KIUNGO Mshambuliaji wa Simba, Ibrahim Ajibu amesema kuwa kilichomkibiza TP Mazembe ni maslahi kwani dau alilowekewa na timu hiyo lilikuwa la kishkaji.
Mazembe walikuwa wakiisaka saini ya nyota huyo ambaye kwa sasa ni mali ya Simba akiwa amesaini kandarasi ya miaka miwili.
Akizungumza na Saleh Jembe, Ajibu amesema kuwa mchezaji siku zote ni sawa na mfanyabiashara anachoangalia ni maslahi kwanza mambo mengine yatafuata.
“Suala la kuachana na dili la Mazembe ishu kubwa ni maslahi, mchezaji ni mfanyabiashara kitu kikubwa cha kuangalia ni faida, hivyo dau ambalo niliwekewa na Simba ni kubwa kuliko lile la Mazembe,” amesema Ajibu.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.