NAHODHA wa Simba, John Bocco amesema kuwa kesho watambana mbele ya Biashara United ili kupata pointi tatu muhimu.
Simba itaikaribisha Biashara United, Februari 22, Uwanja wa Taifa mchezo wa ligi wa pili kwa mzunguko wa pili.
Bocco amesema: “Ni mchezo wetu mgumu kutokana na ushindani uliopo, tunawaheshimu wapinzani wetu kwani ni timu nzuri ambayo tutakutana nayo ila nasi pia tupo vizuri tutapambana ili kupaya pointi tatu muhimu mashabiki watupe sapoti,” amesema.
Bocco ana mabao matatu ndani ya ligi kwa msimu huu wa 2019/20 na pasi moja ya bao.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.