Tuesday, January 13, 2026
Home Blog

SIMBA KUPEWA FURAHA NA SIMBA QUEENS

0

WAKATI mashabiki wa Simba wakisalia na maswali kuhusu mwenendo wa timu ya wanaume, timu ya wanawake ya Simba Queens imeendelea kuwa chanzo cha tabasamu kwa Wanasimba kwa kuonyesha kiwango bora na ushindi wa kuvutia kwenye Ligi ya Wanawake Tanzania.

Simba Queens waliendeleza mwendo huo mzuri baada ya kuibuka na ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya Tausi FC katika mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa KMC Complex, Mwenge jijini Dar es Salaam, ambapo Simba walikuwa wenyeji wa mchezo huo.

Nyota wa mchezo huo alikuwa Aisha Mnuka aliyefunga mabao mawili, akionyesha ubora wake mbele ya lango, huku bao la tatu likifungwa na Jentrix Shikangwa na kuhitimisha karamu ya mabao kwa Simba Queens.

Katika kipindi cha kwanza, Simba Queens walionyesha udhibiti mkubwa wa mchezo na kufanikiwa kutamatisha dakika 45 za mwanzo wakiwa mbele kwa mabao 3-0, hali iliyowapa utulivu na kuonyesha tofauti ya ubora kati yao na wapinzani wao Tausi FC.

Katika michezo mingine ya ligi hiyo, Yanga Princess walipata ushindi wakiwa ugenini baada ya kuifunga Fountain Gate Princess kwa mabao 5-4, ushindi uliothibitisha pia ushindani mkubwa unaoendelea kushamiri kwenye ligi hiyo.

Kwa upande mwingine, mabingwa watetezi JKT Queens waliendeleza ubabe wao baada ya kuibuka na ushindi mwembamba wa bao 2-0 dhidi ya wenyeji wao Ruangwa Queens, matokeo yaliyozidi kuipa ligi hiyo mvuto na ushindani mkubwa.

CHEZA ZOMBIE APOCALYPSE MIZUNGUKO BURE

0

Katika ulimwengu wa burudani ya kidijitali, Meridianbet imechagua njia tofauti kwa kuwasilisha Zombie Apocalypse kama hadithi ya ubunifu kuliko ofa ya kawaida. Kampeni hii inaangazia namna michezo ya kisasa inavyoweza kuunganisha simulizi, teknolojia na burudani ili kumfanya mtumiaji ajisikie sehemu ya dunia inayocheza, si mtazamaji wa pembeni.

Tofauti na michezo inayotegemea bahati pekee, Zombie Apocalypse inajengwa juu ya simulizi linaloendelea. Mchezaji anaingizwa katika mazingira yanayobadilika hatua kwa hatua, ambapo kila mzunguko unaongeza mvutano na matarajio. Mbinu hii ya kusimulia hadithi inaifanya michezo ya kasino kuonekana kama uzoefu kamili wa burudani, si kitendo cha papo kwa papo.

Meridianbet inakuja na michezo ya kasino, mechi zenye odds tamu, na njia rahisi za kujiunga na kucheza. Ukiwa na Meridianbet, kila siku ni nafasi mpya ya kuongeza kipato chako na kufurahia burudani bila mipaka. Tembelea meridianbet.co.tz au piga *149*10#

Mfumo wa mizunguko ya bure umeundwa kuongeza muda wa uzoefu na kutoa nafasi ya kuchunguza vipengele vya mchezo kwa kina zaidi. Utapata hadi mizunguko 50 ya bure kila unapocheza mizunguko 100 ya pesa halisi. Mizunguko hii ya bure inatolewa siku inayofuata baada ya kucheza mizunguko hii 100.

Mchango wa Expanse Studio unaonekana wazi katika ubora wa michoro, sauti na mwendo wa mchezo. Mandhari ya giza, athari za sauti na uhuishaji wa kisasa vinaonyesha jinsi teknolojia ya michezo inavyoweza kuunda hali halisi ya kihisia. Ni mfano wa jinsi sanaa ya kidijitali inavyozidi kuchukua nafasi muhimu katika tasnia ya michezo.

Zombie Apocalypse ni sehemu ya mkakati mpana wa Meridianbet wa kutoa burudani iliyopangwa kwa watu wazima wanaotafuta uzoefu wa kisasa na uliodhibitiwa. Kampeni hii inaweka mkazo kwenye matumizi ya kuwajibika, ikikumbusha kuwa michezo ya aina hii inalenga burudani na inapaswa kufurahiwa kwa mipaka inayokubalika kisheria.

DAU DOGO, PESA NYINGI NA MERIDIANBET

0

Ni siku nyingine ya kibabe kabisa na tulivu ambayo imekuja kwaajili ya kubadili maisha yako. Timu kibao zipo uwanjani kuwania pointi 3 huku wewe ukiwania mkwanja wa maana. Ingia kwenye jamvi akaunti yako na ubeti sasa.

SAUDIA LEAGUE nayo kuna mechi za pesa kabisa ambapo Al Akhdoud atakipiga dhidi ya Al Khoolod ambapo tofauti ya pointi kati yao mpaka sasa ni 7 huku mwenyeji akitaka kuendeleza ushindi wake baada ya kushinda mechi ya mwisho walipokutana. Je pesa yako unaiweka kwa nani kati ya hawa wawili?. Tengeneza mkwanja hapa.

Mechi nyingine ni hii ya Al Fateh dhidi ya Al Riyadh ambao kwenye mechi 12 ambazo wamecheza hadi sasa wamefanikiwa kukusanya pointi 8 huku wenyeji wao wakikusanya pointi 14 hadi sasa. Nafasi ya kushinda mamilioni unayo kwenye mechi hii. Ingia na ubashiri hapa.

Al Ittihad yeye atakuwa ugenini kupepetana dhidi ya Damac ambao mpaka sasa wapo nafasi ya 14 kwenye msimamo wa ligi. Meridianbet wanakwambia ushindi unaanzai kwa kubashiri mechi hii leo. Ingia kwenye akaunti yako na ubashiri hapa kwani kuna machaguo uyapendayo.

Tajirika kwenye michezo ya Kasino ya mtandaoni kama vile Keno, Aviator, Poker, Roulette,Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kule Ujerumani, BUNDESLIGA kama kawaida kitawaka yaani mechi za pesa kabisa VFB Stuttgart atakipiga dhidi ya Eintracht Frankfurt ambapo mara ya mwisho kukutana kati yao mgeni aliondoka na ushindi. Leo hii ni nafasi ya mwenyeji kutaka kulipa kisasi akiwa nyumbani. Mechi hii ina ODDS KUBWA. Bashiri hapa.

Wakati kwa upande wa Borussia Dortmund yeye atakuwa mwenyeji wa Werder Bremen ambao mpaka sasa wanashika nafasi ya 10 huku wenyeji wao wakiwa nafasi ya 2. Kila timu inahitaji ushindi siku ya leo ijiweke kwenye nafasi nzuri. Machaguo zaidi ya 1000 yapo mechi hii. Tandika jamvi hapa.

Huku Leverkusen watakuwa ugenini kumenyana vikali dhidi ya Hamburger SV ambao wamependa daraja msimu huu wakiwa nafasi ya 13 huku wageni wao wakiwa nafasi ya 3 kwenye msimamo wa ligi hadi sasa. Tofauti ya pointi kati yao hadi sasa ni 13. Je nani unampa nafasi ya kuondoka na ushindi siku ya leo?. Suka jamvi hapa.

Mainz 05 vs FC Heidenheim ambapo mechi hii imepewa ODDS za kibabe na machaguo zaidi ya 1000. Takwimu zinaonesha kuwa mara ya mwisho kukutana hawa wawili kila mtu alishinda mechi moja akiwa kwa mwenzake. Hivyo leo hii kila mtu anataka ushindi huu. Jisajili hapa.

Kule Uingereza kutakuwa na mechi kali kabisa ya Nusu Fainali ya FA kati ya Newcastle United vs Manchester City ya Pep Guardiola ambapo wakali wa ubashiri Meridianbet wamempa nafasi kubwa City kuondoka na ushindi. Hii ni mechi ambayo kila timu inataka ushindi mnono kabisa. ODDS KUBWA zipo hapa. Beti sasa.

MTANZANIA APEWA MWAKA MMOJA NA NUSU

0

MSHAMBULIAJI wa Kitanzania, Oscar Evalisto amejiunga na Port Fouad inayoshiriki Ligi Daraja la Pili Misri kwa mkataba wa mwaka mmoja na nusu akitokea Makadi FC.

Evalisto aliitumikia Makadi kwa msimu mmoja akifunga mabao matano na asisti nne kwenye mechi 10 alizocheza akiibuka na tuzo moja  ya mchezaji bora wa mwezi.

Akizungumza na Mwanaspoti, Evalisto amesema Port walitaka kumpatia mkataba wa miaka mitatu lakini alisaini mwaka mmoja na nusu ili aweze kusikilizia ofa za timu za Ligi Kuu.

“Nina siku nne tangu nimejiunga hapa, timu inacheza Ligi Daraja la Pili lakini inataka kupanda daraja la kwanza na inaongoza ligi kwa tofauti ya pointi nne, kesho tuna mechi na timu inayotufuatia kwa pointi.

“Nataka nipambane nimalizie hii miezi sita kama itapanda hii timu itakuwa vizuri zaidi ili msimu ujao nicheze daraja la kwanza kwa kumalizia tu msimu halafu nione hizo baadhi ya timu zinazonifuatilia za ligi kuu tutakuwa tumefikia wapi,” amesema.

“Malengo yangu ni kucheza ligi kuu na kuna timu ambazo tayari zinanifuatilia kupitia hii timu mpya kwa maana hii timu haipo mbali na mjini, kwa hiyo itakuwa rahisi wao kunifuatilia kwa ukaribu tofauti na ile timu ya mwanzo ilikuwa mbali sana.”

TUMERUDI TENA UPYA KAZINI, AHMEDY

0

MENEJA Idara ya Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba, Ahmed Ally, amesema kikosi cha timu hiyo kimerejea rasmi katika uwanja wa mazoezi kuanza maandalizi ya hatua zinazofuata za mashindano mbalimbali yanayowakabili.

Simba wanajiandaa na mchezo wa Kombe la Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Esperance Sportive de Tunis utakaochezwa Januari 23, ugenini.

Ahmed  amesema kurejea huko ni sehemu ya mpango wa benchi la ufundi linaloongozwa na kocha Steve Barker kuhakikisha wachezaji wanakuwa tayari kimwili na kiakili baada ya mapumziko mafupi yaliyotolewa ili kurejesha nguvu na kuondoa uchovu wa ratiba ngumu ya mechi.

“Mazoezi hayo yameanza kwa kasi nzuri, huku wachezaji wakionyesha ari kubwa na morali ya hali ya juu, jambo linalotoa picha chanya kwa benchi la ufundi kuelekea michezo ijayo ya ushindani,” amesema.

Ahmed amesema benchi la ufundi linaendelea kufanya tathmini ya kina kwa kila mchezaji ili kuhakikisha wote wako katika hali bora ya utimamu, huku programu maalum zikitumika kwa wachezaji waliokuwa wakisumbuliwa na majeraha madogo.

Ameongeza kuwa lengo kubwa la Simba ni kuendelea kupambana katika mashindano yote wanayoshiriki, maandalizi haya ni muhimu ili kuhakikisha timu inabaki katika kiwango cha juu na kutimiza malengo yake ya msimu.

Amewatoa hofu mashabiki wa Simba kwa kusema kuwa hali ya kikosi kwa ujumla ni nzuri, hakuna majeruhi wapya wakubwa waliopatikana wakati wa kurejea mazoezini.

Amewataka  mashabiki kuendelea kutoa sapoti yao ya dhati kwa timu, akisisitiza kuwa mchango wao ni muhimu katika kuongeza hamasa kwa wachezaji wanapojiandaa kuwakilisha nembo ya Simba katika viwanja mbalimbali.

NIKO SEHEMU YA MAFANIKIO, OKELLO

0

MSHAMBULIAJI mpya wa Yanga, Allan Okello, ameonesha furaha na ari kubwa mara baada ya kujiunga na klabu hiyo kongwe, amesisitiza kuwa yuko tayari kuwa sehemu ya safari ya mafanikio ya timu hiyo.

Okello amesema anajivunia kuvaa jezi ya Yanga na yupo tayari kupambana kwa ajili ya heshima na malengo ya klabu.

Kupitia ujumbe mfupi aliouandika kwenye mitandao ya kijamii mara baada ya kutambulishwa rasmi, Okello aliweka wazi hisia zake kwa mashabiki wa Yanga.

“Nina furaha kuwa Mwananchi. Daima mbele, nyuma mwiko,” aliandika Okello, akiuambatanisha ujumbe huo na alama ya klabu pamoja na kauli mbiu maarufu ya Yanga.

Nyota huyo alitambulishwa jana usiku saa tano, hatua iliyokuja kama zawadi kwa mashabiki wa Yanga waliokuwa katika shamrashamra za kuadhimisha Siku ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Utambulisho huo uliibua shangwe na hisia miongoni mwa Wananchi wengi waliomkaribisha kwa nderemo na matumaini mapya.

Kwa upande wa historia yake ya soka, Okello ni mchezaji wa kimataifa wa Uganda mwenye uzoefu mkubwa, aliyewahi kuzichezea klabu za KCCA FC, Paradou AC ya Algeria na Vipers SC.

Katika klabu hizo, alijijengea jina kutokana na uwezo wake wa kufunga mabao pamoja na kutoa pasi za mwisho zenye macho.

Ujio wa Okello unatarajiwa kuongeza ushindani na ubunifu mkubwa ndani ya kikosi cha Yanga, hasa katika safu ya ushambuliaji.

Mashabiki wa klabu hiyo sasa wanasubiri kwa hamu kumuona nyota huyo akianza kuchangia moja kwa moja mafanikio ya Yanga katika mashindano ya ndani na kimataifa.

DEPU KUTUA YANGA LEO, DIRISHA DOGO

0

BAADA ya uongozi wa Yanga kumtambulisha rasmi kiungo Allan Okello, macho sasa yanaelekezwa kwa mshambuliaji wao mpya Laurindo Dilson Maria Aurélio maarufu kama Depu, ambaye anatarajiwa kutua nchini leo kuanza safari yake mpya ndani ya klabu hiyo.

Depu anatarajiwa kuwasili nchini leo tayari kwa kukamilisha taratibu zote muhimu, kabla ya kutambulishwa rasmi kama mchezaji halali wa Yanga, hatua inayoongeza nguvu katika safu ya ushambuliaji wa timu hiyo.

Ujio wa mshambuliaji huyo unatarajiwa kuwapa furaha mashabiki wa Wananchi, ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakisubiri kuona maboresho makubwa kwenye eneo la kufunga mabao kuelekea michezo ya ushindani inayokuja.

Kwa mujibu wa taarifa za klabu, Depu atakuwa mchezaji wa nne kusajiliwa na Yanga katika dirisha dogo la usajili, akijiunga na Emmanuel Mwanengo, Mohammed Damaro pamoja na Allan Okello ambaye alitambulishwa rasmi jana.

Kocha Mkuu wa Yanga amesema kuwa ujio wa wachezaji wapya unaongeza ushindani na ubora ndani ya kikosi, hali itakayosaidia timu kuwa imara zaidi katika mashindano mbalimbali ya ndani na kimataifa.

Hata hivyo, kocha huyo amebainisha kuwa anatambua wazi kuwa wachezaji wapya watahitaji muda wa kuitambua falsafa ya timu na mfumo anaoutumia, jambo linalohitaji uvumilivu na maandalizi ya kina.

“Kuna wachezaji wapya ambao wapo kwenye timu yetu na hilo ni jambo jema, lakini ninaamini watatumia muda kuitambua falsafa. Tumeanza kuwapa kile kinachostahili, na mashindano ya Kombe la Mapinduzi ni sehemu sahihi ya kuwajaribu kabla ya mashindano mengine,” amesema kocha Pedro

AWESO AWA GUMZO KENYA

0

KIUNGO wa Kimataifa wa Tanzania, Awesu  Awesu, ametambulishwa rasmi kama mchezaji mpya wa klabu ya Police Kenya FC, hatua inayomfungulia ukurasa mpya katika safari yake ya soka la kulipwa nje ya nchi.

Awesu ametua katika klabu hiyo ya Ligi Kuu Kenya kwa mkataba wa miezi sita, makubaliano yanayolenga kuongeza ushindani kikosini pamoja na kuimarisha safu ya kiungo kuelekea michezo ya nusu ya pili ya msimu.

Kupitia taarifa rasmi za klabu, Awesu amepewa jezi namba 33, namba ambayo ataitumia katika mechi zote za mashindano ya ndani na mengineyo atakayoshiriki Police Kenya FC msimu huu.

Ujio wa nyota huyo umeibua matumaini makubwa kwa mashabiki wa Police Kenya FC, wakiamini uzoefu wake wa kimataifa na uwezo wake wa kukaba, kupiga pasi sahihi na kusoma mchezo utaongeza ubora mkubwa ndani ya kikosi.

Kwa upande wake, Awesu anaingia Kenya akiwa na dhamira ya kujituma, akilenga kutumia vyema fursa hiyo ili kuisaidia timu kupata matokeo chanya, huku akijenga jina lake zaidi katika soka la Afrika Mashariki.

Hatua hii pia inaendelea kuthibitisha thamani ya wachezaji wa Tanzania katika soko la soka la kimataifa, huku mashabiki wakingojea kwa hamu kumuona Awesu akianza kazi rasmi uwanjani akiwa na jezi ya Police Kenya

ANZA SAFARI YA SAMSUNG 26 NA SUPER HELI

0

Cheza leo Super Heli, mchezo unaokuletea msisimko wa kila sekunde. Hapa, kila hatua unayopiga ni hatua moja karibu na zawadi kubwa. Meridianbet inakualika kujiunga na safari hii isiyo na mwisho, ambapo kila raundi ni nafasi ya kubadilisha siku yako kuwa ya ushindi.

Kila Jumatatu, mshindi mmoja huondoka na Samsung A26 mpya kabisa, na kila mzunguko unakuletea nafasi ya kuingia kwenye historia ya ushindi. Hapa, ujasiri na ustadi wako huchangia moja kwa moja kwenye matokeo yako.

Meridianbet haikuachi nyuma, kuna michezo mbalimbali ya kasino mtandaoni pamoja na mechi za kimataifa za kubashiri zenye odds bomba zinazokuongezea nafasi ya kuongeza kipato chako kila siku. Kujiunga ni rahisi! Tembelea meridianbet.co.tz au piga *149*10#.

Kadri unavyocheza, msisimko unakua na fursa zako za ushindi zinapanda. Wachezaji hodari wanajua siri ya kushinda ambayo ni kuzingatia muda, kutumia ustadi wao, na kuchukua nafasi zao kwa busara. Kila mzunguko ni tiketi ya kuwa mmoja wa wale watakaoshinda Samsung A26 na kushuhudia zawadi zisizo na kifani.

Kufungua akaunti ya Meridianbet ni kuunda mlango wa fursa zisizo na mwisho. Cheza mara nyingi, ongeza nafasi zako za kushinda, na ujumuike na wale watakaoshinda zawadi kubwa. Super Heli ni mchanganyiko wa teknolojia, msisimko, na zawadi zisizo na kifani. Tembelea meridianbet.co.tz sasa, chukua nafasi yako, na uandike jina lako kwenye historia ya ushindi.

USHINDI UNAANZIA HAPA NYUMBANI

0

Nafasi ya ushindi hii hapa na wakali wa Meridianbet ambapo kupitia promosheni ya Beti Online unaweza ukaondoka na Samsung A26. Weka dau lako kuanzia 5000 na ubashiri hapa.

Meridianbet inaendelea kuwa kinara katika kutoa promosheni zenye thamani halisi kwa wachezaji wake. Kupitia kampeni yake mpya, kampuni hii inaleta fursa murua kwa mashabiki wa mpira kushiriki bashiri za mechi za Ligi kwa dau la kuanzia shilingi 5,000 tu na kuingia kwenye droo ya kujishindia simu mpya ya kisasa aina ya Samsung A26. Hii ni ofa inayochochea ushindani, msisimko na thamani kwa kila mchezaji anayejiunga.

Meridianbet wanasema kuwa ili ujiweke kwenye nafasi ya kuondoka na simu janja hii hapa na uwe wa Kidigitali kabisa ni vyema ukabashiri mara nyingi zaidi kwani kufanya hivyo kunakuweka karibu na ushindi leo hii wa Samsung A26.

Ukiachana na promosheni hiyo, Meridianbet inakwambia tengeneza mkwanja kupitia michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kampeni hii inalenga kuongeza hamasa kwa mashabiki kufurahia mechi za Ligi wakiwa na matumaini makubwa. Kila ubashiri unaowekwa si tu unaleta msisimko wa kutafuta ushindi wa dau, bali pia msisimko wa kusubiri droo ya kujua kama wewe ndio mteule wa kupata simu mpya. Huku mashindano yakiendelea kila wiki, kila mchezaji anapata nafasi nyingi kadri anavyobashiri mara kwa mara.

Washindi wa promosheni hii watatangazwa kila Ijumaa ambapo ndio siku ambayo simu hutolewa hivyo usikae mbali na fursa hii kwani inakupa nafasi ya wewe kumiliki simu kali ambayo itakufanya uweze kuperuzi.

Kumbuka kuwa unapoingia kwenye mashindano haya ya kuwania Samsung A26, hutakiwi Kuturbo Mkeka wako au CASH OUT kwa namna nyingine haitahusika kwani inatakiwa usubiri jamvi lako limalizike.

Na kufanya hivyo kutakufanya ujiondoe kwenye mashindano kwani tiketi yako itahesabika kama batili. Hivyo subiri hadi mechi zote zikamilike ndipo uweze kuingia kwenye wachezaji ambao sio batili.

329,001FansLike
12,344FollowersFollow
16,900SubscribersSubscribe

EDITOR PICKS