Home Uncategorized BEKI WA MANCHESTER UNITED ASHINIKIZA KUSEPA MAZIMA

BEKI WA MANCHESTER UNITED ASHINIKIZA KUSEPA MAZIMA


BEKI wa Manchester United, Ashley Young imeripotiwa kuwa amegomea mazoezi ya timu yake akishinikiza kutimkia ndani ya kikosi cha Inter Milan.
Young amekubali kujiunga na Inter Milan inayoshiriki Serie A akitokea kwenye timu inayoshiriki Ligi Kuu England na anatarajia kufanyiwa vipimo hivi karibuni kukamilisha dili hilo.
Imeripotiwa kwamba nyota huyo hafurahishwi na maisha yake ndani ya Manchester United na mabosi wa Inter Milan wameweka mezani pauni milioni 15 kuipata saini yake.
Nyota huyo amegomea dili la kuongeza mkataba wa mwaka mmoja ndani ya United na anahitaji kuondoka kwenye usajili wa mwezi Januari licha ya mkataba wake kumeguka mwishoni mwa msimu.
SOMA NA HII  KUBWA KULIKO KUTIKISA JUMAMOSI DAR, RATIBA KAMILI HII HAPA – VIDEO