Home Uncategorized MASHABIKI WAITWA KUICHEKI U 17 BURE KABISA

MASHABIKI WAITWA KUICHEKI U 17 BURE KABISA

BAKARI Shime, Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Wanawake chini ya miaka 17 amesema kuwa kikosi kipo tayari kuwavaa Uganda hivyo mashabiki wajitokezekwa wingi uwanja wa Taifa.

Leo Uwanja Taifa saa tisa kamili pambano hilo litaanza huku kiingilio kwa upande wa VIP A ikiwa  buku 2,VIP B na C Buku moja na mzunguko ni bure kabisa.

“Kila kitu kipo sawa wachezaji wana morali kubwa na tunaamini tutafanya vizuri hivyo mashabiki wajitokeze kwa wingi,” amesema.

Mchezo wa leo ni maalumu kwa ajili kukata tiketi ya kufuzu Kombe la Dunia litakalofanyika mwaka huu nchini India.

SOMA NA HII  JPM AWALILIA WAFANYAKAZI 5 WA AZAM TV WALIOFARIKI WAKIELEKEA CHATO