Home Uncategorized KMC WAANZA KUIVUTIA KASI COASTAL UNION, WACHEZAJI LEO KULA BATA

KMC WAANZA KUIVUTIA KASI COASTAL UNION, WACHEZAJI LEO KULA BATA


BAADA ya kuanza kwa kuchechemea ndani ya Ligi Kuu Bara inayodhaminiwa na Vodacom kwa kufungwa bao 1-0 dhidi ya Azam FC uwanja wa Uhuru, leo wachezaji wa KMC wamepewa mapumziko.

KMC iliyo chini ya Jackson Mayanja itajitupa tena uwanjani Septemba 18 itamenyana na Coastal Union ya Tanga ambayo nayo pia ilipoteza mchezo wake wa kwanza mbele ya Polisi Tanzania.

Akizungumza na Saleh Jembe, Anwary Binde, Ofisa Habari wa KMC amesema kuwa leo wachezaji wamepewa mapumziko wataendelea na mazoezi kesho hivyo kama wataamua kula bata kazi ni kwao.

“Wachezaji wamepewa mapumziko wataendelea na mazoezi kesho kama kawaida uwanja wa Bora,” amesema.

SOMA NA HII  LEICESTER CITY YAZIKAZIA MANCHESTER CITY NA UNITED KWA BEKI WAO