Home Uncategorized WILDER AMFUKUZA KOCHA ALIYETUPA TAULO ULINGONI, KOCHA MKUU AMRUKA

WILDER AMFUKUZA KOCHA ALIYETUPA TAULO ULINGONI, KOCHA MKUU AMRUKA


WILDER AKIJIFUA NA BRELAND


Jay Deas ambaye Kocha Mkuu wa bondia Deotnay Wilder amesema alimkataza msaidizi wake Mark Breland ambaye ni bingwa wa zamani wa dunia kutupa taulo ulingoni wakati Wilder akichakazwa na Tyson Fury katika raundi ya saba ya pambano la uzito wa juu.


Wilder ametangaza kumfuta kazi Breland akisisitiza alivunja makubaliano kwa kuwa walishakubaliana tokea mwanzo, hata apigwe vipi, yeye ni shujaa na mpambanaji na asingependa suala la kurushwa taulo hadi mwisho.


Deas amesema alimkataza Brealand kufanya hivyo hata kama Wilder alikuwa akipigwa vipi lakini hakusikia na kuamua kurusha taulo hiyo iliyomaliza pambano katika ukumbiwa MGM Grand Arena nchini Marekani.


Kwa sasa mabondia hao wako katika harakati za kuangalia kama wanaweza kuwa na pambano la marudiano likiwa la tatu kwa kuwa la kwanza walitoka sare na la pili, Fury kutoka Uingereza akashinda kwa TKO katika raundi ya saba.
SOMA NA HII  MESSI APATWA KIGUGUMIZI KUMZUNGUMZIA ANTONIE