Home Uncategorized MAPILATO WA AZAM FC NA LIPULI LEO HAWA HAPA

MAPILATO WA AZAM FC NA LIPULI LEO HAWA HAPA



Hance Mabena leo atakuwa mwamuzi wa kati kwenye mchezo wa fainali ya kombe la Shirikisho FA utakaochezwa uwanja wa Ilulu, Lindi majira ya saa 9:00 alasiri.


Mabena atasaidiwa na Mohamed Mkono kutoka Tanga, mwamuzi msaidizi namba moja, Frednarnd Chacha kutoka Mwanza, mwamuzi msaidizi namba 2, na Abubakar Mturo kutoka Mtwara atakuwa ni mwamuzi wa akiba.

Waamuzi wasaidizi walioteuliwa kukaa kwenye magoli ni Martin Sanya kutoka Morogoro na Florentina Zablon kutoka Dodoma huku mtathmini wa waamuzi akiwa ni Lesile Liunda kutoka Dar es Salaam na kamishna wa mchezo ni Salum Kurunge kutoka Geita.

SOMA NA HII  PONGEZI ZA DHATI KWA WACHEZAJI SIMBA ZATOLEWA