OFISA Habari wa Simba, Haji Manara amesema kuwa hawana hofu na mchezo wao watakaocheza jumanne siku ya Simba day mashabiki wa Simba wanajua wanachokitaka.
Agosti sita Simba itacheza uwanja wa Taifa na timu ya Power Dynamo mchezo wa kirafiki wenye lengo la kuwatambulisha wachezaji wake wapya na wale wa muda mrefu.
“Haijalishi itakuwa ni jumanne watu wanasema hawatakuja watu sisi tunajua kwamba wana Simba wanapenda kuiona timu yao hivyo nawaomba wanasimba wanunue tiketi mapema ili kupunguza ule msongamano wa kujazana siku ya mwisho.
“Tumejipanga tunajua kwamba watu wanataka kumuona Kahata, wale Wabrazili pia wote watakuwwepo bila kumsahau Meddie Kagere, na wachezaji wengine wote, ni wakati wetu wa kutamba sasa,” amesema.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.