Home Uncategorized BLUE KUKUSANYA KIJIJI LEO MBAGALA, KUPIGA SHOO YA KIBABE MFANO HAKUNA

BLUE KUKUSANYA KIJIJI LEO MBAGALA, KUPIGA SHOO YA KIBABE MFANO HAKUNA

 MSANII nguli kwenye muziki wa Bongo fleva, Mr. Blue amesema kuwa leo atatoa burudani ambayo haina mfano kwenye ukumbi wa Taifa wa Burudani Dar Live uliopo Mbagala Zakhem.

Blue amepanga kufanya mambo makubwa leo na anaamini mashabiki hawatajuta kufika Dar Live kwa kuwa atafanya shoo ambayo itakuwa sapraiz kwa mashabiki wote watakaojitokeza.
“Shoo zangu mzee hazitabiriki. Nimejiandaa vya kutosha kwa hiyo niwaombe tu mashabiki wajitokeze kwa wingi kwani nitagonga ngoma baada ya ngoma. Njooni Dar Live tujimwageee,” amesema Mr. Blue.
Wakali hao walipata pia fursa ya kutembelea studio za +255 Global Radio na kuzungumza mengi waliyopania kuhusiana na tamasha hilo ambalo linawakutanisha kwa mara ya kwanza pamoja na Hamisa Mobeto, uchakavu mdogo tu wa 5,000.
SOMA NA HII  HAPA NDIPO TATIZO LA YANGA LILIPOJIFICHA