Uncategorized

SEPETU: WACHEZAJI WALITUANGUSHA AFCON, LEO HAPANA, MASHABIKI TUJITOKEZE

admin July 28, 2019 2:35 am

WEMA Sepetu, shabiki mkubwa wa timu ya Taifa ya Tanzania na mjumbe wa kamati ya uhamasishaji wa timu ya Taifa amewaomba watanzania kujitokeza kwa wingi kwenye mchezo wa leo kati ya timu ya Taifa ya Tanzania na Kenya huku akiwataka wachezaji wasiliangushe Taifa.

Sepetu amesema kuwa alipata furaha kubwa timu ilipofuzu michuano ya Afcon ila iliyeyuka kama barafu baada ya wachezaji kuboronga nchini Misri.

“Nilifurahi sana nilipoona timu ya Taifa letu imefuzu michuano ya Afcon ila sasa walipofuzu sijui bahati mbaya sijui ilikuaje walituangusha sasa katika hili basi wasituangushe hawa kaka zetu.

“Ninajua watanzania wanapenda mpira hivyo tujitokeze kwa wingi kuipa sapoti timu ya Taifa na ombi langi kwa wachezaji wasituangushe,” amesema.

Stars leo itashuka uwanja wa Taifa kumenyana na timu ya Kenya majira ya saa 10:00 jioni.

SIMBA YAWEKA MEZANI MILIONI 10 KWA AJILI YA KELVIN YONDAN, METACHA MNATA, JUMA KASEJA MWANAMICHEZO AZIM DEWJI AZIDI KUTENGAMAA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6131

Leave a Reply