Home Uncategorized SIMBA YAZITAKA POINTI TATU ZA KMC

SIMBA YAZITAKA POINTI TATU ZA KMC


UONGOZI wa Simba umesema kuwa umejipanga kuona unapata matokeo mbele ya KMC kwenye mchezo wa kesho utakaochezwa Uwanja wa Taifa majira ya saa 1:00.

Kocha Mkuu wa Simba, Sven Vandnbroeck amesema kuwa anatambua mchezo utakuwa mgumu ila anaamini watapata pointi tatu.

“Kila kitu ni hatua na kwa sasa ambapo tupo sio sehemu mbaya tunahitaji kuona tunapata matokeo mazuri yatakayotufanya tuzidi kuwa imara,” amesema.

Simba inaongoza ligi ikiwa imecheza mechi 24 na ina pointi 62.

SOMA NA HII  DULLA MBABE AENDELEA UBABE WAKE AMNYOOSHA MCHINA, JUMATATU KUREJEA BONGO