Home Blog

YANGA YAFUNGUKA KUHUSU MPANZU

0

OFISA Habari wa Yanga, Ali Kamwe, ameweka wazi kuwa si sahihi kwa klabu hiyo kuzungumzia mchezaji ambaye bado ana mkataba na timu nyingine, akisisitiza kuwa wanaheshimu taratibu za usajili pamoja na mikataba ya wachezaji.

Kauli hiyo imeibuka kufuatia gumzo linalomhusisha kiungo wa Simba, Elie Mpanzu, kufuatia taarifa zilizomnukuu Kamwe kana kwamba Yanga ina nia ya kumsajili mchezaji huyo katika dirisha dogo.

Kamwe amesema kwa sasa Yanga inaendelea kufanya kazi kwa kufuata mapendekezo ya Kocha Mkuu, Pedro Gocalves, ambaye tayari amekabidhi ripoti yake kwa uongozi ili kuboresha kikosi kuelekea mzunguko ujao wa ligi.

“Hatusajili kwa mihemuko. Kama kuna nafasi ipo basi tutaongeza mtu. Kuhusu Mpanzu, si busara kuzungumzia mchezaji mwenye mkataba. Ni mchezaji mzuri, lakini tunaheshimu mkataba wake,” amesema Kamwe.

Amesisitiza kuwa Yanga inafanya usajili kwa umakini mkubwa kwa kuangalia wachezaji ambao wamemaliza mikataba au wale waliobakiza miezi sita, ili kuhakikisha wanatoa mchango wa haraka ndani ya kikosi.

“Kama kuna mchezaji mzuri aliyebakiza miezi sita na timu yake imekubali ofa kipindi hiki cha dirisha dogo, basi tutapeleka pesa kwa ajili ya kufanya biashara,” amesema Kamwe.

SIMBA YAIBUKA NA MIKAKATI YA UBORA MPYA

0

UONGOZI wa Simba umefanya kikao maalum cha kimkakati kwa lengo la kuboresha kikosi chao na kurejesha makali ya timu kuelekea mzunguko wa pili wa Ligi Kuu na michuano ya kimataifa.

Taarifa kutoka ndani ya mkutano huo zinasema Bodi ya Wakurugenzi Simba ilikutana kujadili kwa undani mwenendo wa timu katika mashindano yote, ikiwemo tathmini ya matokeo na kiwango cha jumla cha kikosi msimu huu.

Katika kikao hicho, ajenda kubwa ilikuwa ni ujio wa kocha mpya, ambapo imeelezwa kuwa uongozi unahitaji kupata kocha sahihi kabla ya kikosi kurejea kambini ili kuanza maandalizi mapya. Vyanzo vimedai kuwa tayari mchakato wa kumpata kocha huyo umefikia hatua nzuri.

Aidha, kikao hicho pia kilizama kwenye suala la bajeti ya dirisha dogo la usajili, kwa lengo la kuongeza nguvu kwenye maeneo yenye mapungufu ndani ya timu. Inaelezwa kuwa uongozi uko tayari kufanya maboresho makubwa ili kuleta ushindani zaidi.

Mtoa habari kutoka klabuni hapo amethibitisha kuwa uongozi umeafikiana kumpa nafasi kocha mpya atakayekuja kuungana na benchi la ufundi lililopo sasa, huku Seleman Matola akiendelea na majukumu yake kama kocha msaidizi.

“Tunalenga kutumia vyema kipindi hiki cha AFCON kuirudisha timu kwenye uimara wake ili iweze kushindana vema kimataifa na kwenye ligi ya ndani,” kilisema chanzo hicho.

YAO HATARINI MIKONONI MWA PEDRO

0

Hatma ya beki wa Yanga, Attohoula Yao, kuendelea kusalia ndani ya kikosi cha Wananchi ipo mikononi mwa Kocha Mkuu, Pedro Gocalves, ambaye ndiye ataamua mustakabali wa nyota huyo baada ya tathmini ya afya na kiwango chake kukamilika.

Yao, bado ana mkataba na klabu hiyo, aliondolewa kwenye usajili wa msimu huu kutokana na majeraha yaliyomuweka nje kwa muda mrefu,

Licha ya kuwa ni sehemu ya wachezaji wanaolipwa na klabu hiyo kila mwezi. Hatua hiyo ilichukuliwa ili kumpa nafasi ya kutekeleza programu ya matibabu na kurejea kwenye ubora wake wa awali.

Ofisa Habari wa Yanga, Ali Kamwe, amefafanua kuwa kwa sasa wanaisubiri ripoti ya idara ya utimamu wa mwili ambayo itabainisha kama Yao atakuwa fiti ifikapo Januari au Februari.

Ripoti hiyo itakuwa msingi wa kocha kufanya uchambuzi kama bado anamhitaji kwenye eneo lake la ulinzi.

Kamwe amesema katika nafasi anayoicheza Yao, tayari kuna wachezaji wengine wawili; Israeli Mwenda na Kibwana Shomari , hivyo uamuzi wa kumrudisha kwenye usajili au la utategemea mahitaji ya benchi la ufundi na mkakati wa timu kuelekea mzunguko ujao.

“Kocha Pedro atafanya uchunguzi wake binafsi mara tu Yao atakapothibitishwa kuwa fiti kwa asilimia 100, ili kubaini kama kiwango chake kimerudi katika hali inayokidhi mahitaji ya kikosi.

Baada ya tathmini hiyo, kocha atawasilisha ripoti yake kwa uongozi, ikieleza kama anamuhitaji beki huyo ili arejeshwe kwenye usajili, aendelee kufanya mazoezi ndani ya timu au atolewe kwa mkopo ili apate muda wa kucheza mara kwa mara,” amesema.

YANGA KUNGIA KAMBINI DESEMBA 15

0

OFISA Habari wa Yanga, Ali Kamwe, amesema kikosi cha timu hiyo kimepewa mapumziko rasmi na kinatarajiwa kurejea kambini Desemba 15 mwaka huu kuendelea na maandalizi ya Ligi Kuu Tanzania Bara pamoja na michuano ya kimataifa.

Kamwe amesema kuwa benchi la ufundi limetoa mapumziko kuanzia Desemba 7 hadi Desemba 15, ambapo baada ya kurejea, wachezaji wataendelea na programu maalumu hadi Desemba 20 kabla ya kupumzika tena hadi Desemba 28.

Amesema utaratibu huo umelenga kutoa muda wa wachezaji kusherehekea sikukuu na familia zao, ambapo wanatakiwa kurejea Desemba 29 tayari kwa maandalizi ya mwisho kuelekea hatua ngumu zinazowakabili.

Kwa mujibu wa Kamwe, kipindi hicho cha maandalizi ni muhimu kwa kuwa mwezi Januari Yanga itakabiliwa na ratiba ngumu yenye mechi za Ligi Kuu na zile za kimataifa, kutegemea ratiba ya mwisho itakayotolewa na Bodi ya Ligi.

Amesema lengo la programu hiyo ni kuhakikisha timu inarejea kwenye ushindani ikiwa katika hali bora, sambamba na kuhakikisha wachezaji wanaendelea kuwa katika utimamu wa juu kuelekea mashindano hayo.

Akizungumzia timu nyingine ndani ya klabu, Kamwe alisema Ligi ya Wanawake inaendelea ambapo Desemba 12 Yanga Princess watashuka dimbani kuvaana na Tausi FC kwenye Uwanja wa KMC Complex.

Kamwe aliongeza kuwa timu ya vijana ya klabu hiyo, U-20, inatarajiwa kucheza Desemba 17, ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa ratiba ya shughuli za mwezi mzima kwa timu zote tatu za Yanga.

SIMBA HAIJAPOTEZA DIRA YAKE, AHMEDY ALLY

0

MENEJA wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally, amewatoa hofu mashabiki na wanachama wa klabu hiyo akisisitiza kuwa timu bado ipo kwenye mwenendo sahihi licha ya kupoteza mchezo mmoja pekee katika Ligi Kuu Tanzania Bara.

Katika ukurasa kwake wa mtandao wa kijamii, Ahmed amesema hakuna sababu ya wafuasi wa Simba kujihisi wanyonge, kwani kikosi kimeonyesha ubora mkubwa kwenye mechi tano walizocheza mpaka sasa, kikishinda michezo minne na kupoteza mmoja tu.

“Huu ni wastani mzuri, hata kama matarajio ya mashabiki yamekuwa makubwa zaidi msimu huu. sasa wachezaji wako kwenye mapumziko mafupi, mapumziko hayo yanapaswa kuwa ya kimwili pekee huku akili na dhamira za kila mmoja zikiendelea kubaki kazini ili kutathmini namna ya kurejea kwa nguvu mpya na ari ya ushindi,” amesema.

Ahmed aliongeza kuwa mashabiki wa Simba wana matarajio makubwa na wanaitaka timu ifanye vizuri kila mechi, jukumu kubwa liko kwa wachezaji na benchi la ufundi kuhakikisha wanajitoa kikamilifu ili kuyafikia malengo hayo bila kutetereka kutokana na matokeo ya karibuni.

“Klabu itayafanyia kazi maoni, ushauri na hata ukosoaji unaotolewa na wadau mbalimbali kwa lengo la kuboresha utendaji na kuifanya timu iwe imara zaidi ndani na nje ya uwanja. Simba bado ina nafasi kubwa ya kufanya vizuri kwenye mashindano yote inashiriki,” amesema.

Ahmed amesema katika Ligi Kuu, Simba imebakiwa na michezo 25, hali inayotoa fursa ya kurekebisha mapungufu na kuongeza ushindani.

Kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika, amesema zipo mechi nne muhimu zinazohitaji maandalizi makubwa ili kurejea katika kiwango cha kutisha kilichozoeleka.

Ahmed ameeleza kuwa hakuna sababu ya kukata tamaa au kuona msimu umekuwa mgumu kwa kupoteza mchezo mmoja tu, bado mapema na safari ya mafanikio ya Simba ndiyo kwanza inaendelea kuchanja mbuga.

PEDRO AUWASHA MOTO YANGA, AKABIDHI RIPOTI NZITO

0

KOCHA Mkuu wa Yanga, Pedro Gocalves ameanza kufanya yake mapema baada ya kuyawasilisha maagizo rasmi kwa uongozi juu ya maboresho anayoyahitaji katika dirisha dogo la usajili.

Ripoti hiyo imeelezwa kuwa na maelezo ya kina juu ya maeneo yanayohitaji nguvu upya kuelekea mzunguko wa pili wa Ligi Kuu.

Taarifa kutoka ndani ya Yanga zimeeleza kuwa uongozi chini ya Rais Hersi Said unatarajiwa kuketi kikao kizito cha bajeti ya usajili ndani ya siku chache zijazo. Kikao hicho ndicho kitakachotoa uamuzi wa mwisho juu ya majina ya wachezaji wanaoweza kuongezwa kwenye kikosi cha mabingwa hao watetezi.

Dirisha dogo linatarajiwa kufunguliwa Desemba 16 na kufungwa Januari 15, 2026, Yanga wanakesha kuhakikisha hawakosi watakowahitaji. Kwa kawaida dirisha hili huwa fupi na la ushindani mkubwa, klabu inakimbizana na muda ili ikamilishe mpango kabla ya timu nyingine kuvamia wachezaji wanaotakiwa.

Chanzo chetu kimedokeza kuwa ripoti ya Pedro si ya mabadiliko makubwa sana, bali imejikita zaidi katika kuyasafisha maeneo machache yenye udhaifu ambayo yamekwamisha timu kwenye baadhi ya michezo.

Pedro anatajwa kutaka kuongeza ubora katika nafasi mbili au tatu ambazo zimekuwa na upungufu katika miezi ya hivi karibuni.

“Tayari ripoti ya Pedro iko mezani kwa uongozi, na bajeti yake itajadiliwa ndani ya wiki hii,” kilisema chanzo chetu.

Inaelezwa kuwa mkakati wa ndani unataka kila kitu kikamilike mapema ili kocha awe na nafasi ya kuwapokea wachezaji wapya kabla ya kurejea kwa ligi hatua ya moto.

Mtoa habari huyo alifafanua kuwa lengo la ripoti hiyo ni kuongeza uhai wa kikosi, bila kufanya mabadiliko makubwa ambayo yanaweza kuvuruga muunganiko uliopo. Pedro anataka wachezaji waliopo waongezwe nguvu, hasa katika eneo lenye ushindani mdogo na lililoonyesha kusuasua katika mechi kadhaa.

“Baada ya kikao cha Jumamosi tunatarajia kupata mwanga zaidi. Pia kocha anafuatilia mastaa watakaong’ara AFCON ili kuona kama kuna wanaoweza kuongezwa,” amesema chanzo hicho.

PATA 10% YA HASARA YAKO KILA UKICHEZA WIN&GO

0

Mwezi wa Disemba umejaa fursa za kipekee kwa wapenzi wa michezo ya kasino. Meridianbet inakuletea Win&Go na ofa ya kurejeshewa 10% ya hasara zako kila siku. Hii inamaanisha kwamba hata ukiwa na siku mbaya, sehemu ya dau lako inarudishwa, ikikuwezesha kuendelea kucheza bila hofu ya kupoteza.

Win&Go ni mchezo wa haraka wa namba na bahati nasibu ambapo unachagua namba 6 hadi 10 kati ya 48, na kila dakika tano matokeo yanatokea na iwapo namba ulizozichagua zikitokea, unakua umeshinda. Ukipata “gift positions”, namba zako zinaweza kukupa urejeshaji wa dau hata kama hukushinda, na ikiwa zikikutana mara mbili, ushindi wako unapanda mara nne. Hii ni njia ya kipekee ya kuongeza nafasi zako za faida kila sekunde.

Meridianbet inakuja na michezo ya kasino, mechi zenye odds tamu, na njia rahisi za kujiunga na kucheza. Ukiwa na Meridianbet, kila siku ni nafasi mpya ya kuongeza kipato chako na kufurahia burudani bila mipaka. Tembelea meridianbet.co.tz au piga *149*10#

Kwa wale wanaopenda msisimko zaidi, Golden Rounds zinakuja kuongeza ushindi wako mara mbili, na kukupa fursa ya kuzunguka katika droo za dhahabu zinazofanya mchezo kuwa mzuri zaidi. Hii ni nafasi ya kuchukua kila sekunde na kuiunda kuwa faida, huku ukiwa na amani ya akili kutokana na urejeshaji wa hasara.

Kuanzia 01.12.2025 hadi 31.12.2025, mchezaji yeyote anayepoteza angalau Sh. 1,000 kwa siku atarudishiwa 10% ya hasara yake siku inayofuata, hadi Tsh. 15,000 kwa siku. Hii ni fursa ya kipekee ya kucheza kwa uhuru, kujaribu namba zako, na kufurahia michezo bila wasiwasi.

Usikose ofa hii ya kipekee. Jiunge na Meridianbet, cheza mchezo wa Win&Go kila siku, pata Golden Rounds, faida ya gift positions, na 10% ya pesa zako zikirudishwa pale unapokosa ushindi.

DAU LAKO, UTAJIRI WAKO LEO NA UEFA

0

Kama kawaida michuano ya ligi barani Ulaya inazidi kupamba moto ambapo Meridianbet inahakikisha kuwa huondoki patupu. Suka jamvi lako na ubashiri mechi zote hapa hapa.

Arsenal chini ya kocha mkuu Mikel Arteta watasafiri kukipiga dhidi ya Club Brugge ya kule Ubelgiji. The Gunners ndio wapo juu pale kwenye msimamo wa ligi wakishinda mechi zao zote 5, huku wenyeji wao wakiwa na pointi 4 kwenye mechi 5 hadi sasa. Machaguo zaidi ya 1000 yapo kwenye mechi hii. Suka jamvi hapa.

Kwa upande wa Juventus baada ya kushinda mechi yake iliyopita, leo hii atakuwa nyumbani kusaka pointi tatu dhidi ya Pafos ambao walitoa sare mechi yao iliyopita. Wote hawa mpaka sasa wana pointi sawa kwenye msimamo wa ligi. Mechi hii ni muhimu kwa wote wawili. Je beti yako unaiweka kwa nani siku ya leo?. Beti hapa.

Mechi kubwa itakuwa ni hii ya Real Madrid vs Manchester City katika dimba la Santiago Bernabeu huku mechi ya mwisho kukutana, Real waliondoka na ushindi mechi zote mbili. Hii ni vita ya Xabi Alonso vs Pep Guardiola. Pointi 2 ndizo zinazowatengenisha hadi sasa. Bashiri hapa.

Mechi za Kasino ya Mtandaoni kukupa pesa leo, Cheza Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Ajax ambao mpaka sasa ndio vibonde wa kwenye ligi ya mabingwa watakuwa ugenini kukiwasha dhidi ya Qarabag FK. Tofauti ya pointi kati yao hadi sasa ni 7 pekee ambapo mwenyeji anahitaji ushindi huu kwa namna yoyote ile. Je nani unampa pesa yako akupe ushindi?. Bashiri hapa.

Mechi nyingine ni hii ya Athletic Bilbao vs PSG ambao mpaka sasa wana pointi 12, huku wenyeji wao wakiwa na pointi 4 pekee. Mara ya mwisho kukutana timu hizi mbili ilikuwa ni 2011 ambapo Paris waliondoka na ushindi mechi ya pili, lakini ya kwanza walipoteza. Je nani kuondoka na ushindi siku ya leo?. Jisajili hapa.

Kule Ujerumani katika dimba la BayArena kutakuwa na mtanange wa Bayer Leverkusen vs Newcastle United huku tofauti yao ikiwa ni pointi 1 pekee hadi sasa. Kila timu inahitaji ushindi leo hii kwa hali na mali. ODDS KUBWA zipo Meridianbet leo. Ingia na ubeti sasa.

Vijana wa Antonio Conte Napoli wao watakuwa ugenini kumenyana dhidi ya SL Benfica ya kule Ureno. Ikumbukwe kuwa wenyeji mechi yao iliyopita ndio walifanikiwa kushinda toka michuano hii ianze. Mara ya mwisho kukutana Napples waliondoka na ushindi mechi zote mbili. Je ni wakati sahihi kwao kulipa kisasi?. Tengeneza hapa.

HAMZA AFANYIWA UPASUAJI, SIMBA YAPATA TUMAINI

0

BEKI wa kati wa Simba, Abdulrazack Hamza, hatimaye amekamilisha matibabu ya upasuaji yaliyofanyika nchini Morocco, hatua inayompa matumaini mapya ya kurejea uwanjani baada ya kipindi kirefu cha kuwa nje ya majukumu ya timu.

Uongozi wa Simba umethibitisha kuwa mchezaji huyo anaendelea vizuri na kwamba taratibu za mwisho za matibabu wa jeraha lake zinaendelea kufuatiliwa kwa karibu.

Hamza alikuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu kutokana na majeraha yaliyomsumbua msimu huu, hali iliyoathiri mchango wake ndani ya kikosi cha wekundu wa Msimbazi.

Majeraha hayo yaliyokuwa yakijirudia yalimlazimu kufanyiwa vipimo vya kina ambavyo vilionyesha kuwa upasuaji ulikuwa hatua sahihi zaidi ili kurejesha ubora wake.

Kwa mujibu wa taarifa ya Simba, upasuaji huo umefanyika kwa mafanikio nchini Morocco, eneo ambalo klabu hiyo imekuwa ikitumia kwa wachezaji wake kupata huduma bora za kitabibu kutokana na ubobezi wa wataalamu wao.

Madaktari wamethibitisha kuwa beki huyo yupo katika hali nzuri na mwitikio wa mwili wake baada ya upasuaji unaridhisha.

Klabu imesema awamu inayofuata kwa mchezaji huyo ni kuanza programu maalumu ya itakayodumu kwa muda maalumu kabla ya kuruhusiwa kurejea kwenye mazoezi mepesi.

Ratiba yake ya kurejea dimbani itategemea mwendelezo wa maendeleo yake katika kipindi hiki cha kuimarika upya.

Hamza ni miongoni mwa wachezaji waliokuwa wakitegemewa kwenye eneo la ulinzi kutokana na uthabiti, nguvu na utulivu wake katika kuongoza safu ya nyuma. Kutokuwepo kwake kumeifanya Simba kujaribu mbinu na muunganiko tofauti kwenye ulinzi msimu huu.

Kwa sasa mashabiki wa Simba wanapewa matumaini kuwa kurejea kwa Hamza kutaleta nguvu mpya, hasa katika kipindi ambacho timu inajiandaa na mechi ngumu za Ligi Kuu na michuano ya kimataifa.

DUBE KUBEBESHWA MAJUKUMU MAZITO, PEDRO ASEMA

0

KOCHA mkuu wa Yanga, Pedro Gocalves , ameibuka na kufunguka juu ya kiwango cha mshambuliaji wake, Prince Dube, amesema kuwa bado anamwamini lakini sasa anamwekea jukumu zito la kuhakikisha anakuwa mhimili wa safu ya ushambuliaji msimu huu.

Pedro amesema kuwa Dube ameonyesha dalili nzuri, lakini bado anatakiwa kuongeza uthabutu na uthabiti katika mechi kubwa.

“Dube ni mchezaji mwenye kipaji kikubwa na uwezo wa kufanya maamuzi ya haraka ndani ya boksi, jambo ambalo lilionekana katika mchezo na Coastal Union alifunga bao muhimu,” amesema.

Kocha huyo amesisitiza kuwa uwezo huo unapaswa kuonekana mara kwa mara, hasa katika mechi ngumu zinazohitaji utulivu na ubunifu wa hali ya juu.

Ameongeza kuwa moja ya sababu zinazomfanya amtegemee Dube ni namna anavyojituma mazoezini na hamasa ya kutaka kufikia kiwango bora zaidi, ushindani ndani ya kikosi umeongezeka hivyo kila mchezaji anapaswa kupigania namba kwa nguvu zote.

Pedro amesema anapenda kuona Dube akiongeza idadi ya mabao, kuwa mshambuliaji wa kiwango chake anatakiwa kufunga mara kwa mara na sio kutegemea mechi chache kuonyesha ubora.

Ameweka wazi kuwa msimu huu Yanga inataka kumaliza ligi bila kuwa na presha, jambo litakalowezekana ikiwa washambuliaji watawajibika ipasavyo.
Kocha huyo pia amezungumzia changamoto ambazo Dube amekuwa akipitia, ikiwemo majeraha ya mara kwa mara yaliyowahi kumrudisha nyuma.

Ameeleza kuwa timu ya benchi la ufundi imekuwa ikifanya kazi kubwa kuhakikisha anamrejesha kwenye ubora na kumjengea utulivu wa kimwili na kiakili.

Pedro amesisitiza kuwa nafasi ya kucheza haipo kwa jina, bali kwa kile mchezaji anachokifanya uwanjani. amemtaka Dube asipunguze kasi wala kuridhika na kiwango alichokionyesha wiki iliyopita, bali aongeze njaa ya mafanikio na kuwa mfano wa kuigwa kwa washambuliaji wengine.

Pedro ameweka wazi kuwa kama Dube atatimiza mahitaji yake ya kiufundi na kuongeza makali, ataendelea kuwa silaha muhimu ya Yanga msimu huu.

329,001FansLike
12,344FollowersFollow
16,900SubscribersSubscribe

EDITOR PICKS