Kocha wa zamani wa klabu ya Simba, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ ameshangaa kutokuona watanzania wakipewa nafasi ya kuifundisha Taifa Stars.
Kauli ya Julio imekuja siku chache mara baada ya Kocha Mrundi Ettiene Ndayiragije kuchaguliwa kukaimu nafasi ya Emmanuel Amunike aliyekuwa akiinoa timu hiyo.
Julio amemtaja Abdallah King Kibadeni kuwa mmoja wa makocha ambao wana heshima kuwa katika soka la Tanzania akipendelea wapewe nafasi hiyo.
Kocha huyo mwenye maneno mengi anaamini Kibadeni ambaye aliwahi kuinoa na kuichezea Simba pia anafaa kuinoa Stars kwa heshima aliyoiweka Tanzania .
“Nashangaa kwanini wazawa hawapewi nafasi.
“Tuna watu wengi ikiwemo King Kibadeni ambaye anaweza akachukua nafasi hiyo na akaifundisha Stars.”
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.