Wednesday, January 21, 2026
Home Blog

KIPA MPYA ATAMBULISHWA MSIMBAZI

0

KLABU ya Simba SC imemtambulisha rasmi mlinda lango wao mpya, Mahamadou Tanja Kassali, raia wa Niger, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuimarisha kikosi chake kuelekea mashindano yajayo ya ndani na kimataifa.

Tanja amejiunga na Wekundu wa Msimbazi akitokea klabu ya AS FAN ya nchini Niger, ambako amekuwa akionesha kiwango kizuri kilichomvutia uongozi wa Simba kumleta nchini Tanzania.

Kupitia taarifa yao kwa umma, uongozi wa Simba umeeleza kuwa kipa huyo ana uzoefu na uwezo mkubwa wa kulinda lango, sifa walizoona zinaendana na mahitaji ya timu katika msimu huu.

Usajili wa Tanja unatajwa kuwa sehemu ya mpango wa Simba kuongeza ushindani katika nafasi ya kipa akichukuwa nafasi ya Moussa Pinpin Camara ambaye bado hajawa fiti, hatua inayolenga kuhakikisha timu inakuwa na chaguo bora na la uhakika kwa kila mchezo.

Mashabiki wa Simba wanatarajiwa kumuona kipa huyo mpya akianza mazoezi na timu mara moja, huku wakitarajia atachangia kwa kiasi kikubwa kuimarisha safu ya ulinzi na kuongeza ushindani ndani ya kikosi.

TANZANIA YAPANDA NAFASI MBILI UBORA FIFA

0

Timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’imepanda kwa nafasi mbili katika viwango vya ubora wa soka vya Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) kwa mujibu wa chati ya mwezi Januari 2026 iliyotolewa juzi.

Kutinga hatua ya 16 bora ya Fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 zilizofikia tamati huko Morocco juzi Jumapili, kumeonekana kuibeba Taifa Stars ambayo imepaa kutoka nafasi ya 112 hadi nafasi ya 110 ikiwa na pointi 1186.14.

Katika fainali hizo za AFCON 2026, Taifa Stars ilitoka sare katika mechi mbili na kupoteza michezo miwili, ikifunga mabao matatu na kuruhusu nyavu zake kutikiswa mara tano.

Wakati Taifa Stars ikipanda, mambo hayajaenda vizuri kwa timu ya taifa ya Uganda ‘The Cranes’ ambayo imeporomoka kwa nafasi tatu kutoka ile ya 85 hadi katika nafasi ya 88.

Katika fainali za AFCON 2025, Uganda iliishia katika hatua ya makundi baada ya kuchapwa mechi mbili na kutoka sare moja.

Historia imeandikwa na Morocco ambayo kufanya kwake vizuri katika AFCON 2025 ambapo iliishia fainali, kumeibeba na kuipandisha kwa nafasi tatu.

Morocco sasa ni ya nane katika viwango vya ubora wa dunia na imeweka historia ya kuwa Taifa la kwanza la Kiarabu kuingia katika 10 bora ya viwango vya ubora.

Mabingwa wapya wa AFCON 2025, Senegal wamepanda kwa nafasi saba kutoka nafasi ya 19 hadi katika nafasi ya 12 katika viwango hivyo vya ubora.

Timu iliyopanda kwa nafasi nyingi zaidi ni Cameroon ambayo imepaa kwa nafasi 12, kutoka nafasi ya 57 iliyokuwepo awali hadi katika nafasi ya 45.

Hakujawa na mabadiliko katika nafasi saba za juu ambapo timu zilizokuwepo hapo katika viwango vya mwezi Desemba zimeendelea kusalia katika nafasi zao.

Nafasi ya kwanza inashikiliwa na Hispania, Argentina ni ya pili, Ufaransa iko nafasi ya tatu, ya nne ni England huku Brazil ikiwa ya tano.

Ureno imejichimbia katika nafasi ya sita na nafasi ya saba inaendelea kushikiliwa na Uholanzi.

MAKONDA AIHAKIKISHIA FIFA USHIRIKIANO

0

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amekutana na kufanya mazungumzo na rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) Gianni Infantino katika ofisi za FIFA zilizopo Jijini Rabat, nchini Morocco.

Katika mazungumzo hayo Makonda amemshukuru Infantino kwa ushirikiano mkubwa anaoutoa kwa Tanzania katika maendeleo ya mchezo wa mpira wa miguu na amemhakikishia kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan na Serikali anayoiongoza inaunga mkono jitihada hizo na ipo tayari kushirikiana na FIFA.

Amemueleza Infantino kuwa Tanzania ina fursa nyingi za kuchangia katika maendeleo ya mpira wa miguu vikiwemo vipaji vya vijana wengi, maeneo ya kujenga miundombinu ya michezo na utashi wa kisiasa, na kwamba FIFA inakaribishwa kushirikiana na Serikali katika uwekezaji huo.

Aidha, Makonda amemkaribisha rais huyo na amemwambia Tanzania ipo tayari kuwa mwenyeji wa matukio mbalimbali ya FIFA ikiwemo mashindano, mikutano na ziara za viongozi na wataalamu.

Kwa upande Infantino amemshukuru Makonda na ujumbe wake kwa kumtembelea na amesema FIFA ipo tayari kushirikiana na Tanzania katika programu zake za maendeleo ambazo zitasaidia kutengeneza fursa kwa vijana kunufaika na mchezo wa mpira wa miguu ikiwemo ujenzi wa miundombinu na uendelezaji wa vituo vya ufundi.

Infantino ameipongeza Tanzania kwa kazi kubwa inayoendelea kufanywa na Serikali ya ujenzi wa miundombinu ya michezo kuelekea AFCON 2027 na amesema FIFA inaunga mkono jitihada hizo.Katika mazungumzo hayo Makonda aliongozana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, Balozi wa Tanzania nchini Morocco, Ali Mwadini, rais wa Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Michezo Boniface Tamba na Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa Neema Msitha.

YANGA KUIFATA AL AHLY MISRI JUMATANO

0

KIKOSI cha Yanga kinatarajiwa kuondoka nchini kesho alfajiri kuelekea nchini Misri, mji wa Alexandria, kwa ajili ya mchezo muhimu wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya mabingwa wa Afrika, Al Ahly.

Safari hiyo ni sehemu ya maandalizi ya kuelekea pambano gumu la kimataifa linalotarajiwa kuvuta hisia za mashabiki wengi barani Afrika.

Yanga wanatarajiwa kuikabili Al Ahly ugenini Ijumaa Januari 23 mwaka huu, wakiwa na lengo la kusaka alama tatu muhimu zitakazowaweka katika nafasi nzuri kabla ya mchezo wa marudiano utakaopigwa jijini Dar es Salaam.

Mchezo huo unatajwa kuwa kipimo kikubwa kwa kikosi cha Yanga katika kampeni zao za msimu huu wa michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Ofisa Habari wa Yanga, Ali Kamwe, amesema baada ya mchezo wa jana dhidi ya Mashujaa FC, kikosi kimeanza mara moja maandalizi ya safari hiyo muhimu. Ameeleza kuwa leo timu inafanya mazoezi maalumu ya mwisho kwa lengo la kujiweka sawa kabla ya kuanza safari.

Kamwe amesisitiza kuwa hali ya kikosi ipo vizuri kwani hakuna mchezaji mwenye majeraha, jambo linalompa kocha Pedro Goncalves nafasi ya kuchagua kikosi bora kitakachosafiri kwenda Misri. Ameongeza kuwa ushindani ndani ya timu ni mkubwa huku kila mchezaji akijitahidi kuonyesha ubora wake.

“Timu inatarajiwa kuondoka kesho alfajiri kuelekea Alexandria. Hakuna majeraha, wachezaji wote wapo vizuri na baada ya mazoezi ya leo, kocha wetu Pedro atachagua wachezaji watakaokuwa kwenye msafara,” amesema Kamwe.

BURUDANI NA KALAMBA GAMES NA MERIDIANBET

0

Wachezaji wa kasino, simama tayari kwa mapinduzi ya kweli mtandaoni. Meridianbet imeungana na Kalamba Games, kampuni ya kimataifa inayojivunia ubunifu wa sloti za kisasa zenye muonekano mzuri na uhuishaji wa hali ya juu. Ushirikiano huu unaleta burudani isiyo na kikomo kwa kila mchezaji mtandaoni, ukiwa kama safari mpya ya kila siku ya ushindi na msisimko.

Cheza michezo kama Dragons Glow, Dynasty Spark 7s, Lightning Fortune, na Monkey God, kila mzunguko ni fursa ya kushinda kubwa. Mfumo wa bonasi na alama maalumu unabadilisha kila mzunguko kuwa tukio lisilosahaulika, likikupeleka kwenye ulimwengu wa ushindi wa haraka na changamoto za kila sekunde.

Meridianbet inakuja na michezo ya kasino, mechi zenye odds tamu, na njia rahisi za kujiunga na kucheza. Ukiwa na Meridianbet, kila siku ni nafasi mpya ya kuongeza kipato chako na kufurahia burudani bila mipaka. Tembelea meridianbet.co.tz au piga *149*10#

Mbali na ushindi, michezo ya Kalamba Games inakupeleka kwenye simulizi za kipekee. Kila mzunguko ni hadithi mpya, kila alama inaweza kubadilika kuwa bonasi ya kushangaza, na kila ushindi unaongeza msisimko wa kasino mtandaoni. Hii inafanya wachezaji wa kila aina kufurahia burudani, kutoka wapenzi wa hatari kubwa hadi wapenzi wa mikakati thabiti.

Ushirikiano huu unaleta ubora wa hali ya juu wa kasino mtandaoni, ukiwa na michezo yenye teknolojia ya kisasa, sauti zinachangamsha, na bonasi zinazochangia ushindi mkubwa. Jiunge na maelfu ya wachezaji mtandaoni ambao tayari wanashuhudia mapinduzi haya na kufurahia kila mzunguko na kila ushindi.

Usikae kusubiri tena, tembelea Meridianbet, jisajili, na anza kushinda leo. Huu ni wakati wako kuingia kwenye ulimwengu wa kasino wa kidijitali, furahia burudani isiyo na kikomo, na uishi msisimko wa kila mzunguko. Cheza, shinda, na uzaa ushindi kila dakika.

MFUMO WA YANGA WAANZA KUELEWEKA

0

KOCHA Mkuu  wa Yanga, Pedro Goncalves, amesema kikosi chake kimeanza kuonyesha mabadiliko chanya baada ya wachezaji wapya kuelewa kwa kina falsafa na mahitaji yake ndani ya uwanja.

Pedro amesema hali hiyo imeongeza ufanisi wa timu na kufanya mawasiliano kati ya benchi la ufundi na wachezaji kuwa rahisi zaidi kuliko awali.

Ameeleza kuwa mwanzoni haikuwa rahisi kwa wachezaji kuzoea mfumo wake kutokana na mabadiliko ya mbinu na majukumu mbalimbali aliyoweka.

“Kadri muda ulivyopita na kupitia mazoezi ya mara kwa mara, wachezaji wameanza kuuelewa mfumo huo na kuutekeleza kwa ufanisi mkubwa wakati wa mechi.

maendeleo hayo yamechangia pia kuwapa nafasi nzuri wachezaji wapya kuingia moja kwa moja kwenye mfumo wa timu bila changamoto kubwa,” amesema.

Pedro amesema wachezaji wapya hawachukui muda mrefu kuzoea kwa sababu wanakuta mfumo tayari unaeleweka na unatekelezwa na kila mmoja.

Akizungumzia matumizi ya wachezaji wapya, Pedro amesema siri kubwa ya mafanikio yao ni kuhakikisha kila mchezaji anatumika kwenye nafasi anayoiweza zaidi.

Amefafanua kuwa falsafa yake ni “kuweka wachezaji sahihi kwenye nafasi sahihi ili kuongeza ubora wa timu kwa ujumla,”.

Pedro ameongeza kuwa njia hiyo inasaidia pia kupunguza presha kwa wachezaji wapya, wanapocheza kwenye nafasi wanazozoea, wanakuwa na ujasiri na uwezo mkubwa wa kuonyesha viwango vyao halisi .

“Kuifanya Yanga kuwa timu yenye ushindani mkubwa katika kila mchezo,  lengo lake ni kujenga timu imara yenye mtiririko mzuri wa uchezaji na matokeo chanya,” amesema.

CHAMA NI SWALA LA MUDA MSIMBAZI

0

UONGOZI wa klabu ya Simba umeendelea kuonyesha dhamira yake ya kuimarisha kikosi kwa kufikia makubaliano ya awali na kiungo mshambuliaji wa Singida Black Stars Clatous Chama kwa ajili ya kurejea tena ndani ya Msimbazi.

Taarifa zinaeleza kuwa pande hizo mbili zimekubaliana kandarasi ya mwaka mmoja, kinachosalia ni kukamilisha taratibu chache za mwisho kabla ya dili hilo kuwa rasmi.

Chama ni miongoni mwa nyota waliowahi kuacha alama kubwa ndani ya Simba, anaelezwa  yupo tayari kwa changamoto mpya baada ya mazungumzo kati yake na uongozi wa klabu kufikia hatua nzuri.

Makubaliano hayo yanaashiria kurejea kwa mchezaji aliyewahi kuwa kipenzi cha mashabiki kutokana na mchango wake mkubwa katika mafanikio ya timu.

Inaelezwa kuwa taratibu za mwisho za mchezaji huyo zinatarajiwa kukamilishwa leo, ikiwa ni pamoja na kuwasili Dar es Salaam kwa ajili ya kumalizia maelewano binafsi na kisha kutambulishwa rasmi.

Chanzo cha ndani kimeeleza kuwa Simba imepanga kumaliza dili hilo haraka ili kumpata mchezaji huyo mapema ndani ya kikosi.

Uamuzi huo unaonyesha dhamira ya Simba kuhakikisha inapata huduma ya nyota huyo bila kuchelewesha mipango ya benchi la ufundi.

Kwa kurejea kwa Chama, Simba inatarajia kuongeza ubunifu na uzoefu mkubwa katikati ya uwanja, hasa ikizingatiwa ratiba ngumu ya mashindano ya ndani na kimataifa.

CHAGUA MBINGWA WAKO LEO, UBET NA MERIDIANBET

0

Ligi ya mabingwa barani Ulaya inaendelea leo hii ndani ya Meridianbet huku ikiwa ni bado mechi zipo kwenye mfumo wa ligi. Timu zingine zipo kwenye hali nzuri huku zingine zikiwa bado zinajitafuta sasa. Na wewe jitafute uanze kupiga mkwanja leo.

Real Madrid watakuwa Santiago Bernabeu kupepetana dhidi ya AS Monaco ya kule Ufaransa ambao mpaka sasa wapo nafasi ya 19 huku wenyeji wao wakiwa nafasi ya 7. Ushindi huu ni muhimu wa Real kwani utawapeleka hadi nafasi ya juu. Je beti yako unaiweka kwa nani leo?. Tengeneza jamvi hapa.

Kwa upande wa Sporting Lisbon wao watamenyana dhidi ya bingwa mtetezi PSG ambao mpaka sasa wapo nafasi ya 3 huku wenyeji wao wakiwa nafasi ya 14 na pointi zao 10. Meridianbet wao wanampa bingwa mtetezi nafasi kubwa ya kushinda ugenini. Je wewe unampa nani nafasi ya kushinda?. Jisajili hapa.

Piga pesa kwenye michezo ya Kasino ya mtandaoni kama vile Keno, Aviator, Poker, Roulette,Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Pia Tottenham Host Spurs atamleta kwake Borussia Dortmund ambapo mechi ya mwisho kukutana kati yao ilikuwa ni 2019 ambapo BVB alichapika, hivyo leo hii anataka kulipa kisasi akiwa ugenini. ODDS KUBWA zipo kwenye mechi hii pale Meridianbet, hivyo ingia kwenye akaunti yako na ubeti sasa.

Villarreal uso kwa uso dhidi ya Ajax ambao tofauti ya pointi kati yao hadi sasa ni pointi 2 pekee. Timu zote zipo mkiani kwenye ligi ya mabingwa hadi sasa. Meridianbet wameipa mechi hii Odds kubwa na machaguo zaidi ya 1000 siku ya leo. Jisajili hapa.

Club Brugge atakuwa ugenini kukipiga dhidi ya Kairaty Almaty ambao mpaka sasa wana pointi 1 pekee huku wageni wao wakiwa na pointi 4. Takwimu zinaonesha kuwa timu hizi hazijawahi kukutana kwenye mashindano yoyote hii ndio mara ya kwanza. Je nani kushinda leo?. Bashiri hapa.

Nao vijana wa Pep Guardiola Manchester City watakuwa ugenini kukipiga dhidi ya Bodoe/Glimt ambao mpaka sasa hawajashinda mechi yoyote. City wao wapo nafasi ya 4 na ushindi ni muhimu sana kwenye mechi hii. Meridianbet wanampa nafasi kubwa ya kushinda City. Je wewe beti yako unaiweka kwa nani siku ya leo?. Tandika hapa.

Vijana wa Napoli wao wakiwa na matokeo ambayo hayaridhishi watakuwa ugenini kusaka ushindi dhidi ya Copenhagen ambapo wote wana pointi 7 kwenye msimamo wa Uefa. Kila timu inahitaji ushindi siku ya leo kujiweka kwenye nafasi nzuri kwenye mechi zilizobaki. ODDS KUBWA zipo mechi hii. Jisajili hapa.

Mechi kali ni hii ya Inter Milan vs Arsenal ambao ndio vinara wa msimamo wa UEFA kwani mpaka sasa kwenye mechi 6 walizocheza wameshinda zote huku vijana wa Chivu wao wakishinda 4 na kupoteza mbili hadi sasa. Je vijana wa London wataendeleza ushindi wao?. Machaguo zaidi ya 1000 yapo hapa. Suka jamvi lako hapa.

ISMAEL OLIVER TOURE ATUA RASMI MSIMBAZI

0

HATIMAYE sintofahamu imefikia tamati baada ya uongozi wa Klabu ya Simba kukamilisha usajili wa beki wa kati, Ismael Oliver Touré, kutoka klabu ya FC Baniyas ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na kujiunga rasmi na wekundu wa Msimbazi.

Simba imemtambulisha rasmi nyota huyo kama mali yao mpya kwa lengo la kuongeza nguvu na uimara katika safu ya ulinzi, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kuboresha kikosi kinachonolewa na kocha mkuu, Steve Barker.

Touré amejiunga na Simba baada ya kuachana na FC Baniyas hivi karibuni, ambapo alikuwa akishiriki Ligi Kuu ya UAE, hatua inayomfungulia ukurasa mpya katika taaluma yake ya soka barani Afrika.

Beki huyo wa kati anatajwa kuwa na uzoefu mkubwa wa soka la ushindani, hali inayotarajiwa kuipa Simba faida kubwa hasa katika michuano ya ndani na ile ya kimataifa.

Kabla ya kwenda kucheza soka la UAE, Touré aliwahi kuwa nguzo muhimu katika kikosi cha Stellenbosch FC ya Afrika Kusini, timu ambayo wakati huo ilikuwa chini ya kocha Steve Barker.

Uzoefu wa awali kati ya Touré na Barker unatajwa kuwa chachu kubwa ya usajili huo, huku mashabiki wa Simba wakitarajia kuona mchango wake uwanjani akisaidia kuimarisha safu ya ulinzi ya timu hiyo

DEPU AANZA KAZI, YANGA KUICHAPA MASHUJAA

0

Nyota mpya wa Yanga, Laurindo Aurelio ‘Depu’ ameanza kwa neema ndani ya klabu hiyo baada ya leo kuhusika na mabao mawili katika ushindi wa mabao 6-0 ambao timu yake imeupata dhidi ya Mashujaa FC, katika Uwanja wa KMC Complex, Dar es Salaam.

Nyota huyo raia wa Angola, amefunga bao moja na kupiga pasi moja ya mwisho akiiwezesha Yanga kupata ushindi huo ambao umeipeleka kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Depu aliyeingia katika kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Maxi Nzengeli, alianza kwa kupiga pasi iliyozaa bao la Mudathir Yahya katika dakika ya 81.Dakika ya 89, Depu aliwainua vitini mashabiki wa Yanga baada ya kuifungia timu hiyo bao la sita akimalizia mpira uliotemwa na kipa Erick Johora baada ya mkwaju wa faulo wa Allan Okello.

Katika mechi hiyo ya leo, mabao mengine ya Yanga yamefungwa na Prince Dube, Mohamed Damaro, Duke Abuya na Pacome Zouzou.

Baada ya dakika 90 kukamilika, Mudathir Yahya alitangazwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo.

Kipa wa Yanga, Abuutwalib Mshery aliondoka mifuko ikiwa imenona baada ya kutuzwa fedha na kundi kubwa la mashabiki wa Yanga walioonekana kukoshwa na kitendo cha kipa huyo kumaliza mchezo bila kuruhusu bao (clean sheet).

Huo ni ushindi wa sita kati ya saba iliyocheza kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu ambapo imepanda rasmi kileleni ikifikisha pointi 19, mbili zaidi ya zile za JKT Tanzania iliyokuwa ikiongoza hapo awali.

Baada ya ushindi huo, kibarua kinachofuata kwa Yanga hivi sasa ni mechi ya hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika huko Cairo, Misri, Ijumaa wiki hii dhidi ya Al Ahly.

329,001FansLike
12,344FollowersFollow
16,900SubscribersSubscribe

EDITOR PICKS