Wednesday, January 7, 2026
Home Blog

SAKATA LA CONTE NA DOUMBIA KAMWE AFICHUA

0

OFISA Habari wa Klabu ya Yanga, Ali Kamwe, amefunguka kuhusu sakata linalowahusu nyota wao wawili, Balla Conte na Mohammed Doumbia, wanaodaiwa kugoma kutolewa kwa mkopo kwenda Singida Black Stars.

Yanga na Singida Black Stars zilikuwa zimefikia makubaliano ya kubadilishana wachezaji, ambapo Marouf Tchakei na Mohamed Damaro wamejiunga  na kikosi cha Wananchi, huku Conte na Doumbia wakielekea kujiunga na Walima Lizeti kwa mkopo.

Hata hivyo, mpango huo haujakamilika baada ya nyota hao kushindwa kujiunga na Singida Black Stars, huku zikiibuka taarifa kwamba wamegoma na kudai kulipwa fedha zao pamoja na kuvunja mikataba yao, jambo ambalo uongozi wa Yanga umelikataa.

Kutokana na msimamo huo, Yanga imeendelea kuwajumuisha Conte na Doumbia katika kikosi chake kilichopo visiwani Zanzibar kwa ajili ya mashindano ya Kombe la Mapinduzi, hatua iliyolenga kuonyesha kuwa bado ni sehemu ya timu.

Akizungumza kuhusu suala hilo, Kamwe amesema wachezaji hao bado ni mali ya Yanga na wapo kambini Zanzibar pamoja na timu, huku akisisitiza kuwa taarifa nyingi zinazoandikwa hazina ukweli.

“Hao wachezaji ni mali ya Yanga na wapo na timu hapa Zanzibar. Kuna watu wamekuwa wanaandika vitu tofauti tofauti, lakini kama kutakuwa na suala lolote la kutolewa kwa mkopo au kusitisha mikataba yao, taarifa rasmi itawekwa wazi,” amesema Kamwe.

SIMBA YATOA ONYO KALI KWA WANA JANGWANI

0

Klabu ya Simba  imeweka wazi kuwa haiko tayari kufanya usajili wa kukurupuka katika dirisha dogo la usajili, kuwa kila hatua inayochukuliwa inalenga kuimarisha kikosi kwa kuzingatia mahitaji halisi ya benchi la ufundi chini ya Kocha Mkuu, Steve Barker.

Akizungumza kuhusu mikakati ya klabu hiyo, Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Simba, Ahmed Ally, amesema uongozi unafanya kazi kwa umakini mkubwa ili kuhakikisha usajili unaofanyika unaongeza ushindani na ubora ndani ya kikosi, badala ya kuongeza majina bila sababu za msingi.

Kwa kipindi cha hivi karibuni, Simba imekuwa ikihusishwa na majina mbalimbali ya wachezaji, akiwemo kiungo Clatous Chama, ambaye kumekuwa na tetesi za kurejea kwake Msimbazi. Hata hivyo, Ahmed ameeleza kuwa kwa sasa taarifa nyingi zinazosambaa mitandaoni ni tetesi za kawaida za kipindi cha usajili.

“Kinachoonekana mitandaoni ni sehemu ya kelele za dirisha dogo. Kuhusu Chama au mchezaji mwingine yeyote, ukweli utajulikana pale mambo yatakapokuwa yamekamilika,” amesema Ahmed.

Ameongeza kuwa Simba inalenga kufanya maboresho madogo lakini yenye tija, ili kujiandaa vyema na ushindani mkubwa katika mashindano yanayokuja.

“Tunaangalia maboresho machache yatakayoongeza nguvu ya timu. Wale waliopo kwenye mpango wetu, mambo yakikaa sawa, tutawaweka wazi kwa wakati muafaka,” amesisitiza.

Ahmed ameongeza kuwa Simba haitafanya usajili kwa shinikizo la kufunguliwa kwa dirisha, bali itaangalia kama kikosi kilichopo kinamridhisha kocha.

Endapo kutabainika mapungufu, ndipo usajili wa mchezaji mwenye mchango wa moja kwa moja utafanyika, na si kwa lengo la kumpa muda mfupi kabla ya kumtoa kwa mkopo.

HATUMPI PRESHA KOCHA, MANGUNGU

0

MWENYEKITI wa Klabu ya Simba, Murtaza Mangungu, amesema kuwa kucheza mechi mbili pekee hakuwezi kuwa kipimo cha kutathmini ubora wa kocha mkuu wa timu hiyo, Steve Barker, huku akisisitiza kuwa uongozi hauko tayari kumuwekea presha mapema.

Mangungu amebainisha kuwa Barker ametambulishwa hivi karibuni kama kocha mkuu wa Simba, jukumu lake rasmi lilianza katika mashindano ya Kombe la Mapinduzi yanayoendelea visiwani Zanzibar, hivyo bado ni mapema kutoa tathmini ya kina kuhusu uwezo wake.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti huyo, suala la kuridhika au kutoridhika na kocha halipaswi kuamuliwa kwa kuangalia michezo miwili pekee, hali ya kikosi pia haijakaa sawa kutokana na wachezaji nane hadi tisa kukosekana.

“Hatuwezi kumpima kocha kwa mwenendo huo, hasa timu ikiwa imecheza mechi mbili tu na bado wachezaji wengi muhimu hawapo kikosini,” amesema Mangungu.

Ameongeza kuwa uongozi wa Simba umempa muda kocha Barker kuandaa kikosi chake kwa utulivu, kwa lengo la kujenga timu imara itakayokabiliana na mashindano makubwa yaliyo mbele, ikiwemo michuano ya kimataifa.

Akizungumzia mchezo wa jana dhidi ya Fufun SC, Mangungu amesema Simba ilimaliza salama licha ya changamoto chache za kiufundi zilizojitokeza, akiamini kuwa kocha Barker atazifanyia kazi kwa kina.

“Ni kweli timu ilicheza chini ya kiwango kwa baadhi ya nyakati, wachezaji walionekana kuwa na uoga kidogo wakifikiria mashindano ya kimataifa na hivyo kucheza kwa tahadhari ili kuepuka majeraha,” amesema Mwenyekiti huyo.

CAMARA AIOKOA SIMBA, YAKATA TIKETI YA NUSU FAINALI

0

SIMBA   imefanikiwa kukata tiketi ya kucheza hatua ya nusu fainali ya Kombe la Mapinduzi baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Fufuni SC katika mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa New Amaan Complex, visiwani Zanzibar.

Kiungo wa Simba, Naby Camara, alikuwa shujaa wa mchezo huo baada ya kufunga bao la ushindi dakika ya 90, bao lililowahakikishia Wekundu wa Msimbazi nafasi ya kuendelea na safari yao katika michuano hiyo.

Hata hivyo, Simba ilianza mchezo huo kwa kushtukizwa baada ya Fufuni SC kupata bao la mapema dakika ya 15 lililofungwa na Mbonj Steven, jambo lililoifanya Simba kuongeza kasi ya mashambulizi wakisaka bao la kusawazisha.

Juhudi za Simba zililipa dakika ya 23 baada ya Hussein Mbegu kufunga bao la kusawazisha, bao lililorejesha matumaini kwa mashabiki wa timu hiyo na kuwafanya wachezaji kuendelea kushambulia kwa umakini mkubwa.

Mchezo uliendelea kuwa wa ushindani mkubwa hadi dakika za mwisho, ambapo Camara alitumia vyema nafasi aliyopata na kuifungia Simba bao la pili, lililohitimisha ushindi wa 2-1 na kuzima kabisa matumaini ya Fufuni SC.

Kwa matokeo hayo, Simba sasa inatinga hatua ya nusu fainali ya Kombe la Mapinduzi ambako itakutana na Azam FC, timu iliyofanikiwa kuiondoa URA ya Uganda kwa ushindi wa mabao 2-1 katika mchezo mwingine wa robo fainali.

HOLIDAY DROPS INAKUPA ZAWADI ZA KUANZA MWAKA

0

Meridianbet inakuleta fursa ya kipekee ya kushinda kupitia Holiday Drops. Hii si michezo ya kawaida, ni tukio la kipekee ambapo zawadi hujitokeza ghafla, zikibadilisha kila mzunguko kuwa fursa ya mshangao na ushindi. Huu ni msimu wa kusherehekea mwaka mpya ukiwa na furaha na tabasamu kwenye uso wako.

Holiday Drops inakuletea msisimko wa kasino mtandaoni bila kikomo. Kila mzunguko ni safari mpya, na kila sekunde ni nafasi ya kuibuka kwa zawadi zisizotarajiwa. Hii inakuwezesha kufurahia kila mchezo huku ukiwa na shauku ya kuona zawadi zinazomiminika kwenye akaunti yako kwa kasi ya upepo.

Meridianbet inakuja na michezo ya kasino, mechi zenye odds tamu, na njia rahisi za kujiunga na kucheza. Ukiwa na Meridianbet, kila siku ni nafasi mpya ya kuongeza kipato chako na kufurahia burudani bila mipaka. Tembelea meridianbet.co.tz au piga *149*10#

Kwa wale wanaopenda kudhibiti burudani yao, Meridianbet inakupa chaguo rahisi la kuwasha au kuzima Holiday Drops. Ukibofya ikoni ndogo juu kulia, unaweza kuamua ni lini zawadi zianze kumiminika. Hii inakupa uhuru wa kucheza kwa mtindo wako huku ukijua kila mzunguko unaweza kuwa tukio la kipekee la ushindi.

Michezo ya Holiday Drops kama Snowing Gifts 3, Joker’s Wild Ride – Xmas, Majestic Santa, na Wild Xmas – Hold & Hit imesukwa kwa ustadi wa hali ya juu. Mandhari ya kuvutia, mitindo ya kipekee, na zawadi zinazoibuka ghafla vinakuleta burudani ya kiwango cha juu.

Jisajili sasa na Meridianbet, chagua mchezo wako wa kushiriki na uanze kumwagikiwa na mvua ya zawadi. Huu ndio wakati wa kuanza 2026 ukiwa na ushindi na furaha isiyoisha.

USHINDI UNAANZIA HAPA NYUMBANI

0

Nafasi ya ushindi hii hapa na wakali wa Meridianbet ambapo kupitia promosheni ya Beti Online unaweza ukaondoka na Samsung A26. Weka dau lako kuanzia 5000 na ubashiri hapa.

Meridianbet inaendelea kuwa kinara katika kutoa promosheni zenye thamani halisi kwa wachezaji wake. Kupitia kampeni yake mpya, kampuni hii inaleta fursa murua kwa mashabiki wa mpira kushiriki bashiri za mechi za Ligi kwa dau la kuanzia shilingi 5,000 tu na kuingia kwenye droo ya kujishindia simu mpya ya kisasa aina ya Samsung A26. Hii ni ofa inayochochea ushindani, msisimko na thamani kwa kila mchezaji anayejiunga.

Meridianbet wanasema kuwa ili ujiweke kwenye nafasi ya kuondoka na simu janja hii hapa na uwe wa Kidigitali kabisa ni vyema ukabashiri mara nyingi zaidi kwani kufanya hivyo kunakuweka karibu na ushindi leo hii wa Samsung A26.

Ukiachana na promosheni hiyo, Meridianbet inakwambia tengeneza mkwanja kupitia michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kampeni hii inalenga kuongeza hamasa kwa mashabiki kufurahia mechi za Ligi wakiwa na matumaini makubwa. Kila ubashiri unaowekwa si tu unaleta msisimko wa kutafuta ushindi wa dau, bali pia msisimko wa kusubiri droo ya kujua kama wewe ndio mteule wa kupata simu mpya. Huku mashindano yakiendelea kila wiki, kila mchezaji anapata nafasi nyingi kadri anavyobashiri mara kwa mara.

Washindi wa promosheni hii watatangazwa kila Ijumaa ambapo ndio siku ambayo simu hutolewa hivyo usikae mbali na fursa hii kwani inakupa nafasi ya wewe kumiliki simu kali ambayo itakufanya uweze kuperuzi.

Kumbuka kuwa unapoingia kwenye mashindano haya ya kuwania Samsung A26, hutakiwi Kuturbo Mkeka wako au CASH OUT kwa namna nyingine haitahusika kwani inatakiwa usubiri jamvi lako limalizike.

Na kufanya hivyo kutakufanya ujiondoe kwenye mashindano kwani tiketi yako itahesabika kama batili. Hivyo subiri hadi mechi zote zikamilike ndipo uweze kuingia kwenye wachezaji ambao sio batili.

YANGA YAJIPANGA KIVITA DHIDI YA TRA UNITED

0

KIKOSI cha Yanga kinatarajiwa kushuka dimbani kesho Januari 6, 2026 kuikabili TRA United katika mchezo wake wa pili wa mashindano ya Kombe la Mapinduzi yanayoendelea visiwani Zanzibar.

Mchezo huo unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana na historia ya timu hizo pamoja na umuhimu wa pointi katika hatua ya makundi.

Mabingwa hao wa Tanzania Bara wataikaribisha TRA United katika dimba la New Amaan Complex, ambapo timu zote mbili zinashiriki Ligi Kuu Tanzania Bara.

Uzoefu wa ligi moja umeifanya kila timu kufahamu vyema mbinu na uwezo wa mpinzani wake, jambo linaloongeza presha na mvuto wa pambano hilo.

Yanga wanaingia katika mchezo huo wakiwa na kumbukumbu chungu ya kupoteza alama tatu mbele ya TRA United kabla ya kuanza kwa msimu huu, wakati timu hiyo ikiitwa Tabora United.

Hali hiyo inawafanya Wananchi kuwa makini zaidi na kuutambua mchezo huo kama mtihani mgumu unaohitaji umakini wa hali ya juu.

Kwa upande wao, TRA United nao wanakumbuka uchungu wa kufungwa na Yanga katika dimba lao la nyumbani msimu uliopita. Hilo linawapa motisha ya ziada ya kutaka kulipa kisasi na kuonyesha mabadiliko waliyojiwekea kuelekea msimu huu.

Akizungumza kuelekea mchezo huo, Kocha Mkuu wa Yanga, Pedro Gocalves, amesema kikosi chake kimefanya maandalizi ya kutosha na kiko tayari kwa changamoto hiyo.

Amesisitiza  kuwa lengo lao ni kufanya vizuri katika kila mchezo bila kujali muda wa maandalizi wa mpinzani.

“Dhamira yetu kubwa ni kuwa tayari kila wakati. Haijalishi wenzetu wamepata muda mrefu wa kujiandaa kuliko sisi, ni lazima tuwe tayari kushinda. Ninaamini baada ya mchezo wa kesho tutatinga hatua ya nusu fainali,” amesema Pedro kwa kujiamini.

Hata hivyo, Yanga watakosa huduma ya wachezaji kadhaa akiwemo Clement Mzize ambaye anaendelea na mazoezi ya kurejea kwenye kiwango bora baada ya majeraha, pamoja na Mudathir aliye karibu kurejea uwanjani.

Aidha, Lassine Kouma na golikipa Khomein nao bado wapo kwenye majeraha, lakini kocha Pedro anaamini kikosi alichonacho kina uwezo wa kufanya vizuri na kuendeleza mwendo mzuri katika mashindano hayo.

NDANI YA MASAA 48 JANGWANI KUTAMBULISHA WAPYA

0

UONGOZI wa Klabu ya Yanga umeweka wazi kuwa mchakato wa usajili bado unaendelea, leo na kesho wakitarajiwa kuendelea kuwatambulisha nyota wapya wa kimataifa watakaokiongeza nguvu kikosi hicho kuelekea michuano ijayo.

Ofisa Habari wa Yanga, Ali Kamwe, amesema klabu hiyo bado haijafunga rasmi dirisha la usajili na ndani ya siku mbili zijazo mashabiki watarajie taarifa nyingine njema kuhusu wachezaji wapya.

Kamwe ameeleza kuwa uongozi umejipanga kikamilifu kuhakikisha kikosi kinakuwa imara zaidi, hasa kwa kuongeza wachezaji wenye ubora na uzoefu wa kimataifa ili kukidhi malengo makubwa ya klabu ndani na nje ya nchi.

Hadi sasa, Yanga tayari imethibitisha usajili wa nyota watatu, ambapo wawili ni Mohammed Damaro na Marouf Tchakei waliotua kwa mkopo kutoka Singida Black Stars, huku usajili wa tatu ukiwa ni mzawa Emmanuel Mwanengo aliyechukuliwa kutoka TRA United.

Kwa mujibu wa Kamwe, usajili wa wachezaji wazawa tayari umefikia tamati, na sasa nguvu zote zinaelekezwa kwa nyota wa kigeni wanaotarajiwa kuongeza ushindani na ubora ndani ya kikosi cha Wananchi.

“Hatujamaliza usajili bado, tunatarajia kutangaza nyota wengine wawili kama siyo leo (Jumatatu) basi kesho (Jumanne). Kuhusu wazawa tayari tumeshafunga ukurasa,” amesema Kamwe,

BOYELI NA JANGWANI KWISHA HABARI

0

UONGOZI wa Klabu ya Yanga umetangaza rasmi kuachana na aliyekuwa nyota wao, Andy Boyeli, baada ya kumalizika kwa mkataba wake wa mkopo wa miezi sita aliokuwa akiitumikia timu hiyo.

Taarifa hiyo imetolewa na Ofisa Habari wa klabu hiyo, Ali Kamwe, ambaye amesema pande zote mbili zimefikia makubaliano ya kumalizana kwa amani.

Boyeli alijiunga na Yanga mwanzoni mwa msimu akitokea klabu ya Sekhukhune United ya Afrika Kusini kwa mkataba wa mkopo wa miezi sita.

Licha ya kupewa nafasi katika kikosi, mshambuliaji huyo hakufanikiwa kuonyesha kiwango kilichotarajiwa na benchi la ufundi pamoja na mashabiki wa klabu hiyo.

Kutokana na hali hiyo, uongozi wa Yanga uliona ni busara kutomwongezea mkataba baada ya muda wake wa mkopo kukamilika, kuruhusu arejee katika klabu yake ya Sekhukhune United.

Kamwe amesema uamuzi huo umezingatia tathmini ya kiufundi pamoja na mipango ya baadaye ya timu.

Ameongeza kuwa Boyeli ni miongoni mwa wachezaji wachache waliopata baraka ya kuondoka rasmi katika dirisha la usajili, hadi sasa hakuna mchezaji mwingine aliyeachwa zaidi ya waliotangazwa wazi.

Mbali na Boyeli, Kamwe amethibitisha pia kuondoka kwa mchezaji mwingine, Denis Nkane, ambaye amepelekwa kwa mkopo kujiunga na timu ya TRA kwa ajili ya kupata nafasi zaidi ya kucheza na kuendeleza kiwango chake.

Kwa mujibu wa Kamwe, Yanga itaendelea kufanya maamuzi ya kimkakati kuhusu kikosi chake ili kuhakikisha timu inakuwa imara zaidi katika mashindano mbalimbali yanayoendelea, huku ikizingatia maslahi ya klabu na maendeleo ya wachezaji wake.

YANGA YATOA ONYO KALI ZANZIBAR YAICHAPA NA……..

0

KIKOSI cha  Yanga kimeendelea kudhihirisha ubora wake baada ya kuanza kwa kishindo mashindano ya Kombe la Mapinduzi, kufuatia ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya KVZ katika mchezo uliochezwa kwa ushindani mkubwa visiwani Zanzibar.

Yanga ilianza mchezo kwa kasi na dhamira ya wazi ya kutafuta ushindi wa mapema, hali iliyowalazimu KVZ kujilinda kwa muda mrefu katika eneo lao. Shinikizo hilo liliwapa Wananchi matokeo dakika ya 32, pale kiungo mshambuliaji Pacome Zouzoua alipofunga bao la kwanza baada ya kumalizia kwa ustadi krosi safi kutoka kwa Max Nzengeli.

Baada ya bao hilo, Yanga iliendelea kutawala mchezo kwa kumiliki mpira na kutengeneza nafasi kadhaa za kufunga. KVZ walijaribu kujipanga upya kwa kujilinda kwa nidhamu na kusubiri mashambulizi ya kushtukiza, lakini hawakufanikiwa kubadili mwelekeo wa mchezo. Kipindi cha kwanza kilimalizika Yanga wakiwa mbele kwa bao 1-0, licha ya Nzengeli kukosa nafasi nzuri dakika ya 45 baada ya shuti lake kupaa juu ya lango.

Kipindi cha pili Yanga walirejea uwanjani wakiwa na kasi zaidi, wakiongeza presha iliyowavuruga mabeki wa KVZ. Mashambulizi hayo yaliwazaa matunda dakika ya 55, ambapo Célestin Ecua alifunga bao la pili na kuzidisha maumivu kwa wapinzani wao.

Bao hilo liliwakatisha tamaa KVZ na kuwapa nguvu zaidi Wananchi kuendelea kushambulia. Yanga waliendelea kulisakama lango la wapinzani wao kwa mashambulizi ya kasi kutoka pembeni pamoja na pasi za haraka katikati ya uwanja, wakionyesha tofauti kubwa ya kiwango kati ya timu hizo mbili.

Hatimaye, Yanga walihitimisha ushindi wao kwa bao la tatu lililotokana na makosa ya ulinzi wa KVZ, hali iliyompa nafasi Emmanuel Mwanengo kutikisa nyavu. Ushindi huo wa mabao 3-0 umeipa Yanga mwanzo mzuri wa Kombe la Mapinduzi na kuonyesha wazi kuwa Wananchi wamekuja Zanzibar wakiwa na dhamira ya kutwaa taji hilo.

329,001FansLike
12,344FollowersFollow
16,900SubscribersSubscribe

EDITOR PICKS