Home Uncategorized WAGENI 100 WAIGOMBANIA NAFASI YA AMMUNIKE, WAZAWA WAICHUNIA

WAGENI 100 WAIGOMBANIA NAFASI YA AMMUNIKE, WAZAWA WAICHUNIA

WILFRED Kidao, Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) amesema kuwa mpaka sasa tayari wamepokea maombi ya makocha 100 wanaotaka nafasi ya kuinoa timu ya Taifa.

Katika orodha hiyo hakuna hata jina moja la mzawa ambaye ameomba kuinoa timu ya Taifa ya Tanzania baada ya 
Kocha Mkuu Emmanuel Ammunike  kusitishiwa mkataba wake baada ya kuboronga kwenye michuano ya Afcon 2019 nchini Misri.

 “Tumepokea maombi ya makocha zaidi ya 100 wakitaka kazi ya kuifundisha timu ya Taifa, maombi ni mengi na tunayafanyia kazi.

 “Kwa sasa nguvu zeru tunazielekeza kwenye michuano ya Chan na kwenye maombi hayo 100 hakuna mzawa hata mmoja,” amesema.

SOMA NA HII  KIKOSI CHA SIMBA DHIDI YA KMC MCHEZO WA KIRAFIKI