Home Uncategorized KOCHA LIGI KUU AHOFIA WACHEZAJI KUSHUKA VIWANGO LIGI IKIREJEA

KOCHA LIGI KUU AHOFIA WACHEZAJI KUSHUKA VIWANGO LIGI IKIREJEA


ZUBER Katwila, Kocha Mkuu wa Mtibwa Sugar amesema kuwa iwapo wachezaji watashindwa kuendelea kufanya mazoezi wakati huu wa mapumziko kupisha Virusi vya Corona endapo Ligi Kuu Tanzania Bara itarejea wengi watakuwa wanaweza shuka viwango.

Kwa sasa Ligi Kuu imesimamishwa na Serikali ambapo tamko hilo lilitolewa Machi 17 na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa inatarajia kurejea iwapo hali itakuwa shwari.

Katwila amesema:”Iwapo wachezaji watashindwa kufanya mazoezi wakati huu itakuwa ngumu kurejea kwenye ubora wao iwapo ligi itarejea.

“Kikubwa ambacho wanapaswa kukifanya kwa sasa ni kufuata program ambazo wamepewa na makocha wao itawasaidia kulinda vipaji vyao,” .

SOMA NA HII  MBAO FC YAINYOOSHA SIMBA MABAO 3-2 TAIFA DAR