Home Uncategorized ARSENAL YAMVUTIA KASI BEKI WA AJAX

ARSENAL YAMVUTIA KASI BEKI WA AJAX

INAELEZWA kuwa Klabu ya Arsenal ipo kwenye hesabu za kuwania saini ya nyota anayekipiga ndani ya Klabu ya Ajax, Nicolas Tagliafico.

Nyota huyo mwenye miaka 27 amemvutia Kocha Mkuu wa Arsenal, Mikel Arteta ambaye anahitaji kuboresha kikosi chake.

Arteta anahitaji kuimarisha safu ya ulinzi ambapo jina la beki huyo linatajwa kuwa kwenye rada zake.

Akiwa ndani ya Ajax beki huyo amecheza jumla ya mechi 68 na ametupia mabao sita.

SOMA NA HII  ASTON VILLA YAMALIZANA NA KIPA WA ARSENAL