UONGOZI wa Yanga umesema kuwa umejipanga kusepa na pointi tatu leo mbele ya Alliance kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara utakaochezwa Uwanja wa Taifa.
Ofisa Habari wa Yanga, Hassan Bumbuli amesema kuwa kikosi kipo tayari na wachezaji wana morali kubwa ya kusaka ushindi.
Bumbuli amesema:”Tumekuwa tukiambiwa wanyonge kutokana na matokeo ambayo tumekuwa tukiyapata hilo hatulijali kwa kuwa ubora wetu tunautambua na hatubahatishi tupo imara.
“Baada ya kumalizana na Gwambina sasa kazi inayofuata itakuwa dhidi ya Alliance, tupo tayari kuona tunapata ushindi kikubwa tunachotaji pointi tatu, mashabiki watupe sapoti,”.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.