Home Uncategorized NYOTA WA YANGA AMALIZANA NA ALLIANCE FC

NYOTA WA YANGA AMALIZANA NA ALLIANCE FC

JERSON Tegete nyota wa zamani wa kikosi cha Yanga na Kagera Sugar msimu ujao atakuwa ndani ya uzi wa Alliance FC ya Mwanza.

Uongozi wa Alliance umesema kuwa Tegete ni pendekezo la Kocha Mkuu wa kikosi hicho, Athuman Bilali baada ya kukubali uwezo wa nyota huyo.

Tegete amesaini kandarasi ya miaka miwili hivyo msimu ujao ataitumikia timu yake mpya ya Alliance.

SOMA NA HII  VITA YA KUWANIA SAINI YA NYOTA WA SIMBA NA TP MAZEMBE NI BALAA