Home Uncategorized KAKOLANYA ACHEKELEA MAISHA NDANI YA SIMBA

KAKOLANYA ACHEKELEA MAISHA NDANI YA SIMBA

BENO Kakolanya, mlinda mlango namba mbili wa Simba amesema kuwa anafurahia maisha anayoishi ndani ya kikosi hicho cha mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Ligi kwa sasa imesimamishwa na Serikali kutokana na maambukizi ya Virusi vya Corona ambavyo ni janga la dunia.

Kakolanya amesema:”Nipo ndani ya Simba kwa sasa ninafurahia maisha yangu kwa kuwa ni miongoni mwa timu bora na kuna ushirikiano mkubwa kuanzia kwa viongozi pamoja na wachezaji achilia mbali sapoti ambayo tunaipata kutoka kwa mashabiki,” .

Simba ikiwa imecheza mechi 28, Kakolanya amekaa kwenye mechi saba za ligi msimu huu.

SOMA NA HII  MTUPIAJI NAMBA MOJA MZAWA ANAPATA TABU KWELI