Home Uncategorized MSUVA AIPA AHUENI STARS BURUNDI, MECHI YAMALIZIKA 1-1

MSUVA AIPA AHUENI STARS BURUNDI, MECHI YAMALIZIKA 1-1


Taifa Stars imelazimisha suluhu ya bao 1-1 dhidi ya Burundi katika mchezo wa kufuzu kucheza michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2022 huko Qatar.


Stars iliyokuwa ugenini ilianza kuruhusu nyavu zake kuguswa mnamo dakika ya 80 kupitia kwa Amiss Cedric baada ya kuwapiga chenga mabeki Stars na kupiga shuti ambalo lilimuacha Juma Kaseja akiwa hana cha kufanya.

Ilichukua dakika tano pekee kwa Simon Msuva kuweza kurejesha bao kupitia mpira wa KAUNTA ATAKI ambayo alimalizia vema langoni mwa Burundi baada ya kipa wao na beki kujichanganya.

Ushindi huo unawapa nafasi ya kufanya vema Stars ambao watakuja kucheza tena na Burundi kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
SOMA NA HII  SAKATA LA KOCHA WA YANGA KURUDI BONGO LIMEFIKIA HAPA, NI NDANI YA SPOTIXTRA JUMAPILI