Home Uncategorized BEKI YANGA AKUBALI UWEZO WA MTUPIAJI NAMBA MOJA WA SIMBA

BEKI YANGA AKUBALI UWEZO WA MTUPIAJI NAMBA MOJA WA SIMBA


ALLY Mtoni.’Sonso’ beki wa kati wa Klabu ya Yanga amesema kuwa miongoni wa mabeki ambao anawakubali ndani ya Bongo ni pamoja na Meddie Kagere anayekipiga ndani ya Simba.

Sonso amekuwa bora msimu wake wa kwanza ndani ya Yanga iliyo chini ya Kocha Mkuu Luc Eymael ambaye amekuwa akimuamini na kumpa nafasi ya kuanza kikosi cha kwanza.

Kwa sasa Ligi Kuu Tanzania Bara imesimamishwa kutokana na maambukizi ya Virusi vya Corona.

Mtoni amesema:”Miongoni mwa washambuliaji ambao ninakubali uwezo wao wakiwa ndani ya uwanja kwenye ligi ya Bongo ni pamoja na Kagere anajitahidi kupambana na anafanya kazi yake vizuri,”.

Kagere ni kinara wa kutupia ambapo kwa sasa ametupia mabao 19 ndani ya Ligi Kuu Bara na ana pasi tano kati ya mabao 63 yaliyofungwa na Simba.

SOMA NA HII  NYOTA SABA KUJIUNGA LEO NA TIMU YA TAIFA, MMOJA TAARIFA ZAKE HAZIFAHAMIKI