Thursday, January 22, 2026
Home Blog

STRAIKA PRISONS ATUA COASTAL

0

ALIYEKUWA mshambuliaji wa maafande wa Tanzania Prisons, Abdulkarim Segeja, amekamilisha usajili wa kujiunga na Coastal Union kwa mkataba wa miezi sita utakaomweka ndani ya kikosi hicho cha Wagosi wa Kaya hadi mwisho wa msimu huu.

Nyota huyo aliyejiunga na Prisons katika dirisha dogo la Januari 2023 akitokea Copco ya jijini Mwanza, alisaini mkataba wa miaka miwili, japo mazungumzo ya kuongeza mwingine yaligonga mwamba na kuamua kutafuta changamoto mpya.

Akizungumza na Mwanaspoti, Segeja alisema amefikia uamuzi wa kujiunga na Coastal Union katika dirisha hili dogo la usajili huku akiamini timu hiyo itampa nafasi zaidi ya kucheza na kuonyesha kipaji tofauti na alikotoka.

“Kuna mambo ambayo awali hayakwenda vizuri na Prisons, baada ya kukaa na menejimenti yangu tukaona tuvunje rasmi mkataba uliobakia ili niangalie changamoto mpya, hivyo ni kweli nimekamilisha taratibu za kujiunga na Coastal Union,” alisema.

Aidha, mshambuliaji huyo alisema licha ya kukaa nje kwa takribani miezi miwili bila ya kucheza mechi za ushindani, lakini bado alikuwa anaendelea na mazoezi binafsi, ambapo kwa hatua aliyopo anaamini atakuwa chachu ya mafanikio ya Coastal Union.

Nyota huyo wakati anajiunga na Prisons alitokea Copco ya jijini Mwanza iliyokuwa inashiriki Ligi ya Championship, ambapo kwa msimu wa 2023-2024, aliifungia mabao manane, huku akicheza timu mbalimbali ikiwemo TRA United zamani Tabora United.

Pia, Mwanaspoti linatambua nyota wengine walio katika mazungumzo ya kujiunga na Coastal Union ni beki wa kati wa Mbuni ya Arusha inayoshiriki Ligi ya Championship, Ambokise Mwaipopo, aliyejiunga na kikosi hicho msimu huu akitokea KenGold.

Mbali na Ambokise, Coastal Union inafuatilia pia saini ya aliyekuwa beki wa kulia wa Geita Gold, Polisi Tanzania, Dodoma Jiji na JKT Tanzania, George Aman Wawa, ili kwenda kuongezea nguvu kikosi hicho katika dirisha hili la usajili.

MIDO SINGIDA ANUKIA AZAM

0

MABOSI wa Azam wanaangalia uwezekano wa kumsajili kiungo mshambuliaji wa Singida Black Stars raia wa Ivory Coast, Idriss Diomande, baada ya nyota huyo aliyehusishwa pia kuhitajika na Simba katika dirisha hili dogo dili lake kugonga mwamba.

Nyota huyo alikuwa akihusishwa kujiunga na Simba kwa ajili ya kuchukua nafasi ya kiungo mshambuliaji, Jean Charles Ahoua aliyejiunga na CR Belouizdad ya Algeria, ingawa baada ya Clatous Chama kurejea kikosini hapo, dili lake limeota mbawa.

Baada ya Chama kurejea Simba, uongozi wa Azam umefungua rasmi mazungumzo ya kumuhitaji kiungo huyo aliyejiunga na Singida Black Stars Agosti 20, 2025, akitokea Zoman FC ya kwao Ivory Coast, huku akisaini mkataba wa miaka mitatu hadi Juni 30, 2028.

Chanzo kutoka Azam kimeliambia Mwanaspoti, kinaheshimu kipaji cha mchezaji huyo, japo suala la usajili huo itategemea na mkataba wake uliopo, ingawa kipaumbele cha kwanza kikosini humo alikuwa asajiliwe winga wa Dodoma Jiji, Benno Ngassa.

“Tunaendelea kuangalia hali iliyopo kwa sababu bado dirisha liko wazi, hivyo lolote linaweza likatokea, kikubwa sisi tunazingatia ripoti ya benchi la ufundi kwa lengo la kuhakikisha tunafanya vizuri msimu huu,” kilisema chanzo hicho.

Hata hivyo, Mwanaspoti linatambua uongozi wa Singida hauko tayari kumuachia mchezaji huyo kirahisi kuondoka kutokana na mashindano mbalimbali inayoshiriki, hususani baada ya kumwachia kiungo mshambuliaji, Clatous Chama aliyejiunga na Simba.

Mwanaspoti linatambua Singida inaweza ikamwachia nyota huyo ili kuendana na idadi ya wachezaji 12 wa kigeni, kwa sababu hivi sasa inakaribia pia kumsajili kiungo mshambuliaji, Linda Mtange anayetokea FC Les Aigles du Congo ya kwao DR Congo.

MKONGOMANI KURITHI NAFASI YA CHAMA

0

MUDA mchache baada ya Singida Black Stars kukubali kumwachia Clatous Chama atimkie Simba, uongozi wa klabu hiyo upo kwenye hatua za mwisho kukamilisha usajili wa kiungo Mkongomani, Linda Mtange kutoka Aigles Du Congo.

Chama aliitumikia Singida Black Stars kwa miezi sita akitua mwanzoni mwa msimu huu akitokea Yanga na alihudumu kwa msimu mmoja akitokea Simba.

Chanzo cha kuaminika kutoka Singida Black Stars, kililiambia Mwanaspoti, wamemwachia Chama baada ya kupata mbadala sahihi ambaye ataweza kuipa vitu vingi zaidi ndani ya timu yao.“Ni kweli Chama anaondoka Singida Black Stars dirisha hili na tayari tumeshampata mbadala wake ambaye tunaamini ataweza kufanya mambo makubwa ndani ya timu, makubaliano ya kumalizana na kiungo huyo yapo katika hatua za mwisho.

“Kuhusu Chama tumemalizana vizuri na makubaliano ya pande zote mbili pia yamekwenda vizuri, kilichobaki sasa ni kila pande kukamilisha mchakato tuliokubaliana,” kilisema chanzo hicho.

Chanzo hicho kilisema mabadiliko yanayofanywa yanazingatiwa na benchi la ufundi ambalo tayari limeona ubora wa nyota waliotoka akimtaja Nickson Kibabage na Chama na kuamua kufanya uamuzi wa haraka kusajili warithi wao.

“Kibabage kaondoka tayari tulikuwa tumeongeza nguvu eneo lake kwa kumnasa beki kutoka KMC, Abdallah Said ‘Lanso’ na sasa Chama katoka chaguo ni Mtange,” kimebainisha chanzo hicho.

NI VITA YA CHIPO, MAXIME LIGI KUU BARA

0

MIEZI 10 na siku 9 imepita kufikia leo Januari 21, 2026 na tunakwenda kushuhudia tena mtanange baina ya Mtibwa Sugar dhidi ya Mbeya City, huku safari hii ikiwa ni katika Ligi Kuu Bara. Uwanja wa Jamhuri uliopo Dodoma, utaamua vita hiyo ya makocha wawili, Yusuf Chipo na Mecky Maxime kuanzia saa 10:00 jioni.

Timu hizo zilizomaliza nafasi mbili za juu katika msimamo wa Ligi ya Championship msimu uliopita 2024-2025 na kukata tiketi ya moja kwa moja kurejea Ligi Kuu Bara, zinakutana kwenye mechi ya ligi kila moja ikihitaji matokeo mazuri.

Kwa Mbeya City inayonolewa na Mecky Maxime, inabaki kuwa deni kubwa kwao kwani msimu uliopita dhidi ya Mtibwa Sugar zilipokutana Championship, haikupata ushindi zaidi ya kuambulia pointi moja zilipotoka 0-0, Februari 9, 2025 kwenye Uwanja wa Sokoine, Mbeya ikiwa ni mechi ya raundi ya 18 duru la pili.

Kabla ya hapo, Mtibwa ilishinda nyumbani mabao 2-0 dhidi ya City, Oktoba 5, 2024 ikiwa ni mechi ya raundi ya tatu.

Mwisho wa msimu huo, ilishuhudia Mtibwa Sugar ikimaliza kinara wa Ligi ya Championship ikifikisha pointi 71 baada ya kucheza mechi 30, ikishinda 22, sare tano na kupoteza tatu, huku ikifunga mabao 58 na nyavu zake kutikiswa mara 18.

City ilikuwa ya pili na pointi 68, ikishuka dimbani mara 30, ikishinda mechi 20, sare nane na kupoteza mbili, ikifunga mabao 68 na kuruhusu 26.

Timu hizo baada ya kwenye Ligi ya Championship Mtibwa Sugar kufanya vizuri, City ikaenda kulipa kisasi Machi 13, 2025 katika mechi ya hatua ya 16 bora ya Kombe la Shirikisho (FA) iliposhinda 2-1 na kufuzu robo fainali, ikaenda kukwaa kisiki cha Simba. Hiyo ndiyo ilikuwa mara ya mwisho City kucheza dhidi ya Mtibwa.

Msimu huu Ligi Kuu, Mtibwa Sugar inayonolewa na Yusuf Chipo, ipo juu ya City tena kwa tofauti kubwa ya pointi na nafasi.

Mtibwa kabla ya mechi mbili zilizochezwa jana, ilikuwa nafasi nane ikikusanya pointi 11 baada ya kucheza mechi tisa, ikishinda mbili, sare tano na kupoteza mbili, ikifunga mabao matano na kuruhusu idadi hiyo.

City haijaanza vizuri sana msimu huu kulinganisha na mpinzani wake kwani inakamata nafasi ya 13 ikikusanya pointi nane zilizotokana na kushinda mechi mbili na sare mbili, ikipoteza nane. Imefunga mabao saba na kuruhusu 13 ikishuka dimbani mara kumi.

Rekodi zinaonyesha kuwa, msimu wa mwisho 2022-2023 timu hizo kukutana Ligi Kuu Bara kabla ya kila moja kushuka kwa wakati wake, City ilifanya vizuri dhidi ya Mtibwa ikikusanya pointi nne baada ya kutoka 2-2, kisha ikashinda bao 1-0.

Tangu msimu wa 2013-2014, timu hizo zimekutana mara 20, Mtibwa Sugar ikishinda sita, City nayo imeibuka na ushindi mara tano, huku sare zikiwa tisa.

Jumla ya mechi 23 zimechezwa baina ya timu hizo katika Ligi Kuu (20), Championship (2) na Kombe la FA (1), huku ikishuhudiwa mara tano pekee zikitoka uwanjani bila ya nyavu kutikiswa, hivyo zinapokutana, ishu ya kufunga bao ipo kwa asilimia kubwa.

Kocha Mecky Maxime, huu ni mtihani wake wa kwanza tangu akabidhiwe mikoba ya kuinoa timu hiyo Desemba 7, 2025 akichukua nafasi ya Malale Hamsini.

Maxime ana mtihani wa kuhakikisha City inapata matokeo mazuri kwani mechi yano za mwisho, imekusanya pointi moja, ilipotoka sare ya mabao 2-2 dhidi ya JKT Tanzania, baada ya hapo ikafungwa na Mashujaa (1-0), ikachapwa 2-0 na Coastal Union, kisha ikapokea kipigo cha 1-0 kutoka Namungo, ikahitimisha na kufungwa 3-0 dhidi ya Simba.

Mtibwa mechi tano za mwisho imekusanya pointi sita ikipoteza mechi moja pekee dhidi ya Yanga ilipofungwa 2-0. Baada ya hapo, matokeo yalikuwa hivi; KMC 0-0 Mtibwa, Mtibwa 2-1 TRA, JKT 0-0 Mtibwa na Simba 1-1 Mtibwa.

HIKI HAPA ALICHOSEMA MAYELE BAADA YA CHAMA KURUDI TENA SIMBA….

0

STRAIKA wa Pyramids ya Misri na timu ya taifa ya DR Congo, Fiston Mayele, ameonyesha wazi furaha yake baada ya Clatous Chama, kurejea katika klabu ya Simba.

Kupitia sehemu ya maoni mitandaoni baada ya Simba kutangaza kumrejesha Chama, Mayele aliandika ujumbe uliovuta hisia za mashabiki wengi huku wengine wakitaka naye atue Msimbazi.

“The Best Number 10 Is Back, Mwamba wa Lusaka good luck!,” amekomenti Mayele katika chapisho la Simba kwenye instagram wakati ikimtambulisha Chama akiwa na maana ya kwamba namba kumi bora amerejea kisha akamtakia kila la kheri.

Baadhi ya waliochangia katika komenti ya Mayele kuhusu usajili huo wa Chama wameandika maoni mbalimbali wakimtaka mshambuliaji huyo aliyewahi kuwa mfungaji bora wa Ligi Kuu Bara 2022–23 na Mfungaji bora wa Kombe la Shirikisho Afrika 2022–2023 wakati anaichezea Yanga, atue Simba akitokea Pyramids.

“Bado wewe”

“Sasa mpaka Mayele anamkubali daaah ila chama 🔥🙌🔥”

“Ungekuja wewe mimi ningefurahi sana hapa Simba yani mambo yangekuwa mazuri sana.”

“Bado wewe tunakusubiri.”

“Rudi kaka utusaidie Wanasimba hatuelewi.”

“Tunakusubiri na wewe Mzee wa kutetema uje Unyamani.”

Ujumbe huo umeonyesha heshima kubwa kwa Chama, ambaye ni mmoja wa viungo mahiri waliowahi kuichezea Simba na kuacha alama kubwa katika Ligi Kuu ya Tanzania.

Mbali na Chama, mastaa wengine walioonyesha hisia zao juu ya usajili huo ni kiungo wa zamani wa Yanga anayecheza Singida Black Stars, Khalid Aucho aliyeandika ujumbe wa kumpongeza na kumtakia kila la kheri: “Congratulations brother and good luck 🙏🙏🙏🙏❤️❤️.”

Naye mshambuliaji wa zamani wa Simba na Namungo, Meddie Kagere ameandika ujumbe wa kumkaribisha: “Welcome back @realclatouschama.”

Wakati huohuo, kiungo wa zamani wa Simba, Pape Ousmane Sakho, naye amendika: “Wow wow wow🔥🔥 @realclatouschama.”

Winga wa zamani wa Simba na Yanga, Emmanuel Okwi naye ameandika: “Karibu tena nyumbani @realclatouschama.”

Huku beki wa zamani wa Simba na Azam, Pascal Wawa amemkaribisha Chama kwa kuandika: “Welcome back home capitaine Mario.”

Kwa sasa, Chama ni Mnyama tena, na mashabiki wa Simba wanaamini kurejea kwake ni baraka kubwa kwa klabu hiyo kuelekea mapambano yao ya msimu huu.

BETI MECHI ZA UEFA NA MERIDIANBET

0

Kupiga pesa ni rahisi sana ndani ya UEFA endapo utaamua kubashiri mechi zote hapa leo. Wakali wa ubashiri wanakwambia kuwa nafasi ya wewe kuondoka na mshindo hii hapa. Tandika jamvi lako hapa.

Vijana wa Darajani Chelsea wataumana dhidi ya Pafos ambao wameshinda mechi moja pekee kati ya 6 huku The Blues wao wakishinda mechi 3. Nafasi ya kuondoka na ushindi pale Meridianbet wamepewa wenyeji. Je vipi wewe beti yako leo unaiweka kwa nani?. Bashiri hapa.

Arne Slot na Liverpool yake watakuwa ugenini kusaka ushindi dhidi ya Marseille ya kule Ufaransa. Timu hizi mbili mpaka sasa zimetofautiana pointi 3 pekee huku wakali wa ubashiri Meridianbet wakiipa mechi hii ODDS KUBWA. Suka jamvi hapa.

Slavia Prague atakuwa nyumbani kukiwasha dhidi ya Barcelona ya Hans Flick ambao ushindi wa mechi hii ni muhimu sana kwao ili waweze kushika nafasi nzuri. Mwenyeji pia anahitaji ushindi wa kila namna kwenye mechi hii. Je vijana wa Hans watatokaje?. Tengeneza jamvi hapa.

Piga pesa kwenye michezo ya Kasino ya mtandaoni kama vile Keno, Aviator, Poker, Roulette,Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kwa upande wa Atalanta wao watakipiga dhidi ya Athletic Bilbao ambao hawapewi nafasi ya kushinda mechi hii ya leo. Kila timu inahitaji ushindi kwenye mechi hii ya leo huku pointi 8 ndio inayowatofautisha hadi sasa. Meridianbet wameipa mechi hii ODDS KUBWA. Ingia na ubeti hapa.

Vijana wa Vicent Kompany Bayern Munich wao watakuwa kibaruani kukiwasha dhidi ya Union Saint Gilloise ambao wameshinda mechi 2 pekee kwenye zile 6 walizocheza, huku wenyeji wao kwenye mechi 6 wameshinda 5 na kutoa sare moja tuu. Meridianbet wanampa nafasi ya kushinda Bayern. Wewe unampa nani nafasi ya ushindi?. Jisajili hapa.

Galatasaray wao watamualika kwake Atletico Madrid ya Diego Simeone ambao mpaka sasa wapo nafasi ya 8 huku wenyeji wao wakiwa nafasi ya 18. Tofauti ya pointi kati yao hadi sasa 3 pekee. Mara ya mwisho kukutana kati yao ilikuwa ni mwaka 2015 ambapo vijana wa Simeone waliondoka na ushindi mechi zote 2. Bashiri hapa.

Juventus uso kwa uso dhidi ya Benfica kutoka kule Ureno ambao kwenye mechi 6 walizocheza hadi sasa wameshinda 2 halikadhalika Bibi Kizee naye kashinda mechi 2 pekee. Tofauti ya pointi kati yao hadi sasa ni 3 pekee. Je nani kuondoka na pointi tatu katika dimba la Allianz?. Jisajili hapa.

AVIATOR YATUMIKA KAMA DARAJA NA MERIDIANBET

0

Katika zama ambazo michezo ya mtandaoni imekuwa sehemu ya maisha ya kila siku, Meridianbet imechagua njia tofauti ya kuwasiliana na wachezaji wake. Kupitia mchezo wa Aviator, Meridianbet imeambatanisha mchezo huu na zawadi ya kisasa ya Samsung Galaxy A26, simu inayokidhi mahitaji ya mawasiliano na matumizi ya kidijitali ya leo.

Aviator haichezwi kwa mazoea, bali kwa umakini. Ni mchezo unaomlazimisha mchezaji kusoma mwelekeo wa muda, kupima hatari na kuchukua hatua kwa wakati sahihi. Ndege inapopaa kwa kasi isiyotabirika, kila sekunde inakuwa muhimu. Hapa ndipo tofauti kati ya mchezaji wa kawaida na mchezaji makini hujitokeza, kwani ushindi hutegemea uamuzi kuliko bahati.

Kwa kuzingatia hilo, Meridianbet imeamua kutambua juhudi za wachezaji wake kwa njia ya kipekee. Imechagua kutoa Samsung A26 kama zawadi ya ziada kwa washiriki wa Aviator. Hii inaifanya promosheni hii kuwa rafiki kwa mchezaji, kwani hakuna kinachobadilika kwenye namna ya kucheza, isipokuwa thamani ya kile unachoweza kushinda.

Meridianbet haikuachi nyuma, kuna michezo mbalimbali ya kasino mtandaoni pamoja na mechi za kimataifa za kubashiri zenye odds bomba zinazokuongezea nafasi ya kuongeza kipato chako kila siku. Kujiunga ni rahisi! Tembelea meridianbet.co.tz au piga *149*10#.

Promosheni hii inawahusu wachezaji wote wanaotumia Meridianbet kupitia tovuti ya meridianbet.co.tz au programu yake rasmi. Ushiriki ni wa moja kwa moja, bila hatua za ziada wala taratibu ndefu. Unacheza Aviator kama kawaida, na kila ushindi unakuwa na maana zaidi kwa kuwa unaweza kuleta zawadi ya kifaa cha kisasa kinachotumika kila siku.

Kwa mtazamo mpana, Meridianbet inaonesha kuwa ubashiri wa kisasa haupaswi kuwa wa kubahatisha tu, bali wa kuleta thamani halisi kwa mchezaji. Kupitia Aviator na zawadi ya Samsung A26, kampuni hiyo inaunganisha maamuzi ya sekunde chache na matokeo ya muda mrefu, ikithibitisha kuwa uamuzi sahihi angani unaweza kubadilisha kabisa hali yako ardhini.

MNYAMA CHAMA AREJEA UNYAMANI

0

BAADA ya Klabu ya Simba SC kumtambulisha rasmi kurejea kwa kiungo mshambuliaji Clatous Chama, Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa klabu hiyo, Ahmed Ally, amesema kurejea kwa nyota huyo ni ishara kuwa kiongozi halisi wa kikosi amerejea nyumbani.

Chama amesaini mkataba wa mwaka mmoja kujiunga tena na Wekundu wa Msimbazi akitokea Singida Black Stars, ambapo alikuwa akitumikia klabu hiyo baada ya kumaliza mkataba wake wa awali wa mwaka mmoja. Awali, mchezaji huyo aliwahi pia kupitia Yanga kabla ya kurejea tena ndani ya Simba.

Ahmed alisema kurejea kwa Chama kunakwenda kurejesha heshima na ubora wa Simba, amesisitiza kuwa hakuna sehemu nyingine ambayo mchezaji huyo anaweza kuonyesha uwezo wake mkubwa kama ilivyo ndani ya klabu hiyo.

“Mwenda tezi na omo, marejeo ngamani. Kila kitu kizuri kimerejea ndani ya Simba. Karibu sana Mwamba, tulikuhitaji sana katika nyakati hizi,” alisema Ahmed huku akionyesha imani kubwa na mchango wa nyota huyo.

Ameongeza  kuwa furaha imerejea Msimbazi, Chama ni mchezaji mwenye ubora wa hali ya juu ambaye alipoondoka hakuweza kuonyesha kiwango chake cha kweli, lakini sasa amerudi nyumbani tayari kuendeleza yale ambayo mashabiki wa Simba wamezoea.

“Chama ni mkongwe ndani ya kikosi cha Simba, ni mchezaji aliyewahi kutupeleka robo fainali kwa mara ya kwanza. Amerudi kuwaambia wenzake kuwa sasa ni wakati wa kuipigania Simba kwa nguvu zote,” amesema.

Kwa mujibu wa Ahmed, kurejea kwa Chama ni hatua muhimu katika dhamira ya kurejesha heshima ya Simba,  kuwa kiongozi huyo amerejea kuongoza wenzake na kupambana kwa ajili ya bendera ya Msimbazi katika mashindano yote yanayokuja.

SIMBA YAPAA TUNISIA, CHAMA NDANI YA KIKOSI

0

KIKOSI cha wachezaji 22 wa Klabu ya Simba SC kimeondoka alfajiri ya leo kuelekea nchini Tunisia kwa ajili ya mchezo muhimu wa Kombe la Shirikisho Afrika, unaotarajiwa kuchezwa Januari 24 mwaka huu, katika mwendelezo wa hatua ya makundi ya michuano hiyo.

Safari hiyo ni sehemu ya maandalizi ya Simba katika kurejesha matumaini ya kufanya vizuri baada ya mwanzo mgumu, huku benchi la ufundi likifanya maboresho kadhaa kwenye kikosi chake kwa lengo la kuongeza ushindani na ufanisi uwanjani.

Kikosi hicho kimejumuisha mchanganyiko wa wachezaji wapya na wale waliokuwepo awali, akiwemo kiungo Clatous Chama ambaye amerejea rasmi Simba na kutambulishwa usiku wa jana akitokea Singida Black Stars, kisha kuungana moja kwa moja na kikosi kilichosafiri kwenda Tunisia.

Chama, aliyewahi kuitumikia Simba hapo awali kabla ya kujiunga na Yanga kwa mkataba wa mwaka mmoja, kisha Singida Black Stars, sasa amerejea tena Msimbazi akitarajiwa kuongeza ubunifu na uzoefu katika eneo la kiungo kuelekea mchezo huo mgumu.

Miongoni mwa wachezaji waliopo kwenye kikosi hicho ni makipa Hussein Abel, Alexander Erasto na Djibrilla Kassali.

Wengine ni Shomari Kapombe, David Kameta, Antony Mligo, Nickson Kibabage, Wilson Nangu, Rushine De Reuck, Ismael Toure, Vedastus Masinde, Yusuph Kagoma.

Naby Camara, Kibu Denis, Elie Mpanzu, Morice Abraham, Neo Maema, Libasse Gueye, Hussein Semfuko, Seleman Mwalimu pamoja na Jonathan Sowah.

Simba ilianza vibaya hatua ya makundi baada ya kupoteza michezo miwili ya awali, hali iliyowavunja moyo mashabiki wake.

Mabadiliko yaliyofanywa ndani ya kikosi na benchi la ufundi yameongeza matumaini mapya ya kupata matokeo chanya, kufufua kampeni ya timu hiyo na kuendelea kupigania nafasi ya kusonga mbele katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

NGOME YA AL AHLY YAVAMIWA NA YANGA

0

KIKOSI cha wachezaji 24 wa klabu ya Yanga kimeondoka leo kuelekea Cairo, Misri, kwa ajili ya mchezo muhimu wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya klabu kongwe barani Afrika, Al Ahly, unaotarajiwa kuchezwa Ijumaa.

Mabingwa hao wa Tanzania wanasafiri wakiwa na dhamira ya kuendelea kuandika historia katika michuano hiyo mikubwa ya Afrika, huku benchi la ufundi likiongozwa na Kocha Mkuu Pedro Goncalves likiwa na imani kubwa na kikosi kilichochaguliwa kwa pambano hilo gumu.

Katika nafasi ya walinda mlango, Yanga imesafiri na Djigui Diarra, Abuutwalibu Mshery pamoja na Hussein Masalanga

Safu ya ulinzi inaundwa na Bakari Mwamnyeto, Frank Assink, Israel Mwenda, Kibwana Shomari, Yao Kouassi, Ibrahim Bacca, Chadrack Boka na Mohamed Hussein, wakitarajiwa kuhimili mashambulizi ya Al Ahly.

Eneo la kiungo linaongozwa na nyota wenye uzoefu na ubunifu akiwemo Duke Abuya, Allan Okello, Mudathir Yahya, Mohamed Damaro, Maxi Nzengeli, Balla Conte.

Wengine ni  Shekhan Ibrahim, Lassine Kouma pamoja na Pacome Zouzoua, ambao wanategemewa kudhibiti mchezo na kuanzisha mashambulizi.

Upande wa ushambuliaji, Yanga imesafiri na Prince Dube, Laurindo Aurélio ‘Depu’ pamoja na Emmanuel Mwanengo, wakitarajiwa kuipa timu hiyo makali ya kusaka mabao muhimu ugenini.

Kwa ujumla, mchezo huo unatajwa kuwa wa presha kubwa kwa pande zote mbili, huku Yanga ikilenga kupata matokeo chanya yatakayoongeza nafasi zake katika hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu huu.

329,001FansLike
12,344FollowersFollow
16,900SubscribersSubscribe

EDITOR PICKS