Home Uncategorized HIKI HAPA KIKOSI CHA MAUAJI CHA YANGA KITAKACHOANZA DHIDI YA SIMBA LEO...

HIKI HAPA KIKOSI CHA MAUAJI CHA YANGA KITAKACHOANZA DHIDI YA SIMBA LEO TAIFA

KIKOSI cha Yanga kinachotarajiwa kuanza leo dhidi ya Simba, leo Machi 8, Uwanja wa Taifa kwa mujibu wa CHAMPIONI Jumatano na sababu zake zatajwa:-

Kipa: Farouk Shikalo, uzoefu unambeba alikuwa langoni kwenye dabi ya Januari 4, Uwanja wa Taifa, Simba 2-2 Yanga.

Beki wa Kulia: Juma Abdul inaonyesha amerejea kwenye ubora wake kwa sasa na amekuwa imara.

Beki wa Kushoto: Jafary Mohamed, kipenzi cha Kocha Mkuu, Luc Eymael.

Beki wa Kati, Lamine Moro, uwezo wa mghana huyu unaimarika kila iitwapo leo akiwa uwanjani.

Beki wa Kati: Kelvin Yondani, bado uzoefu wake unambeba licha ya kutokuwa kwenye mechi za hivi karibuni.

Kiungo Mkabaji: Papy Tshishimbi, alikuepo kwenye dabi ya Januari 4, uzoefu unambeba

Kiungo Mchezeshaji: Haruna Niyonzima, uzoefu na kasi yake vinambeba.

Winga: Balama Mapinduzi, mshuti wake bado unaishi, wengi wanatarajia kuona maajabu kwake

Mshambuliaji:- Tariq Seif, Amecheza mechi tatu za hivi karibuni akimuweka benchi, David Molinga mbele ya Coastal Union, Gwambina, Alliance

Mshambuliaji wa Kati: Ditram Nchimbi, mwili wenye nguvu na mishuti mikali, anapewa nafasi ya kuanza akiwa amefunga abao mawili ndani ya Yanga

Winga: Bernard Morrison, kiungo mshambuliaji raia wa Ghana kipenzi cha mashabiki ana nafasi ya kuanza jumla kwenye kikosi cha kwanza kutokana na uimara wake.


SOMA NA HII  MTAMBO WA MABAO KUTUA YANGA..MAMBO YOTE YAPO HIVI..!!!