Home Uncategorized SIMBA: TUNAZITAKA POINTI TATU ZA YANGA

SIMBA: TUNAZITAKA POINTI TATU ZA YANGA

BEKI Kisiki wa Simba, Pascal Wawa amesema kuwa wanapiga hesabu kubwa kuona namna gani watashinda mchezo wao mbele ya Yanga utakaochezwa Machi 8,2020 Uwanja wa Taifa.
 Wawa amesema kuwa kila mchezo wanaocheza wanahitaji ushindi na wanaamini kwamba utakuwa mchezo mgumu ila watapambana kupata matokeo Machi 8.
Akizungumza na Saleh Jembe, Wawa amesema :”Hatuna muda wa kupumzika kwa sasa kazi ni kubwa na kila mechi tunaitazama kwa umuhimu wake, mechi yetu ya Yanga itakuwa ngumu ila tunazitaka pointi tatu,”. 

Simba ikiwa imefunga mabao 55 amehusika kwenye pasi moja ya bao licha ya kuwa ni beki alimpa psi hiyo Meddie Kagere kwenye mchezo dhidi ya Alliance wakati Simba ikishinda mabao 4-1.
SOMA NA HII  BREAKING: MUKOKO MCHEZAJI BORA MWEZI OKTOBA NDANI YA LIGI KUU BARA