Home Uncategorized MATOLA: AKIPATIKANA MDHAMINI MKUU, MSIMU UJAO UTANOGA

MATOLA: AKIPATIKANA MDHAMINI MKUU, MSIMU UJAO UTANOGA

SELEMAN Matola Kocha wa Polisi Tanzania amesema kuwa msimu ujao utakuwa na ushindani mkubwa endapo atapatikana mdhamini mkuu.

Akizungumza na Saleh Jembe, Matola amesema kuwa kwa sasa mambo bado hayajakaa sawa kutokana na kutopatikana mdhamini  mkuu.

“Bado kwa sasa mambo hayajakaa sawa, endapo mdhamini mkuu atapatikana itasaidia kuleta ushindani na kila mmoja ataona namna ligi itakavyokuwa bora hivyo itapendeza kama mdhamnini atapatikana.

“Msimu uliopita mambo hayakuwa mazuri kwa timu nyingi kutokana na hali ya ukata hivyo ni muda wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuliangalia suala hili mapema,” amesema.

SOMA NA HII  AZAM FC YAKOMAA NA JAMBO LAO