Home Uncategorized NYOTA WA KARIOBANGI AKUBALI KUTUA YANGA KIROHO SAFI

NYOTA WA KARIOBANGI AKUBALI KUTUA YANGA KIROHO SAFI


YIDAH Sven kiungo anayekipiga ndani ya Klabu ya Kariobangi Sharks amesema kuwa yupo tayari kuibukia ndani ya Klabu ya Yanga iwapo utaratibu utafuatwa.

Mkataba wa nyota huyo anayekipiga nchini Kenya unameguka msimu huu pale ligi inapomeguka.


Sven amekuwa akihusishwa kujiunga na Klabu ya Yanga yenye maskani yake mitaa ya Karikaoo.

“Mkataba wangu ndani ya klabu yangu hapa unameguka msimu utakapoisha ila ikitokea klabu ya Yanga ikafuata utaratibu nipo tayari kujiunga nayo kwani kazi yangu mimi ni mpira,” amesema.

SOMA NA HII  WACHEZAJI SIMBA WAGOMA KISA MPUNGA