Home Uncategorized ILE ISHU KWAMBA EMMANUEL OKWI ANAREJEA SIMBA, IKIWEZEKANA MCHONGO UKO HIVI….

ILE ISHU KWAMBA EMMANUEL OKWI ANAREJEA SIMBA, IKIWEZEKANA MCHONGO UKO HIVI….




Mshambuliaji wa zamani wa Simba, Mganda, Emmanuel Okwi ambaye hivi karibuni alitangaza kuachana na klabu hiyo, kuna uwezekano mkubwa akarejea tena kikosini hapo kuendelea kuitumikia timu hiyo.


Ikumbukwe kuwa, hivi karibuni Okwi aligoma kuongeza mkataba wa kuitumikia Simba baada ya kushindwana katika suala zima na fedha na hivi karibuni ikaripotiwa kuwa amejiunga na timu ya Fujairah FC ya Falme za Kiarabu (UAE).


Hata hivyo, habari za kuaminika kutoka ndani ya Simba ambazo Championi Jumatano limezipata zimedai kuwa dili hilo la Okwi la kujiunga na Fujairah limeingia doa, hivyo yupo katika mchakato wa kurudi Simba.


Mmoja wa viongozi wa Simba ambaye hakutaka kutajwa jina lake, alisema kuwa uongozi pia umeonekana kukubaliana na suala hilo.


“Baada ya Okwi kugoma uongozi ulikuwa na mpango wa kumsajili mshambuliaji wa Nkana ya Zambia, Walter Bwalya lakini mpango huo uliingia doa baada ya timu ya El Gouna FC ya nchini Misri kutuzidi kete kwa kutoa dau kubwa mara mbili zaidi yetu, wakamsajili.


“Baada ya hapo nguvu zetu tukazielekeza kwa mshambuliaji wa Orlando Pirates ya nchini Afrika Kusini, Justin Shonga, lakini kabla hatujakaa sawa Al Ahly ya Misri pia wakaingilia dili hilo na kutangaza kumsajili kwa fedha nyingi zaidi ya zile za kwetu.


“Kutokana na hali hiyo hatukuwa na jinsi ikibadi turudi kwa Okwi ambaye kwa sasa mazungumzo yanaenda vizuri kabisa na tunataka kumsajili kwa mkataba wa mwaka mmoja, kwa hiyo kama ulisikia kuna sapraizi inakuja basi anaweza kuwa Okwi,” kilisema chanzo hicho cha habari.


Hata hivyo, alipotafutwa Mtendaji Mkuu wa Simba, Crescentius Magori kuzungumzia hilo hakupatikana lakini taarifa ambazo gazeti hili lilizipata zimedai kuwa hawataki kulizungumzia hilo kwa sasa.

SOMA NA HII  HATMA YA SIMBA IPO KWA MKAPA UONGOZI WAFUNGUKA HAYA KUHUSU WYDAD