ADAM Salamba, mtanzania anayekipiga kwa sasa ndani ya timu ya Al-Jahra SC, iliyopo Uarabuni amesema kuwa ushirikiano anaopewa na wachezaji wenzake ni mkubwa.
Akizungumza na Saleh Jembe, Salamba amesema kuwa amekuwa akifurahia maisha ya huko kutokana na ushirikiano anaopewa na wachezaji wenzake.
“Huku ninaishi vizuri na wenzangu, tunashirkiana vema na kila mchezaji jambo ambalo linanifanya niwe na furaha.
“Nafanya yote kutokana na kupenda kazi yangu, nipo huku ila napeperusha vema bendera ya Tanzania kwani wengi wanapenda kutambua habari za nyumbani,” amesema Salamba.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.