HARUNA Harerimana, Kocha Mkuu wa KMC amesema kuwa wachezaji wake leo wanatakiwa kufuata malekezo yake mwanzo mwisho ili kushinda mbele ya Ndanda FC.
KMC ilikubali kichapo cha mabao 2-1 mbele ya Namungo mchezo uliochezwa Uwanja wa Majaliwa, leo watamenyana na Ndanda Uwanja wa Nangwanda Sijaona.
“Wachezaji wangu wamekuwa na tatizo la kushindwa kufuata maelekezo kipindi cha kwanza jambo ambalo limefanya tuwe na kazi ya kuelekezana kipindi cha pili.
“Nimegundua kwamba tatizo lao ni kushindwa kuelewa na kufanya yale ambayo nimewaambia mwanzo na nina amini watarekebisha makosa yao,” amesema.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.