Home Uncategorized LIVERPOOL YAJIPANGA KUMREJESHA NYOTA WAO WA ZAMANI STERLING WA CITY

LIVERPOOL YAJIPANGA KUMREJESHA NYOTA WAO WA ZAMANI STERLING WA CITY


IMERIPOTIWA kuwa timu ya Liverpool ipo kwenye mpango wa kumrejesha nyota wao wa zamani Raheem Sterling anayekipiga ndani ya Manchester City pamoja na timu ya Taifa ya England.

Nyota huyo alitimka ndani ya Liverpool mwaka 2015 Kwa dau la pauni milioni 49 alikuwa amecheza mechi 95 na kufunga mabao 18.

Sterling mwenye miaka 25 hakuwa tayari kuzungumzia suala hilo kwenye mahojiano na kituo kimoja licha ya kukiri kuwa anaipenda timu hiyo.


Msimu huu wa 2019/20 amecheza mechi 24 za Ligi Kuu England amefunga mabao 11 na ametoa pasi moja ya bao huku akiwa ameonyeshwa kadi tano za njano.

SOMA NA HII  SIMBA MSIMU UJAO MCHEZAJI MMOJA KUCHEZA ZAIDI YA NAFASI MOJA, MIFUMO MPAKA MITATU