Home Uncategorized MTIBWA SUGAR YAKUMBUKA KASI YA LIGI KUU BARA

MTIBWA SUGAR YAKUMBUKA KASI YA LIGI KUU BARA

UONGOZI wa Mtibwa Sugar umesema kuwa miongoni mwa vitu ambavyo unavikumbuka kwa sasa ni pamoja na ushindani wa Ligi Kuu Bara uliokuwa umeanza kushika kasi ila hawana la kufanya zaidi ya kuchukua tahadhari.

Kwa sasa Ligi Kuu Bara imesimamishwa na Serikali ili kuchukua tahadhari dhidi ya maambukizi ya Virusi vya Corona ambavyo ni janga la dunia kwa sasa.

Akizungumza na Saleh Jembe, Ofisa Habari wa Mtibwa Sugar, Thobias Kifaru amesema kuwa ni ngumu kusahau ile kasi ya ligi ilivyokuwa lakini hakuna chaguo.

“Ilikuwa ni kasi nzuri ambayo ilikuwa imeanza kushika lakini kutokana na janga hili la Virusi vya Corona hakuna namna ni lazima tukubali kufuata utaratibu.

“Kila mmoja anakumbuka namna ushindani ulivyokuwa mkubwa lakini ninapenda kusema kuwa kwa sasa wote tunapaswa tuwe ni kitu kimoja kupambana na Virusi vya Corona,” amesema.

Mtibwa Sugar ipo nafasi ya 14 ikiwa na pointi 33 kibindoni ina pointi 33.

SOMA NA HII  SIMBA WAPINZANI WAKE NI KUTOKA NIGERIA, MIAMBA HII RAUNDI YA AWALI HAIWAHUSU