Wednesday, January 14, 2026
Home Blog

WANNE WAVUJA JASHO KWELIKWELI MAPINDUZI CUP 2026

0

TAMATI ya Kombe la Mapinduzi 2026 ilikuwa jana Jumanne Januari 2026 ilipopigwa mechi ya fainali kati ya Azam dhidi ya Yanga kwenye Uwanja wa Gombani, Pemba kuanzia saa 10:30 jioni.

Kabla ya kupigwa mechi ya fainali ya michuano hiyo iliyoanza Desemba 28, 2025, kulikuwa na nyota wanne waliovuja jasho kwa kucheza mechi zote hadi kutinga hatua ya mwisho.

Wachezaji hao ni makipa Aboutwalib Mshery (Yanga) na Aishi Manula (Azam) pamoja na mabeki Chadrack Boka na Frank Assinki wote wanakipiga Yanga.

Mshery ambaye katika mechi tatu alizodaka zikiwamo mbili hatua ya makundi na moja nusu fainali, amefanikiwa kuondoka bila ya kuruhusu bao. Ndiye kipa mwenye clean sheet nyingi katika mashindano ya mwaka huu ambazo ni tatu alizopata dhidi ya KVZ, TRA United na Singida Black Stars.

Kwa upande wa Manula, ameidakia Azam mechi zote nne kwa dakika 360. Katika mechi hizo tatu ni hatua ya makundi na moja nusu fainali, akiruhusu mabao mawili dhidi ya Singida Black Stars na URA hatua ya makundi, huku akiwa na clean sheet mbili alizopata dhidi ya Mlandege (makundi) na Simba (nusu fainali).

Boka na Assinki, ndiyo mabeki ambao wamecheza mechi zote tatu za Yanga bila ya kufanyiwa mabadiliko wakiungana na Mshery kuwa nyota pekee wa kikosi hicho kucheza dakika zote 270.

Wakati huohuo, nyota wawili, Tusuubira Abraham wa URA na Adam Omar Adam wa TRA United wakiweka rekodi ya wachezaji walioingia kutokea benchi, lakini hawakumaliza mechi, wakatolewa baada ya muda kidogo kukichafua.Alianza Adam wakati TRA United ikitoka sare ya bao 1-1 dhidi ya KVZ mechi ikichezwa Desemba 29, 2025, dakika ya 57 aliingia kuchukua nafasi ya James Msuva, akatolewa dakika ya 80 kumpisha Shaban Chilunda. Dakika 23 pekee zilimtosha kuonekana.Tusuubira naye alikutana na hali kama hiyo wakati URA ikifungwa 2-1 na Azam, Januari 5, 2026 ambapo dakika ya 60 aliingia kuchukua nafasi ya Aliro Moses, akatolewa dakika ya 89 kumpisha Amaku Fred. Alicheza kwa dakika 29 pekee.

YANGA KUSHUSHA DAWA YA KUIMALIZA AL AHLY

0

UONGOZI wa Yanga umeweka wazi mikakati yake ya kuimarisha kikosi kabla ya kibarua kigumu dhidi ya Al Ahly ya Misri, huku ukithibitisha kukamilisha usajili wa wachezaji wawili wa kigeni kwa ajili ya kuongeza nguvu katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Ofisa Habari wa Yanga, Ali Kamwe, amesema hadi sasa klabu hiyo imeshawatambulisha wachezaji watatu, lakini bado kuna nyota wawili wa kigeni ambao wanatarajiwa kutua nchini hivi karibuni na kujiunga na kikosi kwa ajili ya maandalizi ya mchezo huo mkubwa.

Kamwe ameeleza kuwa nyota hao wawili watakuwa tayari kabla ya Yanga kusafiri kwenda Misri, ambapo timu hiyo itavaana na Al Ahly Januari 23, 2026, katika mchezo wa hatua ya makundi unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.

Amefafanua kuwa kabla ya Januari 21, siku ambayo kikosi kitapanda ndege kuelekea Misri, klabu itawatambulisha rasmi wachezaji hao wawili ili wawe sehemu ya kikosi kitakachosaka matokeo chanya ugenini.

Akizungumzia ushiriki wa Yanga kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi, Kamwe amesema lengo halikuwa kushinda kombe hilo bali lilikuwa ni kutumia mashindano hayo kama sehemu ya maandalizi, hatua ambayo imesaidia kufanikisha malengo ya kiufundi ya timu.

“Wachezaji wetu wote, wakiwemo waliokuwa kwenye majukumu ya timu za Taifa, wamepata nafasi ya kucheza mechi za ushindani kwa ajili ya kuongeza utimamu na maandalizi kabla ya kukutana na Al Ahly,” amesema Kamwe.

Ameongeza kuwa Yanga pia inatarajia kucheza mechi ya Ligi Kuu baada ya ratiba kupangwa vizuri, jambo litakalosaidia zaidi katika maandalizi ya mwisho kuelekea mchezo huo wa Ligi ya Mabingwa Afrika.

BAHATI KUKUFATA ULIPO NA MERIDIANBET, KASINO

0

Meridianbet imekuja na mtazamo tofauti kabisa kwa kuzindua Non-Stop Win&Go Drop, mpango unaolenga kumweka mchezaji katikati ya tukio muda wote. Hapa, dhana ya kusubiri kwa muda mrefu imeondolewa, na nafasi za kushinda zinakuja kwa mpangilio unaoendana na kasi ya maisha ya kila siku.

Moja ya nguzo kuu za kampeni hii ni uwepo wa tiketi za bure zinazotolewa kila siku. Tiketi hizi zinampa mchezaji fursa ya kushiriki kwenye Win&Go bila kutumia fedha zake, hivyo kuifanya burudani iwe nyepesi na inayofikiwa na wengi zaidi. Ni njia ya kufurahia mchezo bila shinikizo.

Tofauti na michezo mingi ya kasino, Win&Go umebuniwa kwa kuzingatia muda wa mchezaji. Unachagua namba zako, unasubiri kwa muda mfupi, na matokeo yanapatikana haraka. Mfumo huu unaifanya kila raundi kuwa tukio fupi lenye msisimko wake binafsi.

Meridianbet haikuachi nyuma, kuna michezo mbalimbali ya kasino mtandaoni pamoja na mechi za kimataifa za kubashiri zenye odds bomba zinazokuongezea nafasi ya kuongeza kipato chako kila siku. Kujiunga ni rahisi. Tembelea meridianbet.co.tz au piga *149*10#.

Kwa kuondoa hofu ya kupoteza fedha kupitia tiketi za bure, Meridianbet imeunda mazingira rafiki kwa wachezaji wanaoanza na hata wale wenye uzoefu. Mchezaji anapata nafasi ya kujaribu, kuelewa mchezo na kufurahia ushindi bila vikwazo vya kawaida vinavyokwamisha wengi.

Kwa kuunganisha Non-Stop Win&Go Drop na michezo mingine ya kasino pamoja na chaguo za kubashiri michezo ya kimataifa, Meridianbet inaendelea kujijenga kama mshirika wa burudani ya kila siku. Ni jukwaa linaloleta ubunifu, msisimko na fursa katika sehemu moja, likifanya kila dakika kuwa na maana mpya.

SIMBA IKO NJIANI KUREJESHA HESHIMA, AHMEDY

0

MENEJA wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally, amesema ana imani kubwa kuwa timu yao itafanya vizuri na hatimaye kurejesha heshima yake kwa kutwaa taji kubwa hapa nchini, licha ya kipindi kigumu walichopitia katika misimu ya hivi karibuni.

Amesema kwa msimu wa tano mfululizo Simba haijafanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, sambamba na kushindwa kutwaa Kombe la Mapinduzi, lakini akasisitiza kuwa kila jambo lina wakati wake na mafanikio hayaji kwa pupa.

Ahmed amewataka mashabiki wa klabu hiyo kuwa wavumilivu, akieleza kuwa ana uhakika Simba itarejea kwenye mstari wa ushindi na kunyakua kombe kubwa, licha ya kupoteza uhalisia wa kutwaa mataji kwa kipindi cha miaka mitano.

Akizungumza kuhusu ushiriki wa Simba katika Kombe la Mapinduzi, Ahmed alisema walikuwa na malengo mawili makubwa, ikiwemo kumpa nafasi kocha mkuu Steve Barker kuwajua wachezaji wake na mfumo wa timu.

Alifafanua kuwa Barker ni kocha mpya aliyeanza kazi rasmi Desemba 28, na kufikia Januari 3, 2026 Simba tayari ilikuwa ikicheza mechi za Kombe la Mapinduzi, hali iliyomnyima muda wa kutosha wa kukaa na kikosi na kukiweka sawa.

“Tungefurahi kutwaa Kombe la Mapinduzi kama ingetokea, lakini haikuwa bahati yetu. Hatuna sababu ya kujilaumu, badala yake tunaendelea kusonga mbele na mipango yetu ya baadaye, ikiwemo kuandaa timu kwa mashindano mengine,” amesema Ahmed.

Kwa sasa, kikosi cha Simba kimeingia kambini kikijiandaa na mchezo muhimu wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Esperance ya Tunisia, huku matarajio yakiwa ni kufanya vizuri na kuanza safari mpya ya mafanikio.

SIMBA YAVIZIA NYOTA WAWILI WA KIMATAIFA

0

NYOTA wawili wa kimataifa, Libasse Gueye na Khadim Diaw, wanatarajiwa kutua nchini muda wowote kuja kwa ajili ya kukamilisha taratibu za kusaini mikataba ya kuitumikia klabu ya Simba SC, ikiwa ni sehemu ya mipango ya kuimarisha kikosi cha timu hiyo.

Katika dirisha dogo la usajili, Simba imekuwa ikifanya mambo yake kwa siri kubwa, ikilenga kuongeza ubora wa kikosi kuelekea mashindano muhimu yaliyopo mbele yao, ikiwemo Ligi ya Mabingwa Afrika na michuano mingine ya ndani.

Imeelezwa kuwa Libasse Gueye, anayekipiga katika nafasi ya kiungo mshambuliaji kutoka klabu ya Teungueth FC ya Senegal, yuko tayari kutua nchini muda wowote kwa ajili ya kukamilisha zoezi la usajili na kuungana rasmi na wekundu hao wa Msimbazi.

Chanzo cha kuaminika kimesema kuwa viongozi wa Simba wamehakikisha wanaboresha kikosi kulingana na mahitaji ya benchi la ufundi.

“ Gueye akiwa miongoni mwa wachezaji waliokuwa wakihitajiwa pia na klabu ya USM Alger, lakini Simba imefanikiwa kushinda mbio za kupata saini yake baada ya kufikia makubaliano na klabu pamoja na mchezaji,” amesema.

Ameongeza kuwa  Gueye aliwahi kuwa sehemu ya kikosi cha timu ya Taifa ya Senegal katika michuano ya AFCON,  aliibuka mchezaji bora wa mechi katika pambano dhidi ya Nigeria, jambo linaloonyesha ubora wake uwanjani.

Kwa upande wa Khadim Diaw, ambaye ni beki wa kushoto wa timu ya Taifa ya Mauritania, naye ni miongoni mwa usajili uliolengwa na Simba kwa lengo la kuimarisha safu ya ulinzi na kuongeza ushindani ndani ya kikosi.

Mtoa habari huyo amesisitiza kuwa usajili wote unaofanywa na Simba umezingatia mahitaji ya benchi la ufundi, huku lengo kuu likiwa ni kujenga kikosi imara kitakachoweza kushindana kwa mafanikio katika mashindano yote yanayowakabili msimu huu.

TUSUA KIJANJA NA MERIDIANBET

0

Siku ya leo inaenda kubadilisha maisha yako moja kwa moja kwani mechi kibao zipo uwanjani na nafasi ya kuondoka na ushindi ipo mikononi mwako. Ingia kwenye akaunti yako na uanze kubeti sasa.

SAUDI PROFESSIONAL itaendelea ambapo Al Qadsiah atamenyana vikali dhidi ya Al Feiha ambapo tofauti ya pointi kati yao hadi sasa ni 15. Mara ya mwisho kukutana hawa wawili, kila mtu aliondoka na pointi 3 mechi za mbili msimu uliopita. Tandika jamvi lako hapa.

Al Ahli ataumana dhidi ya Al Taawon ambao wapo nafasi ya 3 huku wenyeji woa wakiwa nafasi ya 5 kwenye msimamo wa ligi. Meridianbet wameipa mechi hii ODDS KUBWA lakini pia ina machaguo zaidi ya 1000. Je wewe unampa nani nafasi ya kuondoka na mkwanja wa maana?. Beti hapa.

Pesa ipo kwenye michezo ya Kasino ya mtandaoni kama vile Keno, Aviator, Poker, Roulette,Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

CARABAO CUP hatua ya Nusu Fainali ambapo Chelsea atakipiga dhidi ya Arsenal na hii itakuwa ni London Derby. Mechi ya mwisho kukutana ilikuwa kwenye ligi ambapo walitoa sare. Ikumbukwe kuwa mara ya mwisho The Blues kupata ushindi mbele ya The Gunners ilikuwa ni mwaka 2021. Je nani kusonga mbele kwenye Fainali?. ODDS KUBWA zipo mechi hii. Suka jamvi hapa.

BUNDESLIGA kule Ujerumani inatarajiwa kuendelea kwa mechi kibao ambapo Wolfsburg atakipiga dhidi ya S.T Pauli ambapo mara ya mwisho kukutana kwenye mechi zao mbili walitoa sare yaani hakuna mabaye aliondoka na pointi 3. Je leo hii nani kuondoka na ushindi?. Bashiri hapa.

Pia bingwa mtetezi wa ligi hii FC Bayern Munich atakuwa ugenini kukiwasha dhidi ya FC Cologne ambao wapo nafasi ya 11 hadi sasa. Vijana wa Kompany wanahitaji ushindi mnono kwenye mechi hii kuendelea kujiweka kileleni. Je mwenyeji anaweza kumzuia bingwa kuchukua pointi 3?. Tandika jamvi hapa.

Naye RB Leipzig atakuwa nyumbani kusaka ushindi mkubwa dhidi ya Freiburg ambao hawapewi nafasi kubwa pale Meridianbet kuondoka na pointi 3 muhimu kabisa. Tofauti ya pointi kati yao hadi sasa ni 9 pekee. Pesa kubwa ipo kwenye mtanange huu na Meridianbet. Jisajili hapa.

Vilevile unaweza ukapiga pesa kwenye SERIE A kule Italia ambapo Napoli atakuwa  nyumbnai kusaka ushindi dhidi ya Parma ambao wapo nafasi ya 15 huku wageni wao wakiwa nafasi ya 3 kwenye ligi. Meridianbet wameipa mechi hii machaguo zaidi ya 1000. Bashiri hapa.

Wakati kinara wa ligi, Inter Milan yeye atakuwa pia atakuwa nyumbani kupepetana dhidi ya US Lecce ambao wanashika nafasi ya 16 kwenye msimamo wa ligi. Msimu uliopita wawili hawa walipokutana Milan waliondoka na ushindi mechi zote mbili. ODDS KUBWA na machaguo zaidi ya 1000 yapo hapa. Jisajili hapa.

OKELLO NI MCHEZAJI WA KUAMUA MATOKEO, LULE

0

ALIYEKUWA  kocha wa Singida Black Stars, Mganda Mathias Lule, amemwagia sifa mchezaji Allan Okello akisema ni miongoni mwa wachezaji wenye ubora wa hali ya juu wanaoweza kuleta tofauti kubwa ndani ya uwanja.

Okello amesaini mkataba wa miaka miwili Yanga akitokea katika klabu ya Vipers ya Uganda na tayaru yupo nchini kwa ajili ya kuanza majukumu yake ndani ya klabu hiyo.

Lule ambaye amewahi kuwa kocha wa timu ya Taifa ya Uganda, amesema Okello ni mchezaji mwenye ufundi mzuri (good technique) unaomwezesha kumiliki mpira kwa uhakika, kucheza kwa kujiamini na kufanya maamuzi sahihi katika nyakati ngumu za mchezo.

“Moja ya sifa kubwa za Okello ni uwezo wake wa kuamua matokeo ya mechi wakati wowote, hasa kutokana na akili yake ya mchezo na uwezo wa kusoma nafasi, jambo linalomfanya kuwa hatari kwa wapinzani,” amesema Lule.

Amesema  Okello ni bingwa wa mipira ya adhabu (set pieces), ana uwezo mkubwa wa kufunga au kuandaa mabao kupitia mipira ya faulo na kona, jambo linaloongeza silaha muhimu kwa timu yoyote anayochezea.

Amesisitiza  kuwa ni mchezaji wa timu, anayejali maslahi ya wenzake na anayecheza kwa kushirikiana badala ya kujitafutia sifa binafsi.

Amesema mchezaji wa aina ya Okello ni hazina  kwa kikosi chochote, kwani anaunganisha ufundi, nidhamu na mshikamano wa timu, vitu ambavyo ni msingi wa mafanikio ya muda mrefu katika soka la ushindani.

KUTOKA MOROCCO HADI PEMBA KUIPA YANGA UBINGWA

0

BAADA ya kusubiri kwa miaka minne, klabu ya Yanga SC imerejea  kwa kutwaa ubingwa wa Kombe la Mapinduzi 2026, baada ya kuibuka na ushindi wa penalti 5-4 dhidi ya Azam FC katika mchezo wa fainali uliochezwa Uwanja wa Gombani, Pemba.

Mchezo huo wa fainali ulikuwa na ushindani mkubwa kuanzia dakika ya kwanza hadi ya mwisho, huku timu zote zikionesha nidhamu ya hali ya juu ya kiufundi.

Dakika 90 za kawaida zilimalizika kwa sare ya bila kufungana, hali iliyolazimu kuongezwa kwa dakika 30 za muda wa ziada, lakini bado hakuna timu iliyoweza kutikisa nyavu za mpinzani wake.

Katika kipindi cha kwanza cha mchezo, Azam FC na Yanga zilishambuliana kwa zamu, kila timu ikitafuta bao la mapema, lakini umakini wa walinzi na makipa ulifanya kipindi hicho kumalizika kwa sare ya 0-0.

Hali hiyo iliendelea hadi kipindi cha pili na muda wa ziada, ambapo nafasi chache zilizopatikana zilishindwa kutumika ipasavyo.

Yanga walipata nafasi ya wazi ya kufunga kupitia mkwaju wa penalti ndani ya dakika za kawaida baada ya beki wa Azam FC kucheza mpira wa mkono, hata hivyo Pacome Zouzoua alikosa penalti hiyo, na kuifanya timu yake kuendelea kusubiri ushindi hadi hatua ya mikwaju ya penalti.

Katika hatua ya penalti, Yanga walionyesha utulivu na umakini mkubwa, huku mikwaju yao ikifungwa na Emmanuel Mwanengo, Prince Dube, Pacome Zouzoua, Mudathir Yahya pamoja na Bakari Mwamnyeto aliyepiga penalti ya mwisho na kuipa Yanga ushindi wa 5-4 dhidi ya Azam FC.

Shujaa wa Yanga, Mwamnyeto, alikuwa na safari ndefu kutoka Morocco hadi Pemba, baada ya kujiunga na kikosi hicho jana akitokea katika majukumu ya timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) iliyokuwa ikishiriki fainali za AFCON nchini Morocco, na mchango wake ulihitimishwa kwa penalti ya ushindi.

Kwa ushindi huo, Yanga wametawazwa mabingwa wa Kombe la Mapinduzi kwa mara ya kwanza tangu walipotwaa taji hilo mwaka 2021, ushindi unaowapa morali kubwa kuelekea michuano ijayo ya ndani na kimataifa.

SIMBA KUPEWA FURAHA NA SIMBA QUEENS

0

WAKATI mashabiki wa Simba wakisalia na maswali kuhusu mwenendo wa timu ya wanaume, timu ya wanawake ya Simba Queens imeendelea kuwa chanzo cha tabasamu kwa Wanasimba kwa kuonyesha kiwango bora na ushindi wa kuvutia kwenye Ligi ya Wanawake Tanzania.

Simba Queens waliendeleza mwendo huo mzuri baada ya kuibuka na ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya Tausi FC katika mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa KMC Complex, Mwenge jijini Dar es Salaam, ambapo Simba walikuwa wenyeji wa mchezo huo.

Nyota wa mchezo huo alikuwa Aisha Mnuka aliyefunga mabao mawili, akionyesha ubora wake mbele ya lango, huku bao la tatu likifungwa na Jentrix Shikangwa na kuhitimisha karamu ya mabao kwa Simba Queens.

Katika kipindi cha kwanza, Simba Queens walionyesha udhibiti mkubwa wa mchezo na kufanikiwa kutamatisha dakika 45 za mwanzo wakiwa mbele kwa mabao 3-0, hali iliyowapa utulivu na kuonyesha tofauti ya ubora kati yao na wapinzani wao Tausi FC.

Katika michezo mingine ya ligi hiyo, Yanga Princess walipata ushindi wakiwa ugenini baada ya kuifunga Fountain Gate Princess kwa mabao 5-4, ushindi uliothibitisha pia ushindani mkubwa unaoendelea kushamiri kwenye ligi hiyo.

Kwa upande mwingine, mabingwa watetezi JKT Queens waliendeleza ubabe wao baada ya kuibuka na ushindi mwembamba wa bao 2-0 dhidi ya wenyeji wao Ruangwa Queens, matokeo yaliyozidi kuipa ligi hiyo mvuto na ushindani mkubwa.

CHEZA ZOMBIE APOCALYPSE MIZUNGUKO BURE

0

Katika ulimwengu wa burudani ya kidijitali, Meridianbet imechagua njia tofauti kwa kuwasilisha Zombie Apocalypse kama hadithi ya ubunifu kuliko ofa ya kawaida. Kampeni hii inaangazia namna michezo ya kisasa inavyoweza kuunganisha simulizi, teknolojia na burudani ili kumfanya mtumiaji ajisikie sehemu ya dunia inayocheza, si mtazamaji wa pembeni.

Tofauti na michezo inayotegemea bahati pekee, Zombie Apocalypse inajengwa juu ya simulizi linaloendelea. Mchezaji anaingizwa katika mazingira yanayobadilika hatua kwa hatua, ambapo kila mzunguko unaongeza mvutano na matarajio. Mbinu hii ya kusimulia hadithi inaifanya michezo ya kasino kuonekana kama uzoefu kamili wa burudani, si kitendo cha papo kwa papo.

Meridianbet inakuja na michezo ya kasino, mechi zenye odds tamu, na njia rahisi za kujiunga na kucheza. Ukiwa na Meridianbet, kila siku ni nafasi mpya ya kuongeza kipato chako na kufurahia burudani bila mipaka. Tembelea meridianbet.co.tz au piga *149*10#

Mfumo wa mizunguko ya bure umeundwa kuongeza muda wa uzoefu na kutoa nafasi ya kuchunguza vipengele vya mchezo kwa kina zaidi. Utapata hadi mizunguko 50 ya bure kila unapocheza mizunguko 100 ya pesa halisi. Mizunguko hii ya bure inatolewa siku inayofuata baada ya kucheza mizunguko hii 100.

Mchango wa Expanse Studio unaonekana wazi katika ubora wa michoro, sauti na mwendo wa mchezo. Mandhari ya giza, athari za sauti na uhuishaji wa kisasa vinaonyesha jinsi teknolojia ya michezo inavyoweza kuunda hali halisi ya kihisia. Ni mfano wa jinsi sanaa ya kidijitali inavyozidi kuchukua nafasi muhimu katika tasnia ya michezo.

Zombie Apocalypse ni sehemu ya mkakati mpana wa Meridianbet wa kutoa burudani iliyopangwa kwa watu wazima wanaotafuta uzoefu wa kisasa na uliodhibitiwa. Kampeni hii inaweka mkazo kwenye matumizi ya kuwajibika, ikikumbusha kuwa michezo ya aina hii inalenga burudani na inapaswa kufurahiwa kwa mipaka inayokubalika kisheria.

329,001FansLike
12,344FollowersFollow
16,900SubscribersSubscribe

EDITOR PICKS