Home Uncategorized KOCHA WA SIMBA AWAKOMALIA WACHEZAJI WAKE KUPIGA MATIZI

KOCHA WA SIMBA AWAKOMALIA WACHEZAJI WAKE KUPIGA MATIZI


SVEN Vandenbroeck, Kocha Mkuu wa Simba amesema kuwa hakuna muda wa kupumzika kwa wachezaji wake lazima waendelee kupambana kufanya mazoezi

Mechi za Simba zimeahirishwa kutokana na wachezaji wake kuitwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa kinachojiaanda na michuano ya Chan ikiwa ni pamoja na Jonas Mkude, John Bocco, Erasto Nyoni, Hassan Dilunga, Shomari Kapombe,Mohamed Hussein ‘Tshabalala’, Aish Manula.

“Hakuna muda wa kupumzika kwa wachezaji ambao wamebaki kwa sasa licha ya kwamba wengine wamejiunga na timu ya Taifa ni lazima wafanye mazoezi ili kuwa bora,”.

Simba inaongoza ligi ikiwa na pointi 71 mchezo wake unaofuata utakuwa dhidi ya Ruvu Shooting.

SOMA NA HII  SIMBA WAMFUATA NTIBAZOKIZA,FARID AGOMEA JEZI YAKE NI NDANI YA SPOTI XTRA JUMANNE