Home Uncategorized SIMBA: YANGA WALITUOTEA KUTUCHAPA BAO 1-0

SIMBA: YANGA WALITUOTEA KUTUCHAPA BAO 1-0


CLATOUS Chama, raia wa Zambia anayekipiga ndani ya Simba anaamini kuwa Klabu ya Yanga iliwaotea Machi 8 Uwanja wa Taifa kwa kuwachapa bao 1-0.

Chama ambaye ni kiungo mguuni ana mabao mawili na ametoa pasi saba za mwisho za mabao ndani ya Simba alikuwa ndani ya kikosi kilichoambulia kipigo hicho.

Kwa sasa Simba ipo nafasi ya kwanza kwenye ligi ambayo imesimamishwa kwa muda wa mwezi mmoja na ina pointi zake 71. 


“Nadhani kwetu kupoteza mchezo dhidi ya Yanga ilikuwa bahati mbaya na huenda hatukuwa vizuri sana ndio maana wakatuotea,”.

Mchezo wa kwanza uliochezwa Januari 4 Simba ililazimisha sare ya kufungana mabao 2-2 na mchezo wa pili ilikubali kufungwa bao 1-0 dakika ya 44.

SOMA NA HII  NAMUNGO HESABU ZAO NDANI YA LIGI KUU BARA