BAKARI Shime ‘Mchawi Mweusi’ Kocha Mkuu wa kikosi cha Timu ya Taifa ya Wanawake chini ya miaka 20 ‘Tanzanite’ amesema kuwa kesho watafanya kweli.
Tanzanite kwa sasa ipo nchini Afrika Kusini kwa ajili ya michuano ya COSAFA ambayo imeanza kutimua vumbi leo.
“Kila kitu kinakwenda sawa na wachezaji wamepewa majukumu kwa ajili ya mashindano haya ambayo tumealikwa hivyo ni muda wa watanzania kuwa na imani na sisi,” amesema.
Leo kikosi kimefanya mazoezi kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wa kwanza kesho dhidi ya Botswana utakaochezwa Uwanja wa Gelvandale,Port Elizabeth,Afrika Kusini.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.