Home Uncategorized COASTAL UNION YASIMULIA ILIVYOIBANA YANGA MKWAKWANI

COASTAL UNION YASIMULIA ILIVYOIBANA YANGA MKWAKWANI


JUMA Mgunda, Kocha Mkuu wa Coastal Union amesema kuwa walitambua uimara wa wapinzani wao Yanga jambo lililowafanya wapambane kutafuta matokeo licha ya kuambulia sare ya bila kufungana.

Coastal Union ilikaza mbele ya Yanga, jana Februari 23 kwa kuzuia mashambulizi ya wapinzani wao wanaoongozwa na nyota wao Bernard Morrison raia wa Ghana.

“Tulitambua mchezo wetu utakuwa mgumu ukizingatia kwamba wapinzani wetu walitoka kupata sare nasi tulitoka kupoteza makosa yetu tuliyafanyaia kazi, nawapongeza wachezaji katika hilo,”.

Coastal Union imeambulia pointi moja mbele ya Yanga, kwenye mchezo wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Uhuru, Yanga ilishinda bao 1-0 na kusepa na pointi tatu jumla.

SOMA NA HII  AUBA ACHEKELEA KUTWAA MATAJI MAWILI ULAYA