Home Uncategorized CR 7 KUMBE AMEHUSIKA KICHAPO CHA BARCELONA YA MESSI MBELE YA REAL...

CR 7 KUMBE AMEHUSIKA KICHAPO CHA BARCELONA YA MESSI MBELE YA REAL MADRID


LIONEL Messi nahodha wa Barcelona hakuwa na ujanja mbele ya wapinzani wake Real Madrid zaidi ya kushuhudia wakichapwa mabao 2-0 mchezo wao wa La Liga.

Mabao ya Real Madrid yalifungwa na Vinicius Junior dakika ya 71 na lile la pili lilipachikwa na Mariano dakika ya 90+2 .


Junior amesema kuwa walipata muda wa kuzungumza na nyota wa Juventus, Cristiano Ronaldo muda wa mapumziko aliwapa mbinu zilizowasaidia kuwapa matokeo.

Ushindi huo unaifanya Real Madrid iwe nafasi ya kwanza kwenye msimamo ikiwa na pointi 56 kibindoni ndani ya La Liga.

Barcelona wao wapo nafasi ya pili wakiwa na pointi 55 kibindoni na zote zimecheza mechi 26.

Barcelona imepoteza mechi tano huku Madrid ikiwa imepoteza mechi mbili.

SOMA NA HII  VPL: COASTAL UNION 0-5 SIMBA