Home Uncategorized WAWILI SASA NDANI YA JUVENTUS WATHIBITISHWA KUWA NA CORONA

WAWILI SASA NDANI YA JUVENTUS WATHIBITISHWA KUWA NA CORONA

KIUNGO Blaise Matuidi anayekipiga Juventus ya Italia inayoshiriki Serie A amepatikana na ugonjwa wa Corona.

Klabu yake ya Juventus imethibitisha hilo na kumfanya afikishe idadi ya wachezaji sita ambao wana virusi vya Corona ndani ya Italia.


Raia huyo wa Ufarasa ambaye alishinda Kombe la Dunia alikuwa ameshawekwa kwenye uangalizi maalumu tangu Machi 11 na kwa sasa anaendelea vizuri.

 Matuad mwenye miaka 32 anakuwa mchezaji wa pili ndani ya Juve kungulika na virusi vya Corona wa kwanza alikuwa ni Daniele Rugani aliyegundulika wiki iliyopita. Kwa sasa masuala yote ya michezo ndani ya Italia yamesimaishwa mpaka Aprili 3.
.
SOMA NA HII  IBRAHIM AJIBU KWA SIMBA NDO BASI TENA MSIMU WA 2019/20