Thursday, January 8, 2026
Home Blog Page 3

MZIZI WA FITNA NA WAPINZANI WAVUNJWA NA MPANZU

0

LICHA  ya tetesi nyingi zilizokuwa zikimzunguka kila dirisha la usajili, hatimaye kiungo Elie Mpanzu ametua na kujiunga na kikosi cha Simba kilichopo kambini Visiwani Zanzibar, hatua iliyowavunja matumaini waliodai hatorejea tena ndani ya Wekundu wa Msimbazi.

Kwa kipindi kirefu, jina la Mpanzu limekuwa likitajwa kuhusishwa na uwezekano wa kujiunga na Yanga, huku madai yakizidi kushika kasi kutokana na mkataba wake kubakiwa na muda wa miezi sita pekee. Hali hiyo ilizua sintofahamu kubwa miongoni mwa mashabiki wa Simba kuhusu mustakabali wa nyota huyo.

Hata hivyo, kurejea kwake kambini kumeonyesha msimamo tofauti, ambapo Mpanzu ameonesha dhamira ya kuendelea kuitumikia Simba na kupambana kwa ajili ya mafanikio ya timu hiyo katika michuano inayoendelea.

Nyota huyo aliwasili Zanzibar na kuungana moja kwa moja na kikosi, huku akionekana kuwa sehemu ya wachezaji waliokuwepo jukwaani jana usiku kushuhudia timu yake ikiibuka na ushindi dhidi ya Muembe Makumbi City katika Kombe la Mapinduzi.

Uwepo wake kambini umeongeza morali kwa wachezaji wenzake pamoja na benchi la ufundi, hasa ikizingatiwa uzoefu na mchango wake mkubwa katika kikosi cha Simba.

Mpanzu anatarajiwa kuwa sehemu ya kikosi kitakachoshuka dimbani katika mchezo ujao wa michuano hiyo dhidi ya Fufuni SC, unaotarajiwa kuchezwa kesho Jumatatu Januari 5, 2025 kwenye Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.

Kwa kurejea kwake, Mpanzu ameweka wazi kuwa bado ni sehemu ya Simba, akifunga mjadala uliokuwa unaendelea na kuwaacha mashabiki wakisubiri kwa hamu kuona mchango wake ndani ya uwanja katika michezo ijayo.

BAJEBER BADO ANAJITAFUTA

0

WAKATI mashabiki wa Simba  wakizidi kufurahishwa na mchango wa mshambuliaji wao, Mohammed Bajeber, nyota huyo ameweka wazi kuwa bado hajafikia kiwango chake cha juu cha ufiti.

Amesema  kuwa kile anachokionesha uwanjani ni sehemu ya safari ya kurejea kwenye ubora wake kamili.

Bajeber amesema licha ya kufanikiwa kuipatia Simba mabao mawili muhimu, moja katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara na lingine kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi, mechi hizo zimekuwa sehemu ya mchakato wake wa kurejesha makali baada ya kipindi kirefu cha majeraha.

Mshambuliaji huyo alijiunga na Simba SC katika dirisha kubwa la usajili akitokea nchini Kenya, bado hajarejea kikamilifu baada ya majeraha yaliyomuweka nje ya uwanja kwa muda.

Hata hivyo, baada ya kupona ameanza kupewa nafasi ya kucheza, akianza dhidi ya Mbeya City na kufunga bao lake la kwanza tangu atue ndani ya kikosi cha Wekundu wa Msimbazi.

Amesema mapumziko yaliyokuwepo kabla ya kurejea kambini yalikuwa na mchango mkubwa katika kumsaidia kujiandaa vyema, kwani aliyatumia kufanya mazoezi binafsi yaliyolenga kuongeza ufiti na kurejesha nguvu ya mwili.

Bajeber ameongeza kuwa michuano ya Kombe la Mapinduzi kwake ni fursa muhimu ya kuendelea kujipima na kujinoa zaidi, akitambua kuwa bado ana safari ndefu ya kufikia kiwango bora kinachotarajiwa na mashabiki pamoja na benchi la ufundi.

“Nilitumia mapumziko kufanya mazoezi yangu binafsi ili kujiweka fiti zaidi. Ingawa tayari nimerudi uwanjani, nimecheza mechi mbili na kufunga mabao ikiwemo dhidi ya Mbeya City na kwenye Kombe la Mapinduzi, bado natafuta ufiti wangu kamili,” amesema Bajeber.

mshambuliaji huyo amesema suala la kufikia ufiti wa asilimia 100 linahitaji subira na kumwachia Mungu, huku akibainisha kuwa licha ya matokeo mazuri yanayoonekana, kikosi bado kinaendelea kujijenga hasa ikizingatiwa kuwa benchi la ufundi ni jipya na bado linaendelea kutengeneza mwelekeo wa timu.

BAJEBER AJITAKATISHA NDANI YA ZANZIBAR

0

KIKOSI cha Simba kimeanza kwa kishindo michuano ya Kombe la Mapinduzi baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Muembe Makumbi City katika mchezo uliochezwa Uwanja wa New Amaan Complex, visiwani Zanzibar.

Ushindi huo umeipa Simba mwanzo mzuri katika mashindano hayo yanayoendelea kuvutia hisia za mashabiki wengi wa soka.

Bao pekee la ushindi kwa Simba lilifungwa na Mohamed Bajaber dakika ya 21 ya mchezo, akitumia vyema nafasi iliyotengenezwa na safu ya ushambuliaji ya Wekundu wa Msimbazi. Bao hilo lilikuja baada ya Simba kuonyesha utulivu na umakini mkubwa katika umiliki wa mpira.

Mchezo huo ulikuwa wa kwanza kwa Simba katika michuano ya Kombe la Mapinduzi, ambayo yalianza rasmi Desemba 28, 2025. Licha ya kuwa mchezo wa mwanzo, Simba ilionekana kuingia uwanjani ikiwa na malengo ya wazi ya kuanza kwa ushindi.

Katika kipindi cha kwanza, timu zote zilionyesha ushindani mkubwa huku Muembe Makumbi City ikijaribu kujibu mapigo kwa mashambulizi ya kushtukiza. Hata hivyo, safu ya ulinzi ya Simba ilionekana imara na kuzuia hatari nyingi zilizotengenezwa na wapinzani wao.

Dakika 45 za kipindi cha kwanza zilimalizika Simba ikiwa mbele kwa bao 1-0, matokeo yaliyoakisi ushindani mkali uliokuwepo uwanjani. Mashabiki waliujaza uwanja huo walishuhudia mchezo wenye kasi na nidhamu ya hali ya juu.

Kipindi cha pili kilishuhudia Simba ikiendelea kutawala umiliki wa mpira huku ikitafuta bao la kuongeza ili kujihakikishia ushindi wa mapema. Muembe Makumbi City nao hawakukata tamaa, wakiongeza nguvu katika safu ya ushambuliaji lakini bila mafanikio.

Kwa ushindi huo, Simba imejiweka katika nafasi nzuri kuelekea michezo inayofuata ya Kombe la Mapinduzi, huku benchi la ufundi likipata faraja ya kuona kikosi chake kikianza vyema mashindano hayo muhimu.

NDOTO ZAKO KUTIMIZWA NA MERIDIANBET LEO

0

Siku ya leo mechi kibao za pesa zinaendelea  ndani ya Meridianbet huku wakali wa ubashiri Meridianbet wanakwambia hivi mtafutaji hachoki, yaani ni mwendo wa kusaka ODDS KUBWA tuu na kubashiri. Ingia kwenye akaunti yako sasa na ubashiri leo.

SERIE A kule Italia mechi zinaendelea leo ambapo Como 1907 atamenyana dhidi ya Udinese Calcio ambao wanashika nafasi ya 11 huku wenyeji wao wakiwa nafasi ya 6. Tofauti ya pointi kati yao mpaka sasa ni 5. Je nani unampa nafasi ya ushindi siku ya leo?. Suka jamvi hapa.

Naye Juventus atakuwa nyumbani kusaka ushindi dhidi ya US Lecce ambao mpaka sasa wapo nafasi ya 16 kwenye msimamo wa ligi. Bibi Kizee yupo kwenye mbio za ubingwa msimu huu hivyo kila mechi ni kama fainali kwake. ODDS KUBWA zipo mechi hii. Bashiri hapa.

Na mechi kubwa Italia ni hii ya Atalanta vs AS Roma ambao nao msimu huu wameanza vyema kabisa. Ikumbukwe kuwa msimu uliopita kwenye mechi mbili za ligi walizokutana Roma walipoteza mechi zote mbili. Je mwenyeji kuendeleza ubabe mbele ya vijana wa Gasperini?. Tengeneza jamvi hapa.

Tajirika kwenye michezo ya Kasino ya mtandaoni kama vile Keno, Aviator, Poker, Roulette,Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Uingereza, EPL kuna mechi za kubeti ambapo Aston Villa vs Nottingham Forest ni mechi ambayo itakupa maokoto kibao. Vijana wa Unai wanahitaji ushindi huu kujiweka kwenye nafasi ya kushiriki michuano ya Ulaya msimu ujao. Odds kubwa ipo kwenye mechi hii. Bashiri hapa.

Mechi nyingine ni hii ya Brighton vs Burnley ambao wampenda daraja msimu huu wakiwa nafasi ya 19 ambayo ni ya pili kutoka mwisho. Mara ya mwisho wawili hawa kukutana, mechi zote mbili walitoa sare. Mwenyeji yeye yupo nafasi ya 14 kwenye msimamo wa ligi. Suka jamvi hapa.

Arsenal wao watakuwa ugenini kukipiga dhidi ya AFC Bournemouth ambao hawapewi nafasi ya ushindi kwenye mchezo wa leo. Ikumbukwe kuwa vijana wa Arteta wanahitaji ushindi huu kwa namna yoyote ile ili wajiweke kwenye nafasi nzuri ya kushinda ubingwa ligi kuu msimu huu. Je nani unampa nafasi ya kushinda leo?. Jisajili hapa.

LALIGA pia kule Hispania kuna mechi za pesa ambapo Osasuna atamenyana dhidi ya Athletic Bilbao ambao mpaka sasa wanashika nafasi ya 8 huku mwenyeji yeye akiwa nafasi ya 12. Meridianbet inakuambia kuwa nafasi ya kuondoka na ushindi ipo hapa. Unangoja nini sasa?. Tandika jamvi.

Pia Villarreal ambao wamekuwa na msimu mzuri wao watakuwa ugenini kukiwasha dhidi ya Elche ambapo mara ya mwisho walipokutana kwenye ligi, mwenyeji aliondoka na ushindi. Hivyo leo hii ni siku ya Nyambizi wa Njano kulipa kisasi kwa ODDS za kibabe na Meridianbet. Bashiri hapa leo.

Espanyol Barcelona atakuwa kibaruani kukipiga dhidi ya FC Barcelona ambao wanataka kutetea taji lao na msimu huu. Tofauti ya pointi kati yao hadi sasa ni 13 huku nafasi ya kushinda mechi hii akipewa Hans Flick na vijana wake. Beti hapa.

Ligi kuu ya Ufaransa inatarajiwa kuendelea kibabe ambapo AS Monaco atakipiga dhidi ya Lyon ambapo tofauti ya pointi kati yao hadi sasa ni 4 pekee. KIla timu inahitaji ushindi mkubwa leo iweze kusonga mbele kwenye nafasi inayofuata. Mechi hii pale Meridianbet imepewa machaguo zaidi ya 1000. Beti hapa.

Vilevile kwa upande wa Nice yeye atamenyana dhidi ya Strasbourg ambapo mechi ya mwisho kukutana hawa wawili walitoa sare ya mabao mawili mawili. Kila timu inahitaji ushindi siku ya leo. Wakali wa ubashiri, Meridianbet wanakwambia kuwa hii ni nafasi ya wewe kuondoka na mshindo. Tandika jamvi hapa.

YANGA YAANZA KOMBE LA MAPINDUZI KWA KUJIAMINI

0

KIKOSI cha Yanga kinatarajiwa kushuka dimbani kesho kuanza rasmi kampeni yake ya Mashindano ya Kombe la Mapinduzi kwa kuikabili KVZ, mchezo utakaochezwa katika Uwanja wa New Amaan Complex, visiwani Zanzibar.

Akizungumza kuelekea mchezo huo wa ufunguzi, Kocha Mkuu wa Yanga, Pedro Goncalves, amesema maandalizi waliyoyafanya yamelenga kujenga msingi imara wa ushindani katika kila mechi watakayocheza kwenye mashindano hayo, huku akisisitiza umuhimu wa nidhamu na mshikamano wa kikosi.

Pedro amekiri kuwa kikosi chake kitakabiliwa na changamoto ya kuwakosa baadhi ya wachezaji muhimu, lakini amesema hilo halitapunguza morali wala malengo ya timu katika mashindano hayo.

Ameeleza kuwa Yanga bado ina wachezaji wa kutosha wenye uwezo wa kupambana na timu yoyote, akibainisha kuwa nguvu kubwa ya kikosi hicho ipo kwenye mshikamano, nidhamu ya mchezo na utekelezaji wa maelekezo ya benchi la ufundi.

“Kesho tunaanza rasmi mashindano haya na tumekuja kupambana kwa dhati. Ni kweli tunawakosa baadhi ya wachezaji muhimu, lakini bado tuna kikosi imara cha kushindana,” amesema Pedro.

Kocha huyo ameongeza kuwa Kombe la Mapinduzi ni jukwaa muhimu pia kwa wachezaji wapya wa klabu hiyo kupewa nafasi ya kuonesha uwezo wao na kuanza kuielewa falsafa ya Yanga.

“Sio jambo rahisi mara moja, linahitaji kuchukuliwa hatua kwa hatua. Kupitia mashindano haya naamini wachezaji wetu wapya watapata nafasi ya kujifunza na kutuonyesha kile walichonacho,” amesema Pedro.

GATES OF HALLOWEEN KUJA NA FURSA MERIDIANBET

0

Baada ya shamrashamra za Halloween kupita, msisimko wake bado unaendelea kuishi ndani ya Meridianbet. Kupitia mchezo wa kasino mtandaoni Gates of Halloween, wachezaji wanaingia kwenye dunia ya kipekee iliyojaa mandhari ya kusisimua, burudani ya hali ya juu, na nafasi nyingi za kushinda.

Mchezo huu umejengwa kwa mantiki ya kuendelea mbele. Unapopata alama nane au zaidi, ushindi wako hufunguliwa na safari inaendelea bila kusimama. Kila ushindi huleta mzunguko mpya wa alama, hivyo kukupa nafasi ya kuongeza matokeo yako mara kadhaa ndani ya raundi moja.

Mbali na mchezo huu, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kinachovutia zaidi ndani ya Gates of Halloween ni uwezo wake wa kutoa ushindi mkubwa kutoka kwenye dau la kawaida. Vizidishi vikubwa vinavyoweza kufikia hadi mara 1000 hufanya kila mzunguko uwe nafasi ya kipekee ya kubadilisha bahati yako.

Kwa wachezaji wanaopenda zawadi za ziada, alama maalum huleta mizunguko ya bure bila kuongeza dau, huku kipengele cha Bonus Buy kikitoa uhuru wa kupata nafasi hizo mapema. Kupitia Gates of Halloween, Meridianbet inaendelea kuonyesha kwa nini ni chaguo sahihi kwa mashabiki wa kasino mtandaoni Tanzania. Jisajili leo, burudika na uanze safari yako ya ushindi.

MFUNGAJI BORA MALAWI KUTUA MSIMBAZI

0

KLABU ya Simba imefikia hatua za mwisho za mazungumzo na mabingwa wa Malawi, Nyasa Big Bullets, kwa lengo la kunasa saini ya winga mahiri Chikumbutso Salim maarufu kama Chiku Salim katika dirisha dogo la usajili.

Taarifa za ndani zinaeleza kuwa pande zote mbili zimeridhiana kwa kiasi kikubwa, huku kilichobaki kikiwa ni kukamilisha taratibu chache kabla ya mchezaji huyo kutangazwa rasmi kuwa mali ya Wekundu wa Msimbazi.

Salim amekuwa kwenye kiwango bora msimu huu baada ya kuonyesha makali yake katika Ligi Kuu ya Malawi, akicheza jumla ya mechi 28 na kufanikiwa kufunga mabao 15 pamoja na kutoa asisti 11, rekodi inayomweka miongoni mwa wachezaji hatari zaidi kwenye ligi hiyo.

Kwa mujibu wa takwimu hizo, nyota huyo alifanikiwa pia kuibuka kuwa mfungaji bora  wa Ligi ya Malawi hadi kufikia Desemba 27, jambo lililovutia macho ya klabu kadhaa barani Afrika, lakini Simba ikaonekana kuwa mbele zaidi katika mbio za kumsajili.

Ujio wa Salim unatajwa kuwa sehemu ya mkakati wa Simba kuimarisha safu ya ushambuliaji, hasa eneo la winga, kuelekea nusu ya pili ya msimu na mashindano ya ndani pamoja na yale ya kimataifa.

Iwapo dili hilo litakamilika kama inavyotarajiwa, Salim ataungana na kikosi cha Simba akitarajiwa kuongeza ushindani, kasi na ubunifu katika safu ya mbele.

HATMA YA AHOUA MIKONONI MWA BARKER

0

WAKATI  dirisha dogo la usajili likiwa limefunguliwa, Kocha mpya wa Simba, Steve Barker, ameweka msimamo wake wazi kwa kuutaka uongozi wa klabu hiyo kutokurupuka kufanya usajili wala kuuza wachezaji hadi atakapokamilisha tathmini yake ya kikosi.

Barker amesema anahitaji muda wa kutosha kuwatazama wachezaji waliopo kikosini ili kupata picha halisi ya ubora, udhaifu na mahitaji ya timu, kabla ya kufanya maamuzi yoyote muhimu yanayohusu mabadiliko ya kikosi.

Kocha huyo anazitumia vyema mashindano ya Kombe la Mapinduzi yanayoendelea Visiwani Zanzibar kama jukwaa la kufanya tathmini ya kina kwa wachezaji wake, akilenga kubaini aina ya wachezaji anaohitaji kwa falsafa na mfumo wake wa uchezaji.

Kupitia mashindano hayo, Barker anatazamia kuona uwezo wa wachezaji katika mazingira ya ushindani, jambo litakalomsaidia kufanya maamuzi sahihi kuhusu nafasi zinazohitaji kuimarishwa ndani ya kikosi cha Wekundu wa Msimbazi.

Hata hivyo, taarifa zinaeleza kuwa kuna baadhi ya wachezaji waliopo kwenye orodha ya wanaoweza kuuzwa, akiwemo Jean Charles Ahoua, ambaye inadaiwa anawindwa na klabu ya Raja AC ya Morocco.

Raja AC inanolewa na aliyekuwa Kocha wa Simba, Fadlu Davids, hali inayoongeza uzito wa tetesi hizo, ingawa bado hakuna uamuzi rasmi uliotolewa kuhusu mustakabali wa kiungo huyo.

Chanzo cha ndani kimeeleza kuwa uongozi wa Simba umeamua kumuachia Barker jukumu zima la kuishauri klabu kuhusu usajili, ili kuhakikisha maamuzi yatakayofanyika yanazingatia mahitaji halisi ya timu na malengo ya muda mrefu ya klabu hiyo.

MAROUF RASMI KUITUMIKIA JANGWANI

0

KIUNGO mpya wa Yanga, Marouf Tchakei, ameanza rasmi safari yake ndani ya kikosi cha Wananchi baada ya kuwa sehemu ya timu iliyowasili visiwani Zanzibar kwa ajili ya michuano ya Kombe la Mapinduzi linaloendelea kutimua vumbi.

Tchakei bado hajatambulishwa  na Yanga, amesajiliwa kwa mkopo akitokea Singida Black Stars kufuatia makubaliano maalum kati ya klabu hizo mbili, hatua inayolenga kuimarisha kikosi cha timu hiyo katika kipindi hiki cha mashindano.

Nyota huyo anatarajiwa kuanza kuonekana uwanjani mapema, akitajwa kuwa sehemu ya kikosi kitakachocheza mchezo wa kesho dhidi ya KVZ, utakaopigwa katika Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.

Ujio wa Tchakei unaongeza nguvu mpya katika safu ya kiungo ya Yanga, benchi la ufundi chini ya kocha Pedro Gocalves ana matumaini kuwa atasaidia kuongeza ushindani, ubunifu na uimara katika michezo ya mashindano yaliyopo mbele yao.

Mbali na Kombe la Mapinduzi, Yanga inamwangalia Tchakei kama sehemu ya mpango mpana wa kuhakikisha timu inafanya vizuri pia katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara pamoja na mashindano mengine ya msimu huu.

Akizungumza kuhusu maandalizi ya kikosi, Ofisa Habari wa Yanga, Ali Kamwe, amesema timu imeondoka ikiwa na wachezaji wote waliopo nje ya majukumu ya timu ya taifa pamoja na nyota wao wapya waliosajiliwa.

Kamwe ameeleza kuwa wachezaji wapya wataanza kuonekana katika michuano ya Kombe la Mapinduzi, akisisitiza kuwa usajili uliofanywa umezingatia mahitaji ya benchi la ufundi na malengo ya muda mfupi na mrefu ya klabu hiyo.

0

Mwanzo wa mwaka mpya huja na kiu ya burudani yenye hisia za tofauti, na Sweet Holiday Chase imechukua nafasi hiyo kwa kugeuza mapumziko kuwa tamasha la msisimko. Hii ni kampeni inayochanganya kasi, furaha na hisia za ushindi, ikitoa ladha ya ushindi wa zaidi ya TSh 14,500,000,000/-

Ndani ya Sweet Holiday Chase, kila mshiriki anaalikwa kwenye dimba moja. Zawadi hutolewa kwa mwendelezo, kila wiki ikipewa msisitizo wake, na kila mzunguko ukiwa kama nafasi ya kusukuma mashambulizi. Hakuna kigezo cha ukubwa wa dau, falsafa yake ni wazi, burudani ya kweli ni ile inayotoa nafasi kwa kila mmoja.

Utajiri wako upo kwenye michezo ya Kasino siku ya leo ingia na ucheze Poker, Keno, Roulette, Aviator, Superheli na ukusanye maokoto zaidi na zaidi. PIGA *149*10# AU tembelea tovuti yao meridianbet.co.tz kubashiri mechi zote.

Uzoefu huu unajengwa juu ya urahisi na mtiririko. Kushiriki hakuhitaji maandalizi marefu, bali ni sehemu ya mwendo wa kawaida wa burudani. Mfumo unafanya kazi kimya kimya, ukiwaacha washiriki wafurahie michezo huku fursa zikiendelea kujitokeza bila presha.

Kinachotofautisha Sweet Holiday Chase ni hisia ya mshangao. Zawadi huja wakati wowote, kama bao la kushtukiza linalobadilisha mwelekeo wa mchezo. Ni mwendo wa pasi za haraka, nafasi zinazotokea ghafla, na shangwe inayozuka pale usipotarajia.

Kwa ujumla, Sweet Holiday Chase ni zaidi ya promosheni, ni simulizi la msimu. Kuanzia zawadi za papo kwa papo hadi uwezekano wa ushindi mkubwa, Meridianbet imeunda mazingira yanayofanya mwanzo wa mwaka uanze kwa ladha ya ushindi.

329,001FansLike
12,344FollowersFollow
16,900SubscribersSubscribe

EDITOR PICKS