NYOTA wote wakali ndani ya Yanga leo kuonyesha maajabu bure uwanja wa Jamhuri Morogoro kwenye mchezo wa kukata na shoka wa kirafiki kati ya Yanga na Mawenzi Market.
Mchezo huu wa kipekee ambao ni maalumu kwa ajili ya maandalizi ya ligi msimu ujao utashuhudia mambo mengi ikiwa ni pamoja na zawadi za kutoksha kutoka kwa waandaaji ambao ni Faith Baptist Church (FBC).
Upekee wa mchezo wa leo ni kwamba baada ya kipindi cha kwanza muda wa mapumziko kutakuwa na neno la Mungu pamoja na zawadi ya vitabu ambavyo vitagawiwa bure na hakutakuwa na kiingilio pia kushuhuida mchezo wa leo.
Nyota wakali kama Mrisho Ngassa, Juma Balinya, Farouk Shikalo, Patrick Sibomana bila kumsahau nahodha Papy Tshishimbi wote watakuwa ndani ya uwanja kutoa zawadi ya burudani ya kukata na shoka bure kwa mashabiki.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.