Home Uncategorized KOCHA STARS: LEO KENYA HAWATOKI, TUPO TAYARI KUPATA MATOKEO CHANYA

KOCHA STARS: LEO KENYA HAWATOKI, TUPO TAYARI KUPATA MATOKEO CHANYA


ETIENNE Ndayiragije, Kaimu Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ amesema kuwa nafasi ni kubwa kushinda mbele ya Kenya leo.

Stars ipo Kenya kwa ajili ya mchezo wa marudio dhidi ya Kenya kwa ajili ya michuano ya Chan na ni lazima Stars kupata ushindi baada ya kupata sare ya bila kufungana uwanja wa Taifa ili kuoata nafasi ya kusonga mbele.

“Makosa ambayo tulifanya awali tayari tumeyafanyia kazi na wachezaji wanajua kwa sasa wana kazi moja ya kupata ushindi mbele ya Kenya.

“Tutacheza kwa hesabu kali bila kuwa na presha kama mwanzo kwani kikosi kwa sasa kina utulivu na kimejengeka katika misingi ya kutafuta ushindi,” amesema.

SOMA NA HII  SABABU YA TANZANIA PRISONS KUHAMISHIA MAKAZI YAO UWANJA WA NELSON MANDELA, RUKWA HII HAPA