi alikutana na mastaa wengine wapya akiwemo Prince Dube, Chadrack Boka na Abubakar Khomeiny.

SOMA NA HII  MAKAMBO ARUDI KWA MBWEMBWE BONGO...ATANGAZA VITA